Kiumbe duni
Senior Member
- Dec 3, 2011
- 100
- 8
Kuna ndugu yangu eneo lake limekodishwa na kampuni ya tigo kuweka mnara. Kutokana na kutokuifahamu lugha ya kiingereza akaingia mkataba unaombana ambapo walikubaliana atalipwa laki 5 kila mwezi kwa mwaka, na ktk kodi yake itakatwa kodi 10%. Walisaini nae mkataba wa miaka 20 na wakamwambia kila baada ya miaka mi5 watakaa mezani kujadili upya kodi. Baada ya miaka mi5 kupita akawafuata ili wajadiliane kodi wakamwambia hakuna kipengele hicho kwenye mkataba wao. Kweli mkataba wake unasema ktk hiyo miaka 20 kodi itakuwa automatically renewed kila baada ya miaka mi5 ya bila badiliko la kodi.
Maswali yake ni kama yafuatayo:
(1) Afanye nini ili aweze kuubadili mkataba huu.
(2)Kama akiuza eneo lake anaweza kupata tatizo lolote.
Wadau msaada wenu unahitajika. Nawasilisha
Maswali yake ni kama yafuatayo:
(1) Afanye nini ili aweze kuubadili mkataba huu.
(2)Kama akiuza eneo lake anaweza kupata tatizo lolote.
Wadau msaada wenu unahitajika. Nawasilisha