msaada kuhusu toyota platz na nadia

Kacharimbe

JF-Expert Member
Apr 2, 2011
211
34
Wakuu, nina noah ya mwaka 2001 na nimeiingiza tz sept 2010, odo inasomeka 142880. Kutokana na ugumu wa maisha na kupanda kwa bei ya petrol nimeshindwa kuimudu. Kuna jamaa kapatikana anataka kuichukua anipe toyota platz au nadia. Bahati mbaya hizo gari sijawahi kuzitumia ila kaniambia platz in cc 1000 na nadia cc 1500 na anafahamu kuwa fuel consumption ya gari hizo ni ndogo sana. Naomba waliotumia gari hizo wanisaidie kuhusu mambo mengine kuhusu gari hizo kama vile uimara na bei zake kwa sasa maana amesema ataniongeza na hela kidogo. Mimi gari yangu naithamanisha m14. Msaada please
 
Hiyo noah yako inatumia lita moja ya petroli kwa km ngapi?

km 8/lita. Ingawa tayari kuna jamaa kaniambia nadia haina tofauti na noah. Kanishauri ni opt corrolla premio/premio au raum. Platz anasema ni less fuel consumption bali siyo imara. Kwa hiyo mkuu nishauri kati ya toyota raum na premio
 
mambo ya magari hutegemea sana na prefence ya mtu. cha msingi angalia gari yoyote ambayo ni below cc 1500. Nadia haina tofauti sana na noah katika ulaji wa mafuta ila ni gari nzuri. Kama unataka kwa ajili ya matumizi laini (home-ofcn-home), platz, premio, starlet ni nzuri. ukitaka kubwa zaidi nadhani toyota raum
 
nadia haina tofauti na noah ulaji wa mafta sawasaw alafu m sikushauri uchukue nadia ni vmeo zikianza kusumbua yan unaweza kuumia kichwa na stress za maisha ztakushka haraka we uon mwenzako anataka akupe akuongeze na pesa anajua yaliyomtokea na ni siri yake
 
nadia haina tofauti na noah ulaji wa mafta sawasaw alafu m sikushauri uchukue nadia ni vmeo zikianza kusumbua yan unaweza kuumia kichwa na stress za maisha ztakushka haraka we uon mwenzako anataka akupe akuongeze na pesa anajua yaliyomtokea na ni siri yake

Ni kweli mkuu. Na mimi ndo maana niko makini sana. Baada ya kupitia thread mbalimbali humu jf na ushauri wa jamaa mbalimbali nime shortlist gari tano ambazo ni Yoyota Starlet, toyota platz, Toyota corolla, Toyota Premio na Toyota corona Premio. Nataraji nimwambie anitafutie gari moja wapo kati ya hizo. Bahati mbaya sijapata habari kamili kuhusu toyota corolla na premio/ corona premio. Naomba mwenye ufahamu zaidi anijuze
 
me natumia toyota corona premio,nna mwaka nayo sasa cjaona ubaya wake na consuption iko poa,ni nzuri ya injini ndogo isiwe D-4,utaenjoy mkuu!
 
Ni kweli mkuu. Na mimi ndo maana niko makini sana. Baada ya kupitia thread mbalimbali humu jf na ushauri wa jamaa mbalimbali nime shortlist gari tano ambazo ni Yoyota Starlet, toyota platz, Toyota corolla, Toyota Premio na Toyota corona Premio. Nataraji nimwambie anitafutie gari moja wapo kati ya hizo. Bahati mbaya sijapata habari kamili kuhusu toyota corolla na premio/ corona premio. Naomba mwenye ufahamu zaidi anijuze

Mkuu ukifanikiwa kukamata starlet utakula bata la kufa mtu. Mafuta ni kama kananusa, spea za kumwaga na bei nafuu.....hakuna anayeweza kunishawishi nimuuzie haka kangu asee!
 
Platz inashare platform na vitz au yaris. ni gari isiyo na sura nzuri lakini ni imara na si kama ulivyoambiwa na wengine. engine pia ni ya vitz. hata dash board yake ni ya vitz pia. magari ya toyota ni imara na yanatengenezeka. kwa dunia ya sasa platz ni bora kuliko starlet na hayo premio, nadia, na mengineyo. kwani premio au nadia kama ina injini ndogo ni cc 1800 na starlet ni cc 1300. na ujue kuwa vitz ndo imechukua nafasi ya starlet baada ya kufunga production ya starlet ndo wakaja na vitz na platz wa watu wasiopenda hatch back desines. hizo zingine huwezi fananisha na platz au vitz ambayo km 20 ni lt 1. na ukipata vitz ya kuanzia 2008 yenye injini cc 1300 inakunywa lt 1 km 26. pia zipo trims nyingi sana kuanzia cc 1000 hadi 1800 nawameimprove fuel consumption kwa kiasi kikubwa. so, nakushauri uchague platz.
 
Platz inashare platform na vitz au yaris. ni gari isiyo na sura nzuri lakini ni imara na si kama ulivyoambiwa na wengine. engine pia ni ya vitz. hata dash board yake ni ya vitz pia. magari ya toyota ni imara na yanatengenezeka. kwa dunia ya sasa platz ni bora kuliko starlet na hayo premio, nadia, na mengineyo. kwani premio au nadia kama ina injini ndogo ni cc 1800 na starlet ni cc 1300. na ujue kuwa vitz ndo imechukua nafasi ya starlet baada ya kufunga production ya starlet ndo wakaja na vitz na platz wa watu wasiopenda hatch back desines. hizo zingine huwezi fananisha na platz au vitz ambayo km 20 ni lt 1. na ukipata vitz ya kuanzia 2008 yenye injini cc 1300 inakunywa lt 1 km 26. pia zipo trims nyingi sana kuanzia cc 1000 hadi 1800 nawameimprove fuel consumption kwa kiasi kikubwa. so, nakushauri uchague platz.

Nimekusoma vizuri mkuu. Platz naipenda sema nilikuwa siijui kiundani. Umenifumbua macho. Mimi siangalii shape, naangalia efficiency & economy
 
mkuu umejaribu corolla fielder au carina ti? Hizo vp?

Mkuu bahati mbaya sijawahi kuintract sana na magari, so sijui sana nini kizuri na kibaya katika magari. Ila ninachojua ni cc tu na gharama za spea kwa baadhi ya magari. So far nime rank corolla as no one in my preference simply because ina cc 1300 ila sijafahamu ktk collolla ni aina gani. Labda nisaidie uzuri wa hiyo gari mkuu.
 
mkuu starlet au baby walker(vitz) ndio mpango mzima.. yani watu wakiingia kituo cha mafuta we unapita tu, mi gari yangu nimeisusa siku hizi navinjari na baby walker ya mama!
 
mkuu starlet au baby walker(vitz) ndio mpango mzima.. yani watu wakiingia kituo cha mafuta we unapita tu, mi gari yangu nimeisusa siku hizi navinjari na baby walker ya mama!

kanaweza kupiga masafa angalau mara mbili kuingia vijijini kuwaona akina bibi?
 
kanaweza kupiga masafa angalau mara mbili kuingia vijijini kuwaona akina bibi?

inategemea masafa ya wapi mkuu.. kamabara bara safi kananyooka tu taratibu lakini ila kwa safari za huko ndipo nachukuaga hili jini langu kwenye safari huwa halinywi sana
 
Back
Top Bottom