Msaada kuhusu Butcher la Samaki

Mtalebani Mweupe

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2020
Posts
565
Reaction score
654
Wakuu habari!

Naomba wenye ujuzi wa biashara za samaki, kama wenye mabucha mniambie gharama zake zikoje.

Nina plan ya kuanzisha biashara hii Mungu akijaalia ninahitaji info za kutosha ili nikiji commit nisije kujilaumu mambo yakienda kushoto.

Nahitaji kujua gharama na ushauri wa vitu hivi hapa chini:-

*Mashine ya kukatia
*Samaki bei zake ( Sato & Sangara)
*leseni zipi zinazohitajika kuanzisha butcher la samaki
*Mkoa upi ni cheap kununua samaki?
*freezer aina gani inafaa?

Kama kuna jengine sijaliandika hapo pia mnaweza kunishauri
 
Nenda halmashauri husika kwa afisa biashara kakate leseni ya biashara.
Nenda idara ya afya ma afisa afya ukapate maelekezo ya uendeshaji wa hiyo biashara ya chakula.


#MaendeleoHayanaChama
 
vikwazo ninavyoviona hapo kwenye hiyo biashara unayotaka kufungua, itakuwa ni TRA pamoja na UMEME wa uhakika.
japo ni biashara yenye faida ila jiandae kwa hilo
 
kwa anaehitaji samaki jumla anicheki inbox .bei nafuuu kabisa.kwa sato na sangara.

Sato nauza 8500 kwa kig moja bei ya jumla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…