Msaada kwa al Shabaab toka Tanga

jeoh

Senior Member
Oct 19, 2012
187
185
Katika tovuti ya BBC, mambo ya Somalia kuna taarifa "10 things we've learnt", ambayo mojawapo ya taarifa inataja uhusiano wa karibu wa kikundi kimoja cha Tanga,Tanzania na Al Shabaab.

Kama una subira ukienda kwenye tovuti ya Somalia Report ukisoma taarifa ya "UN Monitoring Group on Somalia and Eritrea" kuna appendix inayoeleza kwa kirefu na kutaja majina ya watu, tarehe na sehemu na hata mitaa inayojihusisha na kusaidia Al Shabaab, pamoja na kupeleka wapiganaji toka TZ, na mambo mengine. Cha kushangaza hakuna neno lolote tumesikia toka wahusika kukanusha au kukubali taarifa hiyo.

Kusadikika kwa ripoti hiyo hasa kuhusu fedha za madawa ya kulevya zitumikazo katika harakati za kusaidia Al Shabaab
ni hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanga kwa wa-Tanazania wawili na raia wa Iran mmoja mwezi August 2012 ambapo faini ya TZS trillioni moja kwa mara ya kwanza ilitolewa kwa wahalifu binafsi Tanzania.

Ingefaa taarifa hiyo itolewe tamko la kukanusha au kukubali, vinginevyo nchi itakuwa imedhalilishwa. taarifa hizo zinapatikana duniani kote.
 
We uko nchi gani hujaona cd kibao zinauzwa hapa dar na tanga zikihimiza watu wakapigane jehadi huko somalia.
 
Mbona hapa Tanga wapo tele na wengi wao wanajifanya wavuvi wa samaki! Na kwa taarifa yako jamaa wamesha jenga mahusiano mazuri na wana usalama mkoani Tanga, hivyo wanaishi na kufanya harakati zao bila shida wala matatizo. Tungoje siku wakitugeuzia kibao.
 
We uko nchi gani hujaona cd kibao zinauzwa hapa dar na tanga zikihimiza watu wakapigane jehadi huko somalia.

Wahubri Wa Kiislam ni bomu linalosubr kulipuka, halafu majority ni completely ignorance, somalia wakapgane jihad ipi? kwan kule alshabab inaeneza lidin lenu hlo, au munauana nyiny kwa nyiny? munashabikia kuuana? ths belief is a problem brotherz, believe me
 
wakuu tafazalin sana, ebu msihusishe trend ya tanga na ugaidi, bado ni mapema muno, tusiligawe taifa ndg zanguni
 
Mbona hapa Tanga wapo tele na wengi wao wanajifanya wavuvi wa samaki! Na kwa taarifa yako jamaa wamesha jenga mahusiano mazuri na wana usalama mkoani Tanga, hivyo wanaishi na kufanya harakati zao bila shida wala matatizo. Tungoje siku wakitugeuzia kibao.
Mambo mengine mnapoyaongea hadharani kama hapa muwe na ushahidi,sasa kama wewe ukiambiwa ukawataje hao jamaa utawataja?maana unaonekana km unajuana nao vzr?
 
Ivi wewe unapoiweka hapa habari ya mwaka 2012 lengo lako nini? Au unataka hayo mambo yawepo nchini? Hakuna haja ya kuweka hapa kwa kipindi hiki hasa unapoona nchi jirani zote zinakumbwa na uhalifu wa kigaidi.
 
Ivi wewe unapoiweka hapa habari ya mwaka 2012 lengo lako nini? Au unataka hayo mambo yawepo nchini? Hakuna haja ya kuweka hapa kwa kipindi hiki hasa unapoona nchi jirani zote zinakumbwa na uhalifu wa kigaidi.
Achana nao mkuu wanatumika na nchi jirani bila kujijua, kuna watu wanalazimisha propaganda kuwa Nchi yetu INA all shabaab hivyo Si salama ili kuhofisha wageni hasa watalii na wawekezaji.
 
Back
Top Bottom