Msaada kwa waliowahi kujenga

Msaada kwa waliowahi kujenga

Dear

Member
Joined
Nov 18, 2009
Posts
46
Reaction score
3
Ndugu zangu!

Mimi ni mara ya kwanza kujenga, na nimefanya vitu vingi tayari kilichobaki kikubwa sasa ni kuweka Gypsum, mbao ameshaweka tayari, na plaster ishapigwa wa umeme kashafanya yake pia.

Fundi aliyeweka mbao zile za gypsum ndio huyo huyo atakuja kufunga gypsum, sasa basi mwanzo kanicharge kwa kazi ya kuweka mbao kwa laki 6 sikubisha nikampa kama ilivyo na sasa kaniambia kufunga gypsum labour charge ni 1,000,000/=.

Sasa hapa nimekuwa njia panda hii ni sahihi au amenizidishia, maana hata nikipunguza nitapunguza kwa ngapi, hii nyumba ya kawaida vyumba vitatu vya kulala, sebule, dining .

Asanteni kwa ushauri!
 
Upo wapi maana Fundi anakua na gharama kulingana na alipo dar charge ni kubwa kuliko mikoani
 
Kakucharge pesa nyingi laki tatu bila kupwesa macho kakuonea kwa saaa 4 laki hiyo ndio bei ya kweri mwana jf
 
Dear

Duuu pole mkuu huyo fundi mwizi! Sijui anakuonaje nyumba ya vyumba vitatu blandeing (draft) laki 6 au ndio maurembo ya kushuka na kupanda lakini bado. Angekuchaji laki 3 tu.
Alafu kuweka gypsum milioni au ni pamoja na vifaa? Maana chumba kimoja hivi vya kitziii hata kiweje hakimalizi sheet 5 na mikada 5 za gypsum. Angekuchaji laki 4 tu au tatu na nusu. Mmh tafuta fundi mwingine bana.
Na ninyi mafundi acheni kuwakatisha tamaa wenzenu.
 
Last edited by a moderator:
Mimi niko dar es salaam
Mbao ulitumia kiasi gani ili kukusaidia kufanya makadirio ya usumbufu wa gympsum. Maana kama maurembo mengi sana na makona, ni wazi atakutoza fedha nyingi. Kingine ni ukubwa wa nyumba, kwa kuwa hujaeleza ukubwa wake ni vigumu pia kueleza makadirio bei
 
Dear

Vyumba vingapi na vya ukubwa gani. Siku hizi watu wanaenda kwa square metre!
 
Last edited by a moderator:
na wa kupaua ulimpa bei gani?
 
Mkuu kiukweli gharama hiyo ya 1m ni kubwa sana. Sana sana gharama isingezidi laki tano. Mwezi uliopita nilikuwa na project kama hiyo mjini Mwanza na ilinigharimu laki nne tu.

Nyumba yenyewe ilikuwa ya vyumba vitatu, sebule, dining,jiko,stoo, choo na bafu.

Gharama hiyo ya kuweka gypsum ilikuwa ni pamoja na kuweka mikanda na maua lakini haikujumuisha kazi ya blandering (sina hakika na hizo spelling) na pia upakaji wa rangi. Kazi ya rangi ilifanywa na mtu mwingine.

Ushauri wangu kama unaridhika na ubora wa kazi ya huyo fundi wako ongea nae akupunguzie gharama vinginevyo jaribu kuongea na mafundi wengine wawili zaidi ulinganishe bei.

Ni kweli kwamba mafundi wa Dar wana gharama za juu ukilinganisha na mafundi wa mikoani lakini si kwa tofauti kubwa kiasi hicho. Pengine huyo fundi alipoona umetoa laki sita za blandering bila kumwomba akupunguzie akaona hata hiyo 1m ya kuweka gypsum ungeitoa kirahisi bila ubishi.
 
Mbao ulitumia kiasi gani ili kukusaidia kufanya makadirio ya usumbufu wa gympsum. Maana kama maurembo mengi sana na makona, ni wazi atakutoza fedha nyingi. Kingine ni ukubwa wa nyumba, kwa kuwa hujaeleza ukubwa wake ni vigumu pia kueleza makadirio bei

Hata mimi nimewaza hivyo...kama chumba cha kulala ni ft. 10 X 10 hakiwezi kulingana na 12 X 12. Nadhani ungetoa vipimo ingekuwa sahihi zaidi.

NB: Moderator, Invisible hamuwezi kuiunganisha hii na ile kubwa ya ujenzi?
 
Last edited by a moderator:
Ndio bei zao hizo, usishangae kiongozi Kujenga kaziii
 
Namimi nipo kwenye step kama yako ulipofikia na nimepata fundi wa gypsum kwa bei nusu ya aliechukua kwako kama vp nicheki tusaidiane
 
Back
Top Bottom