Msaada kuhusu bima za magari

Msaada kuhusu bima za magari

Makampuni ya bima huwa hayataki kudeal na wateja moja kwa moja. Kwa hiyo ukienda kwenye kampuni moja kwa moja utapigwa rate kubwa kuliko ukienda kwa dalali (broker) au wakala (agent).
Si sahihi sana.
Makampuni ya Bima yanapenda pia Wateja directly kwa sababu wanapata 100% profit tofauti na kupitia kwa broker au agent inabidi watoe 10%- 20% commission
 
Mkuu commercial zina rates zake tofauti.

Third party hawaangalii cc za gari tena kama zamani. Kwa sasa third party kwa private cars ni Tsh. 100,000 plus 18% VAT ko jumla inakuwa Tsh 118,000.
We unaongelea road lisence ambayo tayari imefutwa.
Bima haihusiani na cc za gari kabisa tena kwenye bima wewe ndiye waweza thamanisha gari lako mwenyewe
 
We unaongelea road lisence ambayo tayari imefutwa.
Bima haihusiani na cc za gari kabisa tena kwenye bima wewe ndiye waweza thamanisha gari lako mwenyewe
Mkuu kwenye kuthaminisha gari inaweza kuwa tatizo baadaye. Inaitwa disclosure of material fact. Ukitaja thamani ndogo inaweza kuwa tatizo hasa kama una 'comprehensive insurance'
 
Mkuu kwenye kuthaminisha gari inaweza kuwa tatizo baadaye. Inaitwa disclosure of material fact. Ukitaja thamani ndogo inaweza kuwa tatizo hasa kama una 'comprehensive insurance'
Yah hilo ni kweli ilishawahi kumtokea ndugu yangu
 
Mkuu kwenye kuthaminisha gari inaweza kuwa tatizo baadaye. Inaitwa disclosure of material fact. Ukitaja thamani ndogo inaweza kuwa tatizo hasa kama una 'comprehensive insurance'
Yah hilo ni kweli ilishawahi kumtokea ndugu yangu
 
Si sahihi sana.
Makampuni ya Bima yanapenda pia Wateja directly kwa sababu wanapata 100% profit tofauti na kupitia kwa broker au agent inabidi watoe 10%- 20% commission
Tatizo ni sera ya bei. Nilienda kwa wakala akasema 3% nikaenda kwenye kampuni ya bima ikasema 5%. Ndo nikapata picha kuwa wanaachiana majukumu. Mteja unafukuzwa kidiplomasia kwa tofauti ya bei.
 
Makampuni ya bima huwa hayataki kudeal na wateja moja kwa moja. Kwa hiyo ukienda kwenye kampuni moja kwa moja utapigwa rate kubwa kuliko ukienda kwa dalali (broker) au wakala (agent).

Rate ya bima ni sawa kote, hakuna kampuni ya bima utakayolipa zaidi ya nyingine. Kama broker/agent alikuambia atakupunguzia bei, uyo ni mwizi na siku ukipata matatizo hautofidiwa na bima.
 
Mkuu kwenye kuthaminisha gari inaweza kuwa tatizo baadaye. Inaitwa disclosure of material fact. Ukitaja thamani ndogo inaweza kuwa tatizo hasa kama una 'comprehensive insurance'

Ukitaja "sum insured" ndogo ndio hiyo hiyo utakuja kulipwa siku ukipata ajali. Ni vizuri mtu akataja bei halisi ya gari lake hili siku akipata ajali aweze kulipwa bila ya usumbufu wowote.
 
Tatizo ni sera ya bei. Nilienda kwa wakala akasema 3% nikaenda kwenye kampuni ya bima ikasema 5%. Ndo nikapata picha kuwa wanaachiana majukumu. Mteja unafukuzwa kidiplomasia kwa tofauti ya bei.

Ukitaka kukata comprehensive insurance kwa gari binafsi rate ni 3% ya thamani ya gari lako + kodi. Rate ya gari la biashara ni tofauti na gari binafsi.
Wewe ulikua unakatia gari binafsi au la biashara?
 
Nimewasoma wakuu. Asanteni.
Sasa nimebadili mawazo
 
Kabda ya kununua bima zingatia Haya yafuatayo............

  • Hakikisha ni kweli unahitaji bima na itaendana na janga ambalo likitokea na hutoweza kulimudu kifedha. mfano matatizo ya afya, janga la wizi, moto au hasara ya kupoteza fedha katika biashara yako.

  • Angalia gharama ya bima kama utaweza kuzimudu na kwa muda mrefu hata kama malipo ni kwa kila mwezi.

  • Zingatia fidia utakayoipata kama itaendana na majanga utakayo yapata. mfano mkataba wa bima unasema fidia itakua ni 10 milioni endapo likitokea janga la moto katika biashara yako, je ukiangalia katika biashara yako janga la moto likitokea fidia ya 10 millioni itakidhi?

  • Zingatia mashari ya mtakaba wa bima na unaeleza nini endapo janga likitokea , utahisika vipi katika hatua za mwanzo na ni viambatanishi vipi vinajitajika katika kuwasilisha madai ya bima.

  • Zingatia ni kampuni ipi ya bima inatoa bima unayohitaji. hapa utaangalia ubora na uhakika wa kupata huduma haraka endapo majanga yakitokea.

  • Zingalia kuchagua wakala (agent) au dalali (Broker) wa bima ambae ni bora katika kutoa huduma za kibima kuanzia mwazo wa mauzo ya bima hadi pale janga likitokea.


Mwishio, bima ni ni mkataba wa ahadi kwa maana ya kwamba kampuni ya bima inakuahidi kukupa fidia endapo janga fulani likitokea na inakutaka wewe kulipa kiasi kidogo cha fedha kwa kipindi hicho cha makubalianio. Katika makubaliano anaweza kuwepo dalali wa bima au wakala ambaye atasimamia katika hatua za manunuzi ya bima na endapo janga husika likitokea.

Kwa Msaada wa madai ya bima wasiliana na mimi kupitia number +255 765 827 355
 
Back
Top Bottom