Msaada: Kujiunga rasmi na CCM

Msaada: Kujiunga rasmi na CCM

Hiki chama kina ushawishi mkubwa sana kwa wale wapigaji. Trust me
 
Huyu yawezekana ni mdogo wake DEO KISANDU amekuja kwa ID nyingine
 
Uko vizuri Kada! Hongera.
Hivi katibana kanuni mpya za CCM zimesha printiwa?!
Ngoja nikuainishie aina za Mashina na kazi za Balozi wa nyumba kumi anayetokana na Ccm.

Aina za mashina:
1.Mashina yaliyo undwa ktk maeneo ya makazi maarufu kama Mashina ya nyumba kumi.
2.Mashina maalum yaliyo undwa katika Ofisi za Ccm,Jumuiya za wananchi zinazoongozwa na Ccm na Taasisi nyingine za Ccm.
3Mashina ya wakereketwa au Maskani kwa kule Zanzibar yaliyoundwa na wanachama wa Ccm katika maeneo husika baada ya kupata idhini ya Kamati ya Siasa ya Wilaya.
4Mashina ya nje ya nchi Mashina yaliyoundwa nje ya Nchi katika maeneo wanakoishi wanachama wa Ccm baada ya kupata idhini ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa.


Kazi za Balozi wa shina (Balozi wa nyumba kumi) wa Ccm.l
1.Balozi au Mwenyekiti wa Shina atachaguliwa na Mkutano wa mwaka wa Ccm wa shina.
Atakua katika nfasi ya uongozi kwa muda wa miaka mitano.
Lakini anaweza kuchaguliwa tena baada ya muda huo kumalizika.
2. atakua na madaraka ya kuangalia mambo ya Ccm na utandaji kazi katika Shina.
3.Atakua kiungo cha wanachama wote katika Shina.
4.Atakua ndiye mwenezi na mhamasishaji mkuu wa siasa ya Ccm katika eneo lake.
5.Atakua na wajibu wa kuwaeleza wanachama maamuzi yote ya Ccm,kuwaongoza na kuwashirikisha katika utekelezaji wa maamuzi hayo na kufikisha mapendekezo ya wanachama katika vikao vya juu.
6.Atakuwa na wajibu wa kufuatilia utekelezaji wa mambo yote ya siasa katika shina lake.
7.Atakuwa na wajibu wa kujenga uhusiano mwema wa wakazi wa shina lake kwa lengo la kuunda mazingira ya amani na utulivu.
8.Ataongoza Kamati ya Uongozi ya Shina pale panapohusika.
9.Atakua Mwenyekiti wa Mkutano wa Mwaka wa Ccm wa Shina na Mkutano wa Wanachama wote wa Shina.
10.Katika Mikutano atakayoongoza zaidi ya kuwa na kura yake ya kawaida atakua pia na kura ya uamuzi endapo kura zabwajumbe wanaoafiki na wasioafiki zitalingana.
Isipokuwa kwamba kama kikao anachokiongoza ni kikao cha uchaguzi,Mwenyekiti atakua na kura yake ya kawaida tu.Hatakuwa na haki ya kutumia kura yake ya uamuzi endapo kura za wajumbe zimelingana.Wajumbe wa kikao wataendelea kupiga kura mpaka hapo mshindi atakapopatikana.


Hadi hapo hakuna sehemu palipo andikwa kwamba Balozi ni muajiriwa wa Serikali na pia hakuna sehemu iliyo andikwa kwamba Balozi anatoa kadi kwa wanachama wapya.



Katibu wa siasa na uenezi wa Tawi moja ya majukuku yake ni
Ibara ya 45 (a) Kusimamia kueneza na kufafanua masuala yote ya Itikadi,Siasa na Sera za Ccm katika Tawi.a

Moja ya majukumu ya Katibu wa Tawi ni.
Ibara ya 44 (4)Atashughulikia masuala yote ya Organaizesheni ya Ccm katika Tawi ambayoni
(a)Masuala yote ya wanachama.




Hapo nimekumegea kidogo tu ili upate picha ni wapi uanzie ila muhimu umjue Balozi wako kabla hujaenda Ofisi ya Tawi maana lazima utaulizwa eneo unaloishi na kikawaida Balozi nikama mdhamini wako.

;
 
Hapa shida ni nini hasa ...ulitakaje kwa mfano. siamini unachokiamini lazima ukubali utofauti wetu.
Hapana mkuu una haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa ila pia sisi wengine lazma tushangae maana chama ambacho kimetuletea umaskini na uchumi mbaya kwa miaka 50 ya utawala wake na kimeshindwa uongozi ndio unatala kuhamia huko!!!! Kaz kwelikwlei
 
Sikuwezi aisee: Kuna wajumbe wa nyumba kumi kwenye mitaa na hao unaowazungumzia wajume wa mashina wa nyumba kumi
Mjumbe wa shina au Balozi anatokana na chama chochote cha siasa kilicho sajiliwa,ingawa awali vyama vya upinzani havikuwa na huu utaratibu,kwa Chadema wameshaanza nao kuwa na hawa watu muhimu mno kwa ujenzi wa chama wajumbe wa mashina (Mabalozi wa Nyumba Kumi) sinauhakika na vyama vingine.


Pia kuna wajunbe wa Serikali za Mitaa nadhani ndio hawa unao wazungumzia,wewe hawa huwa watano tu ndani ya kila Ofisi ya aserikali za Mitaa,nao huchaguliwa na wananchi wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hutokea kwenye vyama vya siasa kwamaana ya kwamba huwezi kugombea Ujumbe wa Serikali za Mitaa bila kudhaminiwa na chama cha siasa ni kama vile tunavyo waona waheshimiwa Wabunge.

Wajumbe hawa wa Serikali za Mitaa hutenda kama washauri wa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa hawa wamo kwenye system ya Serikali.
Na wakati huu wa muundo wa vyama vingi vya siasa huwa ni mchanganyiko wa Itikadi.
Na hawa huwa hawaruhusiwi kujihusisha kabisa na masuala ya siasa ndani ya Ofisi ya Serikali za Mitaa.
 
Kachukue kadi kibiti, unapewa na uenyekiti kabisaaa!!!
 
kugombea uongozi ni baada ya miaka mitanotangu ulipo jiunga.
 
Sina shaka na afya zenu
Wakuu nimeamua kwa dhati kabisa kujiunga na chama kikongwe nchini na chenye ushawishi mkubwa kwa wananchi wake ukiangalia falsafa, mtizamo na sera za chama. Hii haina maana nilikuwa upinzani no. mm nilikuwa neutral sikuwahi kumiliki kadi ya chama wala kushiriki kazi zozote za kichama. Leo baada ya kutafakari nikaona kama kijana nahitajika pia kujenga nchi yangu kupitia chama na hasa CCM.

Ombi langu kwenu wadau naomba mnipe mwongozo na taratibu za kujiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM)-[Revolutionary party]

Kidumu chama cha Mapinduzi
Asanteni
Ccm oyeee,karibu sana kada kwenye chama cha wazalendo harisi wa nchi hii,chama kilicho asisiwa na Hayati Baba wa Taifa hili,chama cha ukombozi wa Afrika,chama kinacho amini kila binadamu ni sawa na anayo haki ya kuheshimiwa na kuthaminiwa,chama chenye kupigania maslai ya kila mtanzania,Chama kinacho pigana kutokomeza maadui watatu wa Taifa hili ambao ni,
1.UMASKINI
2.UJINGA
3.MARADHI.
Hakika umefanya maamuzi sahihi ya kuwa mzalendo wa Taifa lako,wewe ni mtu huru sasa.
 
Hapana mkuu una haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa ila pia sisi wengine lazma tushangae maana chama ambacho kimetuletea umaskini na uchumi mbaya kwa miaka 50 ya utawala wake na kimeshindwa uongozi ndio unatala kuhamia huko!!!! Kaz kwelikwlei
mm siamini kama chama kinaweza kuleta umaskini nasema tena siamini na uchumi mbaya sio wa chama na hauletwi na chama umaskini ni attitude zenu na utayari wa kufanya kazi hamna taifa limepata maendeleo kwa kuwa na watu kila kukicha wanashinda kwenye magenge ya kahawa
 
Mjumbe wa shina au Balozi anatokana na chama chochote cha siasa kilicho sajiliwa,ingawa awali vyama vya upinzani havikuwa na huu utaratibu,kwa Chadema wameshaanza nao kuwa na hawa watu muhimu mno kwa ujenzi wa chama wajumbe wa mashina (Mabalozi wa Nyumba Kumi) sinauhakika na vyama vingine.


Pia kuna wajunbe wa Serikali za Mitaa nadhani ndio hawa unao wazungumzia,wewe hawa huwa watano tu ndani ya kila Ofisi ya aserikali za Mitaa,nao huchaguliwa na wananchi wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hutokea kwenye vyama vya siasa kwamaana ya kwamba huwezi kugombea Ujumbe wa Serikali za Mitaa bila kudhaminiwa na chama cha siasa ni kama vile tunavyo waona waheshimiwa Wabunge.

Wajumbe hawa wa Serikali za Mitaa hutenda kama washauri wa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa hawa wamo kwenye system ya Serikali.
Na wakati huu wa muundo wa vyama vingi vya siasa huwa ni mchanganyiko wa Itikadi.
Na hawa huwa hawaruhusiwi kujihusisha kabisa na masuala ya siasa ndani ya Ofisi ya Serikali za Mitaa.
Be consistent with what you try to argue. Naheshimu uzoefu wako kwenye chama lakini mkanganyiko huu unatia shaka
 
Kwa Chadema sasa kila anayeachia ngazi hata kama ameyafanya maovu kiasi gani akiwa ccm kwao ni shujaa wao.Leo hii mnamwona kinana ni shujaa kweli? Mnamwona Mecky Sadik ni shujaa kweli Chadema mko serious mna nia ya dhati na mnaitakia mema nchi hii?
kama walivyo kuwa wema wakati mko nao ccm ndivyo hivyo hivyo watakuwa wema wakija upinzani na uadui utaamia kwenu sawa eeeh
 
Be consistent with what you try to argue. Naheshimu uzoefu wako kwenye chama lakini mkanganyiko huu unatia shaka
Kaka usiwe mzito kiasi hicho bwana,mi nimejaribu kukuelewesha kwasabb ulisema unataka kujiunga na chama nikakupa maelekezo lkn bado unaongelea wajumbe sijui wa chana sijui wa serikali.
Ndipo nikajaribu kukuainishia aina hizo za Wajumbe yaani wajumbe "Mabalozi" wa ndani ya chama na wajumbe wa Serikali za Mitaa hawa hawaitwi Mabalozi bali "Wajumbe wa Serikali za Mitaa" sasa ni jukumu lako hapo kujiongeza ili uelewe nini unataka na utakipata wapi.
Lakini kutokana na haya unayo andika nahisi huko serious au hujijui mwenyewe unataka nini hasa.
Binafsi nimejitahidi kukuelewesha hapo ndo uwezo wangu ulipo ishia.
Pole sana mkuu.
 
Sina shaka na afya zenu
Wakuu nimeamua kwa dhati kabisa kujiunga na chama kikongwe nchini na chenye ushawishi mkubwa kwa wananchi wake ukiangalia falsafa, mtizamo na sera za chama. Hii haina maana nilikuwa upinzani no. mm nilikuwa neutral sikuwahi kumiliki kadi ya chama wala kushiriki kazi zozote za kichama. Leo baada ya kutafakari nikaona kama kijana nahitajika pia kujenga nchi yangu kupitia chama na hasa CCM.

Ombi langu kwenu wadau naomba mnipe mwongozo na taratibu za kujiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM)-[Revolutionary party]

Kidumu chama cha Mapinduzi
Asanteni
Nenda ofisi za CCM Kibiti wana kadi za kumwaga ikiwezekana na cheo unapata siku hiyo hiyo.
 
Back
Top Bottom