Hahaaa,nimecheka!
Mi nilifuata taratibu za kawaida kabisa,za 150,ila sikufanya Mimi,nilienda uhamiaji palepale mkoani huko,hiyo ofisi inayohusika ktk story kumbe duh tunafahamiana kiasi,nikasema hapahap nikamwambia shida yangu!huyo mtu pale uhamiaji ana komputa yake ,ndo alinifanyia kila kitu,akajaza hizo form nikalipa 20,akaprint mwenyewe,akamcheki mwanasheria chap akatengenez affidavit ya baba na mama,faster ikaletwa hapohapo ofisini,si unajua mikoani sio km dar ofisi zipo jiranijirani!
Baada ya kuprint tukakaa ofisini hapo akanisaidia kujaza chap,nikalipa hiyo 130 iliyobaki! Basi akaniambia njoo kesho tukamilishe!
Kweli kesho yake nikaenda nikaingizwa kwenye picha,fingerprints mchezo ukawa umeisha! Sa kwa style hii utaacha kumpa mtu hela!? Niliona aibu aisee nikampa 50 elf...nikasepa,14 days passport tayari!si kuhangaika chochote,sikutaka kufanyia dar mambo mengi huku na sikuwa na haraka nayo pia