Ni jamaa yangu tuko naye hapa kazini na namheshimu sana kama kaka yangu, umri wake kwenye 40's hivi. Hata wafanyakazi wenzangu wanaamini mimi ni mdogo wake kwa jinsi tulivyo karibu. Mkewe ni shemeji yangu kwa maana hiyo. Mwaka huu mwanzoni kaka akanisimulia shida yake ambayo alisema ni mimi tu ananiambia, si kwamba anadhani nitaweza kumsaidia, bali anaisema tu kupunguza tension kichwani. Akasema mkewe amepoteza kabisa hamu ya ngono, yaani hataki kabisa, na si kwamba ana-cheat popote ni kwamba hajisikii hata kidogo na hataki hata kugusiwa jambo hilo. Huyu kaka ana ule upole wa kilokole fulani, hana mambo ya mademu wala nini. Kwa hiyo kitendo cha mkewe kukosa hamu kimemuumiza sana maana yeye mwenyewe kaka anajisikia anahitaji hiyo kitu sana na hataki kuipata popote zaidi ya kwa mkewe.
Siku moja kampuni moja ya madawa wakawa wanafanya kama workshop fulani ya kujitangaza kwa madaktari, nikapata tenda ya kuwamo mle ndani niwarekebishie vifaa vyao vya presentation. Katika presentation yao wakaonesha dawa fulani inaitwa Dr Scotts Evening Prime Rose, wakaisifu sana kuwa huwa inawaongezea wanawake ashki, basi nikamkumbuka jamaa yangu. Niliporudi ofisini nikampa habari hiyo akaahidi kuifanyia kazi. Na kweli akainunua, na alisema mkewe alionesha ushirikiano mkubwa sana wa kuimeza kama alivyoshauriwa. Baada ya mwezi tu akaanza kuona mabadiliko, mkewe akaanza kupenda sana tendo, tena akawa yeye ndiye anayedai haki yake, na maisha yakaanza kuwa matamu tena.
Tatizo: Anasema hamu ya shemeji imepitiliza hadi sasa kaka hamuwezi tena, yaani anataka tendo mara nyingi na anataka kwa muda mrefu sana ambao kaka hawezi. Imefikia kaka anamuomba shemeji aache ile dawa kwa muda au apunguze dozi lakini shemeji inaonekana amekuwa addicted, hataki kuiacha. Sithubutu kumshauri chochote huyo shemeji maana sitaki ajue kuwa mumewe alinihusisha kwenye tatizo lake. Wakubwa, jamaa yangu afanyeje hapo?
Siku moja kampuni moja ya madawa wakawa wanafanya kama workshop fulani ya kujitangaza kwa madaktari, nikapata tenda ya kuwamo mle ndani niwarekebishie vifaa vyao vya presentation. Katika presentation yao wakaonesha dawa fulani inaitwa Dr Scotts Evening Prime Rose, wakaisifu sana kuwa huwa inawaongezea wanawake ashki, basi nikamkumbuka jamaa yangu. Niliporudi ofisini nikampa habari hiyo akaahidi kuifanyia kazi. Na kweli akainunua, na alisema mkewe alionesha ushirikiano mkubwa sana wa kuimeza kama alivyoshauriwa. Baada ya mwezi tu akaanza kuona mabadiliko, mkewe akaanza kupenda sana tendo, tena akawa yeye ndiye anayedai haki yake, na maisha yakaanza kuwa matamu tena.
Tatizo: Anasema hamu ya shemeji imepitiliza hadi sasa kaka hamuwezi tena, yaani anataka tendo mara nyingi na anataka kwa muda mrefu sana ambao kaka hawezi. Imefikia kaka anamuomba shemeji aache ile dawa kwa muda au apunguze dozi lakini shemeji inaonekana amekuwa addicted, hataki kuiacha. Sithubutu kumshauri chochote huyo shemeji maana sitaki ajue kuwa mumewe alinihusisha kwenye tatizo lake. Wakubwa, jamaa yangu afanyeje hapo?