Msaada kuhusu kuvunjika mguu

Msaada kuhusu kuvunjika mguu

Zero Competition

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2018
Posts
347
Reaction score
556
Habari zenu wana jukwaa

Nilipata tatizo la mguu baada ya kudondoka na nilipoenda hospital nikapigwa X-ray kisha doctor akanambia kwamba nimevunjika mfupa mdogo ambao haubebi uzito kisha palepale nikatakiwa nivae Plaster of Paris (POP) na nikaambiwa kwamba natakiwa nikae nayo kwa muda wa wiki 4

Siku ya kwenda kufungua POP ilipofika doctor akanambia kabla sijafunguliwa POP natakiwa nipige tena X-ray na kama maendeleo yatakua bado sio mazuri nitatakiwa nikae nalo tena kwa wiki mbili zaidi

Nilivyopiga X-ray doctor akasoma ile picha kisha akanambia kwamba maendeleo ni mazuri kwahiyo inabidi nitolewe ili POP kisha akanipa maelekezo kwamba katika kipindi cha miezi miwili mpaka mitatu sitakiwi kukimbia ila nitembee tu kawaida mpaka pale hali itakapokua imeimarika kabisa

Swali langu hapa ni je, Doctor aliponambia maendeleo mazuri maana yake kwamba mfupa umeshaunga au tafsiri yake ni nini ?

Naomba kwa wenye uzoefu wanijuze
 
Mpaka umetoa POP maana yake mfupa umeshaunga. Kinachobaki ni ku limit mishe zako ili kuuwezesha upone kabisa.
 
Umepotea njia ndugu! Hilo swali ilitakiwa alijibu dakitari wako yeye ndo aliona na hiyo x ray!
Tena ningelakuwa mimi ningemuhoji vipi nikikutana na panya road nisikimbie..?

Mkuu ushauri wangu wa kidakitari uchwala kula Sana vitu vya calcium vikusaidie kuunga haraka kwa huo muda naimani utaanza kukimbia na kupaa kabisa!

Usipokimbia tutakukimbiza...😂
 
Pole sana,ila ungemuuliza daktari wako ingekuwa poa sana.
 
Umepotea njia ndugu! Hilo swali ilitakiwa alijibu dakitari wako yeye ndo aliona na hiyo x ray!
Tena ningelakuwa mimi ningemuhoji vipi nikikutana na panya road nisikimbie..?

Mkuu ushauri wangu wa kidakitari uchwala kula Sana vitu vya calcium vikusaidie kuunga haraka kwa huo muda naimani utaanza kukimbia na kupaa kabisa!

Usipokimbia tutakukimbiza...😂
Shukrani sana kaka 😄😄😄
 
Umepotea njia ndugu! Hilo swali ilitakiwa alijibu dakitari wako yeye ndo aliona na hiyo x ray!
Tena ningelakuwa mimi ningemuhoji vipi nikikutana na panya road nisikimbie..?

Mkuu ushauri wangu wa kidakitari uchwala kula Sana vitu vya calcium vikusaidie kuunga haraka kwa huo muda naimani utaanza kukimbia na kupaa kabisa!

Usipokimbia tutakukimbiza...
Qmmmk!!
 
Habari zenu wana jukwaa

Nilipata tatizo la mguu baada ya kudondoka na nilipoenda hospital nikapigwa X-ray kisha doctor akanambia kwamba nimevunjika mfupa mdogo ambao haubebi uzito kisha palepale nikatakiwa nivae Plaster of Paris (POP) na nikaambiwa kwamba natakiwa nikae nayo kwa muda wa wiki 4

Siku ya kwenda kufungua POP ilipofika doctor akanambia kabla sijafunguliwa POP natakiwa nipige tena X-ray na kama maendeleo yatakua bado sio mazuri nitatakiwa nikae nalo tena kwa wiki mbili zaidi

Nilivyopiga X-ray doctor akasoma ile picha kisha akanambia kwamba maendeleo ni mazuri kwahiyo inabidi nitolewe ili POP kisha akanipa maelekezo kwamba katika kipindi cha miezi miwili mpaka mitatu sitakiwi kukimbia ila nitembee tu kawaida mpaka pale hali itakapokua imeimarika kabisa

Swali langu hapa ni je, Doctor aliponambia maendeleo mazuri maana yake kwamba mfupa umeshaunga au tafsiri yake ni nini ?

Naomba kwa wenye uzoefu wanijuze
Kwa hiyo dokta alipokutoa POP na kukupatia masharti alitoka nduki au?

Hapa utajibiwa na watu wenye stress ulie
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom