Msaada kuhusu UTT , Treasury Bonds/Bills na Fixed deposit accounts

Msaada kuhusu UTT , Treasury Bonds/Bills na Fixed deposit accounts

Wingawinga

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2021
Posts
627
Reaction score
1,533
Habari zenu wadau? Nilikua naomba maelezo kwa mifano halisi namna ya ku calculate hiyo mifuko , nikiwa na maana nikitaka kupata income ya kila mwezi kwa kiasi cha uwekezaji wa Milioni 100,000,000/= , natanguliza shukran.
 
Unapata asilimia moja Kila mwezi kwa utt ya hela uliyowapa. Kwa iyo hela Kila mwezi unapata 1M kwa mwaka unayo 12M, fixed deposit utaambulia ndogo mno benki zinatoa riba tofauti tofauti, Ila mara nyingi watakupa kuanzia 5-9% wao wanakopesha kwa 17%
 
Utanisamehe kwa kutoe elewa vizuri , naomba nitpe mfano halisi
Mfano nina miliioni mia , caltlation je inakwenda kamanhivi ?
100,000,00 X1/100 na ammount nayo ipta ndio hiyo hiyo kwa mwezi? Yabi nikiwa na maana ile 1,000,000 , inakuabkamili au nayo naigawa kwa 12 ? Asante
 
Habari zenu wadau? Nilikua naomba maelezo kwa mifano halisi namna ya ku calculate hiyo mifuko , nikiwa na maana nikitaka kupata income ya kila mwezi kwa kiasi cha uwekezaji wa Milioni 100,000,000/= , natanguliza shukran.
Tunaweza kuelekeza ila hatupo tayari kukuona unatoka Nusu Nusu.....Humu JF kuna Mada nyiingi kama hizi zimezungumzwa pitia
Thread 'Fixed Deposits Account, UTT-Amis ni njia nzuri za kutunza pesa LAKINI SIYO uwekezaji abadani' Fixed Deposits Account, UTT-Amis ni njia nzuri za kutunza pesa LAKINI SIYO uwekezaji abadani

UTT wanasemaga return ni 1% kwa Mwezi Ambapo kwa mwaka inaweza kuwa 12%...Ila inategemea na Aina ya mfuko unaowekeza kuna mifuko hufikia 12% kwa mwaka au zaidi na kuna mifuko inakuwa pungufu ya Hapo .Hivo ni muhimu kufahamu uNataka kuwekeza kwa malengo gani au sehemu zenye Uwekezaji labdah Hisa Tu n.k

•Treasury bills na bonds Hapo ni swala la kuongea na Broker wako Ambapo yeye atakupa mwanga zaidi WA hili

•Fixed deposit ni kuweka Hela ukitegemea faida Fulani mfano million 100 kwa miezi 9 upate return ya 4.5% Ambapo Hela yako huigusi mpaka Muda WA ukomo ufikie
 
ningegusia zote ila naomba niongee kidogo tu kuhusu Treasury bonds ,,wengine wataongelea hizo zingine ..

Wewe naona umependelea ya kila mwezi, kuna njia mbili kuu za kupata mapato kutoka kwa Treasury bond:
Ya kwanza wanaita coupon payments (Riba za Kila Muda), kwa mama ya unapata riba mara kwa mara (kila mwezi, robo mwaka, au mwaka) kulingana na masharti ya bond, muda ukifika unapokea kiasi cha awali (principal).

Mfano kwa wewe,,
Principal (uwekezaji) unawekeza milioni 100,000,000 , Coupon Rate (kiwango cha riba) ni 10% kwa mwaka,,muda wa bond tuseme ni Miaka 5 ,,malipo ya riba ni kila mwezi itakua 833,333/-
Jumla ya riba kwa miaka 5 ni 10,000,000 × 5 = 50,000,000
Jumla ya mapato ambayo utachukua baada ya miaka mitano ni 100,000,000 + 50,000,000 =milion 150.
 
Unapata asilimia moja Kila mwezi kwa utt ya hela uliyowapa. Kwa iyo hela Kila mwezi unapata 1M kwa mwaka unayo 12M, fixed deposit utaambulia ndogo mno benki zinatoa riba tofauti tofauti, Ila mara nyingi watakupa kuanzia 5-9% wao wanakopesha kwa 17%
Kimsingi kwa 100m hawez pata 1m kila mwez tapata around 850k hv au juu kdg ili apate 1m atahitaj kuweka 120m
 
Fixed - Hapana

UTT
  • 1% kwa mwezi na
  • Kuna Option ya kupata hela yako ndani ya muda mfupi ukiihitaji..

Treasury Bonds
  • 1.25% - 1.575% kwa mwezi
  • Kuna Bond za miaka 2 - 25
  • Unaweza kuhamishi umiliki
  • Unaweza kukopea mkopo
 
Back
Top Bottom