Inawezekana kabisaa Tatizo watu kutoka Africa wanashindwa kutofautisha kati ya Citizenship na Permanent resident kwa kujua Citizenship ni bora zaidi ya PR kwa mgeni wanashindwa kuvumilia miaka 5 -10 kupata Citizenship wanataka kupata Citizenship kwa muda mfupo ndipo wanajikuta wameoa rejected material kama Wazee,mabonge ,wajane na kujikuta wako under pressure kwani kile wanachokipata wanajikuta mke ndio mpanga matumizi na wanajikuta kwenye pingu za child support nusu ya kipato chote kinakwenda kwa mke
Pia ktk ndoa za kuoa haraka haraka unajikuta umeoa mwanamke ambae no low class yani wanafanya kazi daraja la chini
Lakini ukivumilia miaka 5-10 unaweza kupata uraia bila ya shida nchi nying baada ya kumaliza chuo wanakupa miezi 3 ya kutafuta kazi na ukipata kazi kama ni ya muda mrefu inapata PR tofauti ya mwenye PR na Citizens ni ndogo sana hasa hasa kwenye mambo ya siasa tu yani ww uruhusiwi kupiga kura tu lakini huduma zingine kama Afya, Elimu,Kijamii wote mnakuwa Sawa tu
Mkuu, hii 5-10 years unayozungumzia ni kwa wapi USA, Ulaya au wapi?
Siku hizi nchi nyingi wanaiga "point based system" ya Australia ambayo kwa ujumla inamkata mtu kama mleta mada.
Yaani katika mfumo huo wanaangalia mambo kama umri, elimu, kipato, akili kama imetulia na mambo kama hayo.
Hata Marekani nao wamesema wanataka kuingia huo mtindo ili kuwapata wengi.
Nchi zingine kama New Zealand na Canada wao bado wanaweza kutoa mwanya kama una vyeti vyako.
Suala la kuoa kwa nchi kama Uingereza wao wameweka kabisa kwamba mmoja wenu awe anapata mshahara wa kuanzia pauni 18,600 kwa mwaka bila ya makato ya kodi.
Ila mleta mada kwa hali yake ya kuwa tayari ni "overstayer" inakuwa ni vigumu kufanya next move labda kama anaamua tu kwamba achukue risk na akae tu huko US jambo ambalo ni hatari kwake.
Hili ndilo tatizo kwa vijana wengi kwamba unapokuwa kwenye nchi kama USA usisahau kulipa kipaumbele suala la makaratasi.
Sasa mtu yupo ndani ya eneo la tukio na anashindwa kufunga goli.
Kuhusu mke wako huwezi kumuoa kama huna karatasi ila utaweza kumuoa kama hujaoza na umerudi Tanzania halafu atakuja kukuchukua, na kwanini mmekaa miaka sita sasa na hujaweza hata kupata angalau katoto kamoja ka kuwafanya jamaa wakuhurumie?
Ungekuwa na mtoto ungeweza kuwa unakwenda kukasalimia na kumuona mama na hapo ungejenga trust kuwa unashiriki kumkuza mtoto.
Narudia tena kama huna karatasi una nafasi ndogo sana ya kuzunguka.