Msaada kwenye jambo hili,linanitatiza kidogo

Msaada kwenye jambo hili,linanitatiza kidogo

Jack Daniel

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
4,058
Reaction score
16,927
Wasalaam.

Hii ni Kwa wanaume wenzangu japo hata akina dada,mama mnaweza toa ushauri.

Iko hivi,

Juzi, yaani jumamosi,
Nilijichanganya kwa kuhisi nimepotelewa na kifaa changu ndani cha muhimu mno,yaani mno.

Sasa kumbe kuna mtu aliniazima na Mimi nikasahau kabisa kuwa nimeazimisha Mtu.

Basi katika kutafutatafuta na kukosa ,tuhuma zote nikazielekeza Kwa kijana wangu,ambaye muda mwingi sikai naye kwani huwa anaishimkoani anakosoma.

Basi nilitoa maneno yoooote mabaya,huku mwanangu akikataa hajahusika ,nikamsogelea nikamtikisa kama kutaka kumpiga, lakini kijana akapiga magoti huku akidai hajachukua kifaa kile.kwani Hana kazi nacho.

Kwahiyo tangu juzi tumekaa Kwa kukwepana huku nikiamini kijana kapoteza kifaa changu,

Chaajabu jioni hii saa 11 nimeletewa kifaa na mtu niliyekuwa nimemuazima huku akishukuru kwakuwa kimemsaidia mno ,ni takribani wiki tatu zimepita tangu aazime.

Sasa ,najikuta mwenye hatia,mwanangu nimemuonea,natamani hata nimuombe msamaha,je, inawezekana kumuomba msamaha mwanao wa kumzaa?

Majibu yenu tafadhali.
 
Kumpa amani pia kwako ni heri umuombe msamaha, Muite pembeni kwa utulivu sana kisha ongea kumuomba msamaha...hii itampatia amani zaidi. Usipofanya hivyo hatokaa asahau kamwe tukio hilo wala kuachilia, ataweka hiyo kitu moyoni mpaka anakufa.

MUOMBE MSAMAHA TU.
 
Wasalaam.

Hii ni Kwa wanaume wenzangu japo hata akina dada,mama mnaweza toa ushauri.

Iko hivi,

Juzi, yaani jumamosi,
Nilijichanganya kwa kuhisi nimepotelewa na kifaa changu ndani cha muhimu mno,yaani mno.

Sasa kumbe kuna mtu aliniazima na Mimi nikasahau kabisa kuwa nimeazimisha Mtu.

Basi katika kutafutatafuta na kukosa ,tuhuma zote nikazielekeza Kwa kijana wangu,ambaye muda mwingi sikai naye kwani huwa anaishimkoani anakosoma.

Basi nilitoa maneno yoooote mabaya,huku mwanangu akikataa hajahusika ,nikamsogelea nikamtikisa kama kutaka kumpiga, lakini kijana akapiga magoti huku akidai hajachukua kifaa kile.kwani Hana kazi nacho.

Kwahiyo tangu juzi tumekaa Kwa kukwepana huku nikiamini kijana kapoteza kifaa changu,

Chaajabu jioni hii saa 11 nimeletewa kifaa na mtu niliyekuwa nimemuazima huku akishukuru kwakuwa kimemsaidia mno ,ni takribani wiki tatu zimepita tangu aazime.

Sasa ,najikuta mwenye hatia,mwanangu nimemuonea,natamani hata nimuombe msamaha,je, inawezekana kumuomba msamaha mwanao wa kumzaa?

Majibu yenu tafadhali.
Muombe haraka sana asije weka chuki nafsini
 
Kumpa amani pia kwako ni heri umuombe msamaha, Muite pembeni kwa utulivu sana kisha ongea kumuomba msamaha...hii itampatia amani zaidi. Usipofanya hivyo hatokaa asahau kamwe tukio hilo wala kuachilia, ataweka hiyo kitu moyoni mpaka anakufa.

MUOMBE MSAMAHA TU.
Vipi mkuu, umesharudi kutoka mwanza na passo yako?

Au bado unainjoy samaki
 
Duh!! Mkuu unauliza kuomba msamaha kwa mtoto uliye mzaa wewe!? Mimi nilishawahi kuadhibu mwanafunzi kimakosa,baada ya kutambua kuwa nilikosea Basi ilinibidi kumwomba msamaha.

Sasa wewe uzito unaupata wapi kwa kumuomba msamaha mtoto wako wa kuzaa!? Omba msamaha bwana.

Heshima ni kwa mkubwa na mdogo, hilo tambua
 
Wasalaam.

Hii ni Kwa wanaume wenzangu japo hata akina dada,mama mnaweza toa ushauri.

Iko hivi,

Juzi, yaani jumamosi,
Nilijichanganya kwa kuhisi nimepotelewa na kifaa changu ndani cha muhimu mno,yaani mno.

Sasa kumbe kuna mtu aliniazima na Mimi nikasahau kabisa kuwa nimeazimisha Mtu.

Basi katika kutafutatafuta na kukosa ,tuhuma zote nikazielekeza Kwa kijana wangu,ambaye muda mwingi sikai naye kwani huwa anaishimkoani anakosoma.

Basi nilitoa maneno yoooote mabaya,huku mwanangu akikataa hajahusika ,nikamsogelea nikamtikisa kama kutaka kumpiga, lakini kijana akapiga magoti huku akidai hajachukua kifaa kile.kwani Hana kazi nacho.

Kwahiyo tangu juzi tumekaa Kwa kukwepana huku nikiamini kijana kapoteza kifaa changu,

Chaajabu jioni hii saa 11 nimeletewa kifaa na mtu niliyekuwa nimemuazima huku akishukuru kwakuwa kimemsaidia mno ,ni takribani wiki tatu zimepita tangu aazime.

Sasa ,najikuta mwenye hatia,mwanangu nimemuonea,natamani hata nimuombe msamaha,je, inawezekana kumuomba msamaha mwanao wa kumzaa?

Majibu yenu tafadhali.
Hii kitu iliwahi nikuta nikiwa nimetoka kumaliza shule ya msingi miaka ya 90 huko. Mzee wangu aliaminishwa na mama mlezi ambaye na mke wake kuwa nimeiba kitu na kukiuza. Nilipoulizwa nilikataa kuwa sijachukua na kweli sikufanya hicho kitu.

Kwa aliambiwa lazima ni mimi nimechukua hicho kifaa basi usiku ule aliniambia nilale ila kabla hajaamka niwe nimeondoka. Ule usiku sikulala nawaza naenda wapi kwa umri ule. Nililala nimejiegesha nikiwa na mawazo.

Asubuhi saa 11 kesho yake kabla sijatoka aligonga mlango wa chumba changu cha nje. Nilipokutana naye aliniambia, " Samahani kile kifaa tumekipata chumbani kwetu kilifichwa sehemu fulani, unaweza rudi kulala." Niliumia sana ila pia kwa jinsi alivyokuja kuomba msamaha nilimuonea huruma maana nilijua wazi na yeye hajalala baada ya kukipata kifaa chake.

Muombe msamaha ndio uungwana.
 
Mkuu watu wamekushaur uombe msamaha fanya hivyo ila me Nina swali shida ni nini mpaka unakosa kumbukumbu kama hivi?

Jaribu kufatilia hili tatizo sio la kufumbia macho kabisa na kama ni Yale mambo ya kuinua na kushusha jaribu kuacha maana nayo yanaathiri kumbukumbu
 
Muombe msamaha, usipofanya hivyo akija kufikia uwezo wa kujitegemea utajuta kumfahamu maana atajitenga nawewe kipindi ambacho unamuhitaji
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom