Msaada: Jinsi ya ku-block email usizozitaka.

Rubi

JF-Expert Member
Oct 5, 2009
1,615
326
Wataalamu naombeni msaada wa jinsi ya kuzi-block e-mail usizozitaka mfano hizi zinazotangaza viagra n.k maana siku hizi nimekuwa nakerwa sana na hizi email maana imekuwa ndio fasheni ukifungua unakuta email imetumwa na mtu ambaye yuko kwenye contact zako au wakati mwingine hata imejiandika jina lako lakini inaandika no subjet ukifungua unakuta hakuna kitu kingine zaidi ya link za ajabuajabu tena unakuta hizo link zimetumwa mpaka kwenye email za watu unaowaheshimu ambao umesevu email address zao kwenye address book. kiasi inakuwa kero.

Msaada jamani nikifanikiwa kuzi- block nitashukuru sana. maana zinanikera kupita maelezo.
 
Mi nilifikiri peke yangu! ngoja kwanza tuwaone ma IT watusaidie
 
nadhani uki-right click ama ukii-tick then ukiangalia hapo juu utapata options. angalia jinsi ya ku-report kama spasm. unaweza kuweka option ya filter,japo inasumbua coz kuna baadhi ya adress hasa za makampuni zitatupwa huko. gmail ina unafuu haileti hayo matakataka
 
Kweli kabisa, huu mchezo sijui unafanywaje. E-mail moja inahusu tumiaji wa viagra na dick enlargement pills ilipokelewa na wafanyakazi kibao eti ina toka kwa Mama mmoja wa heshima zake. Watu walishangaa sana huyu mama ameanzisha biashara hiyo? Lakini kumbe hata yeye alishangazwa na kuwa taarifu staff wenzake siyo yeye mtumaji. Anyway tulimuelewa lakini ilileta usumbufu kiasi.
 
ukipokea mail kama hizo kwanza usizifungue. ni hatari. e mail nyingi za namna hiyo ni za ulaghai (fraud au spam) na zina kuwa zimeambatana na
program za kompyuta ambayo inakopi anwani za watu wako wote kwenye adress book na mara nyingine hukopi pia passowrd yako jina lako na mawasiliano yako yote na kutuma kwa aliyekutumia hiyo email . program hizo huitwa spyware au ke loggers na huwezi kuona kwani zinafanya kazi hizo kwenye background! wanaokutumia ni wataalam wa mifumo ya kompyuta wanotumia intaneti kuiba password za watu za benki, au utambulisho wako(identity fraud) na habri zako lakni mara nyingine ni matangazo ya biashara ambayo huyahitaji. Lakini uwe makini pia kutoa email yako kwenye websites unapokuwa kwenye intanet, ukikuta website inakulazimisha kuingiza email yako ndio uendelee basi ifunge na uachane nayo kama sio ya msingi.
 
nadhani uki-right click ama ukii-tick then ukiangalia hapo juu utapata options. angalia jinsi ya ku-report kama spasm. unaweza kuweka option ya filter,japo inasumbua coz kuna baadhi ya adress hasa za makampuni zitatupwa huko. gmail ina unafuu haileti hayo matakataka
King'ast asante kwa maelekezo yako nimeajaribu njia hii naonaina work lakini swali langu ni je zile email za ajabu walizotumiwa wanatumiwa ndugu, jamaa na rafiki zangu kwa jina la email yangu nazo zitakoma? au wao wataendelea kuzipata kwa jina langu na hali mimi nitakuwa sijui kitu? nieleweshwe tafadhali.
 
Alichokuambia Kin'gasti ndo chenyewe, ucw na hofu juu y email za watu wengine. Itachagua uliyochagua kuwa kama spam. Ila kama ukichagua kufilter kabla ya kuempty folder la spam lifungue kwanza maana inaweza kuwa na email ya muhim. Unajua haya matechnolojia hayako pafect
 
Kuhusu zile email, waombe tu samahani waliotumiwa hizo takataka. Muhimu ni kujua kuwa hutajaribu kufungua email ambayo huijui, ukifungua tu imekula kwako. Niliwah kuwa na tatizo kama hilo nikagundua zilitumwa from my box, yaan nilizikuta kwenye sent item, nikagundua wamehack paswedi yangu. Nikabadilisha pasword ujinga ukaisha. Pole sana!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom