Msaada: Maana ya ndoto hii

Diwani

JF-Expert Member
Oct 25, 2014
2,672
2,697
Bila Shaka mu wazima wa Afya. Mungu mkubwa.

Mpaka wakati huu naandika 'Post' hii, nimekuwa natafakari nilichoota usiku wa kuamkia leo. Si ndoto ya kutisha, La hasha, lakini imefanya nitafakari sana, nadhani yeyote angetafakari kama angelitilia maanani.

Ni hivi; Mazingira niliyootea yana mandhari ya Shule, naam, shule, na ni katika ngazi ya Elimu ya Upili ya Sekondari, yaani 'Advanced', katika eneo ambalo, linaakisi Mazingira yasiyo ya mjini, Pasi na shaka ni kijijini, au mji unaokuwa hivi sasa. Kwa kuweka sawa, elimu hii nilisoma mkoani Ruvuma, hivyo najaribu kupafananisha na mazingira niliyootea.

Basi bwana, katika eneo moja, la ninchodhani ni shule, tulikuwa kwenye foleni ndefu, inafanana na foleni ya chakula, sina hakika mbeleni kilikuwa kinatolewa kitu gani, sikumbuki, ila nahisi kwa 80% ni chakula.

Nafasi yangu haikuwa nyuma sana, wala mbele sana na zoezi lilipokuwa likiendendelea, lakini kwenye mstari huo hapakukosa stori za hapa na pale na wale waliosimama mbele na nyuma yangu, nikiangalia mstari, Alhmadullilah, ulionyesha nakaribia kufika, nikigeuza kichwa niendelee na soga na wale mabwana, ambao kwa maumbile na namna walivyo ukilinganisha na tulichokuwa tukizungumza iliashiria kwamba ni Wanafunzi, kisha niangalie tena mbele nilikuta foleni inazidi kuwa ndefu, na pale zoezi lilipokuwa likiendendelea pako mbali na macho yangu.

Nilisimama kwenye foleni tu, sina kumbukumbu vizuri, kama wale niliokuwa napiga nao soga awali, ndio hawa hawa niliowakuwa nao wakati yote yakiendelea, lakini hali hii ya kukaribia kwenye 'Lile zoezi' na kukuta mbele watu wamejaa zaidi.

Basi katika tukio moja nalokumbuka ni kwamba, kuna bwana alijaribu kujipenyesha kwenye mstari, nadhani ni kama mtu wa pili kutoka nyuma yangu hivi, alisemwa yule bwana, alisakamwa, ikambidi aepuke lile nongwa, akakaa pembeni akingoja. Hiki ni kati ya kisa nakikumbuka kwenye ile ndoto.

Karibuni kwa Msaada wa Ufasiri.

images%20-%202023-03-21T065238.442.jpg
 
Hii sio ndoto...hii ni nightmare.

Unatakiwa ujue kuna hatua kadhaa mpaka kuota ndoto.

1. Dream 2. Vision 3. NightMare

Vitu hivi vyote hutokea wakati mtu akiwa amelala usingizi au amelala fofo.

Physically miili yetu huwa inaota moto, lakini spiritually roho zetu huwa zinaota upepo au kupunga upepo.

Ndo maana wazee wetu walikua wanapenda sana kutuwashia moto katikati ya uwanja...tuuote kabla ya kwenda kulala ili tuwe na ndoto njema. Na wengine walidiriki kuweka dawa kwenye moto ili tuepukane na nightmares au tuzipate nightmares kwà maana tujikute au tujione tunacheza ngoma , kimbizwa, etc

Kiufupi...hiyo iliyoiota sio ndoto....ni nightmare
 
Japokuwa hujasema hali yako ya maisha kwa sasa ikoje...I mean unasoma, unafanya kazi, biashara na kipato chako kipoje, kuota upo shule wakati ulishamaliza shule siku nyingi maana yake ni "kurudishwa nyuma" kuwa kwenye foleni ambayo haufiki maana yake ni "kucheleweshwa" ukichukua maana ya kwanza (kurudishwa nyuma + Kucheleweshwa) utagundua kuwa kuna nguvu zinapambana na wewe ktk kile unachokifanya sasa, chukua taadhari na mwombe sana Mungu akuvushe!! kitu chochote kinachotokea kwa mtu huanza ktk ulimwengu wa "roho" then matokeo yake huonekana ktk ulimwengu wa mwili
 
Japokuwa hujasema hali yako ya maisha kwa sasa ikoje...I mean unasoma, unafanya kazi, biashara na kipato chako kipoje, kuota upo shule wakati ulishamaliza shule siku nyingi maana yake ni "kurudishwa nyuma" kuwa kwenye foleni ambayo haufiki maana yake ni "kucheleweshwa" ukichukua maana ya kwanza (kurudishwa nyuma + Kucheleweshwa) utagundua kuwa kuna nguvu zinapambana na wewe ktk kile unachokifanya sasa, chukua taadhari na mwombe sana Mungu akuvushe!! kitu chochote kinachotokea kwa mtu huanza ktk ulimwengu wa "roho" then matokeo yake huonekana ktk ulimwengu wa mwili
Umemaliza yote nyongeza tu ni kuwa amerudishwa nyuma katika harakati za kushirikiana kusaka riziki""maana ya chakula katika ndoto ni ushirikiano
 
Mimi pia hunikut tofauti yan kam nikistuka mida ya alfajir kam saa 10 kuanzia hapo afu nitoke nje usingiz ukatok na nikirud ndan kulal tena naota ndoto ambayo ikij kiuhalisia inakuj inversely proportional ( kinyume ) chake nakile nilicho kiota
 
Hii sio ndoto...hii ni nightmare.

Unatakiwa ujue kuna hatua kadhaa mpaka kuota ndoto.

1. Dream 2. Vision 3. NightMare

Vitu hivi vyote hutokea wakati mtu akiwa amelala usingizi au amelala fofo.

Physically miili yetu huwa inaota moto, lakini spiritually roho zetu huwa zinaota upepo au kupunga upepo.

Ndo maana wazee wetu walikua wanapenda sana kutuwashia moto katikati ya uwanja...tuuote kabla ya kwenda kulala ili tuwe na ndoto njema. Na wengine walidiriki kuweka dawa kwenye moto ili tuepukane na nightmares au tuzipate nightmares kwà maana tujikute au tujione tunacheza ngoma , kimbizwa, etc

Kiufupi...hiyo iliyoiota sio ndoto....ni nightmare
Bado sijajua haswa, tofauti ya vitu hivi viwili, nadhani nitajifunza zaidi maana nilidhani awali nightmare ni ndoto za kuogofya labda.
 
Japokuwa hujasema hali yako ya maisha kwa sasa ikoje...I mean unasoma, unafanya kazi, biashara na kipato chako kipoje, kuota upo shule wakati ulishamaliza shule siku nyingi maana yake ni "kurudishwa nyuma" kuwa kwenye foleni ambayo haufiki maana yake ni "kucheleweshwa" ukichukua maana ya kwanza (kurudishwa nyuma + Kucheleweshwa) utagundua kuwa kuna nguvu zinapambana na wewe ktk kile unachokifanya sasa, chukua taadhari na mwombe sana Mungu akuvushe!! kitu chochote kinachotokea kwa mtu huanza ktk ulimwengu wa "roho" then matokeo yake huonekana ktk ulimwengu wa mwili
Sawa, naweka sawia. Kuhusu hali yangu ya maisha kwa sasa, naweza kusema, mali/amali pekee niliyonayo ni Uhai, kiuchumi ambayo ni funguo ya hali nyingine ni Mbaya, Yes, hali ni Mbaya ukifananisha na miaka miwili iliyopita. Ambayo kimsingi nilikuwa kazini, kwa sasa sina kazi, yaani naingia huku na kule tu ili mradi nipate rizki.

Kuhusu nguvu inayonirudisha nyuma 'Nahisi' ni kweli, wala hujakosea, kuna background kwa watu wangu wa karibu, nikimaanisha Ukoo, Familia, Marafiki na Majirani ambayo si nzuri, labda ufafanuzi wako, na hisia zangu zinaweza kuwa jibu kamili. Hili, nalifanyia kazi.
 
Sawa, naweka sawia. Kuhusu hali yangu ya maisha kwa sasa, naweza kusema, mali/amali pekee niliyonayo ni Uhai, kiuchumi ambayo ni funguo ya hali nyingine ni Mbaya, Yes, hali ni Mbaya ukifananisha na miaka miwili iliyopita. Ambayo kimsingi nilikuwa kazini, kwa sasa sina kazi, yaani naingia huku na kule tu ili mradi nipate rizki.

Kuhusu nguvu inayonirudisha nyuma 'Nahisi' kuna background kwa watu wangu wa karibu ambao si nzuri, labda ufafanuzi wako, na hisia zangu zinaweza kuwa jibu kamili. Hili, nalifanyia kazi.
Mimi nimeota kuna ndugu yetu mmoja ananikabidhi maburungutu ya Pesa yamejaa kwenye briefcase, sasa sijajua ndoto itatimia au itayeyuka Ila nmeota leo saa 9 usiku
 
Bado sijajua haswa, tofauti ya vitu hivi viwili, nadhani nitajifunza zaidi maana nilidhani awali nightmare ni ndoto za kuogofya labda.
Nightmare ni mizimu, mambo yanayokujulisha matukio mbalimbali ya kimaisha.Chakula ni riziki, kipato na mema yeyote.foleni ni mipango matarajio zamu na mfumo wa kutafuta.Kuongezeka kwa foleni ni hali ya kuharibiwa mipango au riziki pindi tu unapoikaribia.

Kisha ukaoneshwa mtu anaeharibu na kuingilia kila unapokaribia kuipata na si kwako pekee huvuruga na kwa wengine pia.Yeye na wenzie kama wapo wanakufuatilia sana na wanahakikisha ukipata tu wanatibua.Wakati mwingine uanafunzi ni mafunzo na maisha.
 
Nightmare ni mizimu, mambo yanayokujulisha matukio mbalimbali ya kimaisha.Chakula ni riziki, kipato na mema yeyote.foleni ni mipango matarajio zamu na mfumo wa kutafuta.Kuongezeka kwa foleni ni hali ya kuharibiwa mipango au riziki pindi tu unapoikaribia.
Kisha ukaoneshwa mtu anaeharibu na kuingilia kila unapokaribia kuipata na si kwako pekee huvuruga na kwa wengine pia.Yeye na wenzie kama wapo wanakufuatilia sana na wanahakikisha ukipata tu wanatibua.Wakati mwingine uanafunzi ni mafunzo na maisha.
 
Na mimi nimeota ndoto mji flani mimi na mke wangu lakini baadae simwonj mara ghafla upepo ufanano na tetemeko lakini unazoa mchanga na kama lile la jangwani unafunika watu na tunakimbia wengine nyumba zinaanguka wakiwa ndani wanashika nguzo zake lakini wanafunikwa na mchanga na mimi nikawa nakwepa mpaka nikajikuta niko mji mwingine nikiwa na mama na mwanamke fulani akatupokea nikasema huku kuko salama yule mama akasema hapana hali hii utokea alipo maliza tu kusema vile upepo ukaanza kuvuma na tulikuwa kwake ambapo pamezungukwa na miti mirefu na mawe makubwa yaliyobebana nyumba zipo katikati.

Tukiwa nje tunapiga story hizo ghafla mti ulikatika na kuja usawa wangu nikapangua mara jiwe kubwa likajadiliwa usawa wangu kunisaga lakini nikashanga limenikosa na kupita pembeni tkaoaombia ndani ila mimi nikibaki nje mvua ikaanza kunyesha nikawa nimejikinga chini ya paa la nyumba baadae niliona naingia jikoni na kuwaiuta mama na yule mama wanapika basi nikakaa ndoto ikaisha.
 
Na mimi nimeota ndoto mji flani mimi na mke wangu lakini baadae simwonj mara ghafla upepo ufanano na tetemeko lakini unazoa mchanga na kama lile la jangwani unafunika watu na tunakimbia wengine nyumba zinaanguka wakiwa ndani wanashika nguzo zake lakini wanafunikwa na mchanga na mimi nikawa nakwepa mpaka nikajikuta niko mji mwingine nikiwa na mama na mwanamke flani akatupokea nikasema huku kuko salama yule mama akasema hapana hali hii utokea alipo maliza tu kusema vile upepo ukaanza kuvuma na tulikuwa kwake ambapo pamezungukwa na miti mirefu na mawe makubwa yaliyobebana nyumba zipo katikati. Tukiwa nje tunapiga story hizo ghafla mti ulikatika na kuja usawa wangu nikapangua mara jiwe kubwa likajadiliwa usawa wangu kunisaga lakini nikashanga limenikosa na kupita pembeni tkaoaombia ndani ila mimi nikibaki nje mvua ikaanza kunyesha nikawa nimejikinga chini ya paa la nyumba baadae niliona naingia jikoni na kuwaiuta mama na yule mama wanapika basi nikakaa ndoto ikaisha
aisee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom