Utamtafuta mshenga kwa kusaidiana na binti(mshenga sanasana anakuwa anajua taratibu zote anawadirect kila hatua naye ndo anakuwa msemaji mkuu)
Baada ya hapo mtapanga siku ya kwenda kujitambulisha, tarifa zitatolewa na mtakaribishwa kabla ya yote na wala hamjaanza mazungumzo kuna hela ya kupita mlangoni na ya mkeka(mlangoni 500k na mkeka 100k ),mkishalipa hiyo hela mtaruhusiwa kuingia ndani mtakaa na kuanza kuongea.
Mazungumzo yenu ni pamoja na kujileza nyie ni akina nani na dhumuni la kuwa pale.
Baada ya hapo wataleta orodha ya vitu vinavyotakiwa ili uweze kumchukua binti yao
Mfano,ni mfano tu jamani
Suti ya baba 150000
Hela ya mama mfano simitank ltr 5000 na kg 25 sukari
Baba wadogo.150000
Wajomba. 150000
Shangazi 10000
Mama wadogo 10000
Kaka zake 150000
Blanket ya bibi. 50000
Hela ya babu 10000
Hela ya wazazi wa kiroho. 50000
Mahari millioni 6
Baada ya kusoma hiyo karatasi mtaangalia ikiwa mnaweza kuanza kulipa hivo vitu mnalipa mda huo huo(na huu ndo mda wa mshenga kuwasaidia kubagain yaani inaweza pungua kutoka 100k kuja mpaka 50k hapo ni umahiri wenu kwenye kujitetea na kutia huruma)kwa hapa mtalipa vile mtavyoweza na vinavyobaki mtaenda kujipanga tena.mfano mnaweza maliza vile vingine alafu mahari mkajipanga siku nyingine.
Cha muhimu mtabagain ukiwa na hela mkononi
NOTE.
Gharama hizo zinatofautiana kulingana na family status lakini pia status ya binti(educated vs non educated kuna tofauti kubwa kwenye mahari)
Lakini pia njia ya kuoa,ukienda kuchumbia direct ndo utakutana na gharama za kutosha,ukioa ile ya usiku ukija unapigwa faini halafu gharama zinakuwa ndogo sana
Na mwisho,mahari unaweza kukopwa umalize taratibu taratibu hapa kuna watu wanazeeka mpaka hawajamaliza mahari,ila ukifata process zote kuna heshima fulani.
MWISHO
Unapoenda kujiintroduce jitahidi uwe na vichenji angalai si chini ya 1M la sivyo utaishia mlangoni