Ndugu zangu!
Mimi ni mara ya kwanza kujenga, na nimefanya vitu vingi tayari kilichobaki kikubwa sasa ni kuweka Gypsum, mbao ameshaweka tayari, na plaster ishapigwa wa umeme kashafanya yake pia.
Fundi aliyeweka mbao zile za gypsum ndio uyo uyo atakuja kufunga gypsum, sasa basi mwanzo kanicharge kwa kazi ya kuweka mbao kwa laki 6 sikubisha nikampa kama ilivyo, na sasa kaniambia kufunga gypsum labour charge ni 1,000,000/=.
Sasa hapa nimekuwa njia panda hii ni sahihi au amenizidishia, maana hata nikipunguza nitapunguza kwa ngapi,hii nyumba ya kawaida vyumba vitatu vya kulala, sebule, dining .
Asanteni kwa ushauri!
acha kudanganya watu wewe,ingekuwa kazi moja lakini sio kwa laki 6.atupe vipimo tumpe makisio.ila kama ni nyumba kubwa kufanya gypsum,skimming na undercoat kwa em moja ni sawaPole sana mkuu, Blundering na kuweka Gypsum always huwa ni kazi moja. Inalipwa kama kazi moja. Kakupiga huyo. Kama bado nicheck nikupe Fundi kwa bei nafuu sana.
Asante kwa ushauri mzuri sana yaani umenifaa saaana,sasa naona hata soni kuwatajia ya umeme jamaa alinicharge ndefu sana yaani nikawa nakosa amani,lakini sababu mtu ninafahamiana naye,naona hata aibu kumuuliza but naona jamaa kaniibia kabisa sema tu sitaki kujua maana nitaumia roho sana.
Mimi nadhani hizi sio kazi moja inategemea mmepatanaje na fundi.Pole sana mkuu, Blundering na kuweka Gypsum always huwa ni kazi moja. Inalipwa kama kazi moja. Kakupiga huyo. Kama bado nicheck nikupe Fundi kwa bei nafuu sana.