Msaada: Kuhama Marekani kwenda Australia au Canada

Msaada: Kuhama Marekani kwenda Australia au Canada

Sababu wanayokupa ni nini? Maana kuna ndugu ameenda hata miezi sita haijaisha ka apply ndoa na vibali vya kazi amepata....kutakuwa na sababu katika case yako!
 
kwa mfano mtanzania (mwanaume) ukienda nje kusoma ukimaliza kusoma lazima kupata makaratasi lazima utumie njia kuoa hili ayapate??

Je ukimaliza kusoma ukataka kufanya kazi kwenye nchi hiyo hiyo ulipo soma na ukapata work permit si unaweza kufanya kazi bila kuoa??

Plz naomba jibu.
Inawezekana kupata makaratasi bila kuoa, zipo njia nyingi, kwa mfano unaweza kupata mchongo wa ukimbizi hiyo ipo sana kwa nchi za Canada, German na nchi nyingi za Scandinavia na Europe, pia kupata makaratasi bila kuoa inawezekana lakini in rahisi zaidi kwa kwa mtu Mwenye visa ya muda mrefu kama student visa kwa vile ana nafasi ya kuwepo muda mrefu ndani ya hiyo nchi,
 
umeeleza mubashara kabisa.
Sasa hapo inapotokea akaoa haijarishi ni rejected materials au la na akajikuta kwenye pingu za child support, je?

1.hiyo nusu ya kipato chake kwenda kwa mwanamke ni sheria?
2. Je kuna haja ya kusema nusu ya kipato cha mwanaume inaenda kwa mwanamke wakati wanaishi wote baba+mama+ mtoto?
3. Kwani baba si niwajibu wake kumtunza mtoto bila kupangia niasi gani kiende kwa mwanamke?
apo ni mkizinguana ndo hayo hutokea.
 
Kwanza unatakiwa kujua ya kwamba wazungu wanaheshimu vitu vifuatavyo
1 Wanawake
2 Mbwa au wanyama
3 Wanaume

Pia unatakiwa kujua ya kwamba si kuwa unapooa au kuolewa si hapo hapo unapewa uraia inaweza chukua miaka 3-10 kupata Citizenship utakacho pata ni Permanent resident ili uweze kufanya kazi wakati makaratasi yako ya kupata Citizenship yakishugulikiwa

Sasa ktk kipindi chote majaliwa yako ya kupata Citizenship yanakuwa juu ya mwanamke so ukimpiga au kimfanyia jambo lolote ambalo si lakiungwana kama kupiga akienda kusema ujue safari ya kurudi Africa inakuwa tayali kumbuka mwenye PR anaweza kufukuzwa ila mwenye citizenship hawezi kufukuzwa nakumbuka mwaka 2000 mama yangu alimpokea kaka yake kutoka Norway aliyekuwa ameoa kosa alimpiga tu mkewe alifatwa na Police kwenye kibarua chake na hakupata hata nafasi ya kuaga watoto moja kwa moja airport alichokuja nacho kutoka Norway kwa miaka yote 7 aliyekuwa huko alikuja na Rasta na tishet nyeupe pamoja na jinzi la Blue na raba za Nike


Kumbuka sisi wa Africa tuna tamaduni zetu na mila zetu ambazo ni kinyume na mila za wazungu yani ni kama amri kumi za Mungu na amri kumi za shetani yani hii usiue hii kill hii usiibe hii kaibe

Mwafrica wote tunaamini kuwa kichwa cha family ni mwanaume na kwetu hakuna haki Sawa tuna wajibu neno haki limebaki kwenye makaratasi tu

Lakini kwa wenzetu mwanamke ni mfalme wa family na wanaume ni mtafutaji wa family mwanamke ndio muhasibu wa family anataka kujua kila senti inayotoka kwa family inakwenda wapi?

ITAENDELEA............
umeniacha hoi apo uliposema alirudi na rasta na tshirt nyeupe kwa seven years!hah ha
 
Inawezekana kupata makaratasi bila kuoa, zipo njia nyingi, kwa mfano unaweza kupata mchongo wa ukimbizi hiyo ipo sana kwa nchi za Canada, German na nchi nyingi za Scandinavia na Europe, pia kupata makaratasi bila kuoa inawezekana lakini in rahisi zaidi kwa kwa mtu Mwenye visa ya muda mrefu kama student visa kwa vile ana nafasi ya kuwepo muda mrefu ndani ya hiyo nchi,
noted
 
Kwa uelewa wangu, mambo ya permanent residency(PR), work permit, citizenship ni mambo ya pesa tu. Kama pesa ipo we tafuta immigration law agency nzuri itakusaidia kiurahisi.

Sioni umuhimu wa mtanzania kuapply citizenship nchi za watu wakati PR ina uwezo wa kukusaidia katika mishe zako zote kihalali.
 
Marekani wamekukatalia makaratasi kwa sababu gani? Utakuwa una criminal record ya felony maana si kawaida kukataliwa makaratasi mara 3 kama una legal marriage certificate. Na kama ni kweli, then my friend you are doomed. Huwezi ku immigrate Canada au Australia.

Sina criminal record yoyote,sijawahi kushikwa na police wala sijawahi kupata ticket. Nafanya kazi kama kawaida sijawahi kukosa kulipa kodi. Kinachonifanya nifikirie kuhama nchi ni nipate nafasi ya kurudi nyumbani kuwaona wazazi na kurudi.
 
Inawezekana kabisaa Tatizo watu kutoka Africa wanashindwa kutofautisha kati ya Citizenship na Permanent resident kwa kujua Citizenship ni bora zaidi ya PR kwa mgeni wanashindwa kuvumilia miaka 5 -10 kupata Citizenship wanataka kupata Citizenship kwa muda mfupo ndipo wanajikuta wameoa rejected material kama Wazee,mabonge ,wajane na kujikuta wako under pressure kwani kile wanachokipata wanajikuta mke ndio mpanga matumizi na wanajikuta kwenye pingu za child support nusu ya kipato chote kinakwenda kwa mke

Pia ktk ndoa za kuoa haraka haraka unajikuta umeoa mwanamke ambae ni low class yani wanafanya kazi daraja la chini ambazo kipato chake ni kuanzia 500 - 2500 $

Lakini ukivumilia miaka 5-10 unaweza kupata uraia bila ya shida nchi nying baada ya kumaliza chuo wanakupa miezi 3 ya kutafuta kazi na ukipata kazi kama ni ya muda mrefu inapata PR tofauti ya mwenye PR na Citizens ni ndogo sana hasa hasa kwenye mambo ya siasa tu yani ww uruhusiwi kupiga kura tu lakini huduma zingine kama Afya, Elimu,Kijamii wote mnakuwa Sawa tu
Izzo is great person i like you soo much brother
 
Canada pako taiti sana pia Australia nako panazidi kuwa pafinye,
Chakufanya nenda Australia maana ndo kwenye unafuu na nirahisi kutoboa maana maisha ya kule ni cheap ukilinganisha na maisha ya canada.
Tafuta sponsorship za kule ukifika kule komaa tena ununue mwanamke umlipe mfunge ndoa upate makaratasi kule kidogo hawabani sana kwenye swala la ndoa.
Au upate host kutoka kule ukifika kule unafanya mchakato wa kubaki kule pia kule nursing inalipa sana japo itakubidi uingie tena darasani ndiyo upate work permit ukiwa Australia.
Kila lakher mkuu pambana nakutakia mafanikio mema.

Si kweli! Usimpotoshe jamaa, ili ufanikiwe kufika OZ kuna visa ya skill (ila lazima uwe umeisomea Oz au Some selected countries. Kuoa noo skushauri imeshakua too complicated, the easiest way ni kutumia student visa na usome zile demand course ikiwemo Nursing naukasome outback huko km Darwin au Cairns ni rahis zaid kupata papers.

Check na age yako isiwe kubwa sana tokaTonny abbot aingine dah kabadili vitu ni kusoma namba tu hadi Tanbul anaendeleza hayo hayo
 
Kwa uelewa wangu, mambo ya permanent residency(PR), work permit, citizenship ni mambo ya pesa tu. Kama pesa ipo we tafuta immigration law agency nzuri itakusaidia kiurahisi.

Sioni umuhimu wa mtanzania kuapply citizenship nchi za watu wakati PR ina uwezo wa kukusaidia katika mishe zako zote kihalali.

Kwa wapi??
 
Sina criminal record yoyote,sijawahi kushikwa na police wala sijawahi kupata ticket. Nafanya kazi kama kawaida sijawahi kukosa kulipa kodi. Kinachonifanya nifikirie kuhama nchi ni nipate nafasi ya kurudi nyumbani kuwaona wazazi na kurudi.
Sasa sababu gani umekataliwa greencard mara 3 zote ilhali umeoa Mmarekani?
 
Kwa wapi??
Si tunaongelea 1st world countries mkuu.

Hizo nchi nyingi ukiweza kuingia na kiasi fulani cha pesa au kununua property ya amount fulani unakuwa termed kama investor na unaqualify kupata PR, na ukihold PR kwa miaka kadhaa unaruhusiwa kuapply citizenship.

Na nchi nyingi ukiwa na PR nadhani unakuwa na haki zote kama raia except huwezi kupiga kura na haupewi passport.

Correct me if am wrong.
 
Inawezekana kupata makaratasi bila kuoa, zipo njia nyingi, kwa mfano unaweza kupata mchongo wa ukimbizi hiyo ipo sana kwa nchi za Canada, German na nchi nyingi za Scandinavia na Europe, pia kupata makaratasi bila kuoa inawezekana lakini in rahisi zaidi kwa kwa mtu Mwenye visa ya muda mrefu kama student visa kwa vile ana nafasi ya kuwepo muda mrefu ndani ya hiyo nchi,
Wakuu hivi mtu akiingia Canada kama mkimbizi, akaishi kama mwaka mmoja au miwili akitaka kuhamia USA inawezekana??? na kule USA akioa na akiishi kama miaka nane akiomba uraia anaweza kupewa ???? Wakuu nisaidieni
 
Back
Top Bottom