SONGEA
Senior Member
- May 29, 2008
- 101
- 8
Kuna tofauti kati ya paid vacation na unpaid vacation na kulipiwa nauli ya kwenda kwenu whether umechukua paid au unpaid vacation. Ambacho sielewi ni kwa nini mtu ulipiwe nauli ya kwenda kusalimia kwenu ilhali unalipwa mshahara.
Paid vacation haiathiri mshahara wako. Ukienda likizo utalipwa mshahara wako kama kawaida. Ila kwa uzoefu wangu, unapochukua unpaid vacation ni kwamba unakuwa huna PTO (paid time off) hivyo ukitaka kuchukua likizo basi hiyo likizo itakuwa ni ya bila malipo.
Sasa unaenda zako likizo halafu eti mwajiri wako anakulipia nauli ya kwenda huko unakoenda, WTF!! Nahisi labda tunazungumzia labor laws za nchi tofauti kabisa. Mwisho wa siku ni uamuzi wa mwajiri na sheria za hiyo nchi zinasemaje kuhusiana na hayo mambo ya vacation/ paid time off na kadhalika.
Naona kama mambo yanachanganywa. Kuna waajiri wanaolipa mshahara wa mwezi mmoja mtumishi anapokwenda likizo, wengine wanalipia nauli n.k.
Ila suala ni palae mtu anapokuwa analipia nauli halafu mtu analala njiani siku tatu. Anastahili posho ya kula/kulala?