Msaada jamani! Yamenifika

Msaada jamani! Yamenifika

ruhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
5,032
Reaction score
8,072
Nawasalim wana MMU,

Mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa MMU na nimepata kujifunza mambo mengi sana lakini kuna jambo limenitokea naombeni ushauri wenu.

Kwa sasa ninaishi Dar nimetokea kumpenda mdada mmoja yuko Shinyanga (ndiko anakoishi), kwa sasa yapata miezi saba tokea tujuane (tulikutana Shinyanga nilienda kusalimia ndugu); mimi ninafanya kazi kwenye kampuni ya ujenzi (temporary) na huyu dada anayo saloon ya kike hapo shinyanga mjini.

Tatizo langu linakuja kwenye suala la pesa; kwani kila mara nikipokea simu yake baada ya kujuliana hali anaomba pesa mara shampuu na mafuta mengine zimeisha za saloon mara nimtumie pesa za matumizi mara wateja wamepungua sana anadaiwa kodi la nyuma (saloon).

Yote hayo yaweza kua sahihi lakini linapokuja suala la mafuta na shampuu huwa nashindwa kuelewa make haviwezi kuisha bila kuingiza pesa kwani zinatumika kwa wateja, pili kwa nini anapiga simu akiwa na shida la pesa tu? yungali tuko wachumba?

Mimi nilishamweleza hali halisi ya kipato changu na msaada ambayo twaweza kusaidiana, lakini niliona kama hajaelewa make alikua akipiga simu analalamika mithili ya mtu anaelia kitu ambacho sipendezwinayo. Kutokana na hiyo hali nilipanga safari adi Shinyanga wiki mbili zilizopita wala sikuona hali mbaya sana kwenye saloon yake, kurudi Dar baada ya wiki moja ameanza tena mara anataka kuleta mfanyakazi anejua kusuka vizuri kwa hiyo nimsaidie kulipa mara amepata chuo uku Dar kuna kozi anataka kuja kusoma nimchangie,,jamani!

Naombeni ushahuri huyu mdada anayo nia nzuri na mahusiano YETU? au anataka kula PESA na kusepa?
MUHIMU: SIJAWAI KUFANYA NAE MAPENZI
 
Umeingia choo cha kike achana naye huyo ni kibaka nahapo bado hujamuweka ndani huyo ni wawenzio ndg
 
Kumbe hauwajui wadada wa saluni!!! habari ndio hiyo na ulipoingia tu saluni akatabasamu ulipotoka tu akabinua midomo,tafuta mwanamke mwingine
 
Yaani hapo mwisho ndio umenilegeza kabisaaa..!
 
wadada wa salon ni noma.
Kabla sijamaliza kusoma nilishapredict mwisho wake.
Kimbia mkuu umegeuzwa chumio
 
Nilimpenda sana, ila nimeshtuka sana....ni kweli wadada wengi wa saloon wako ivyo?
 
Hapo hamna mapenzi....
Kama una uwezo wewe hudumia tu , si papuchi yake anakupa ila usitarajie makubwa kivile kutoka kwenye hayo mahusiano.
 
Dah sijasikitikia pesa zako ila nimesikitika wewe kutokupewa naniliu....
 
Ka apply ule msemo usemao "mapenzi ulaya,,,bongo pesa,," MPOTEZEE,,, mapenzi ya shy na dar ,,kuumia kunakuhusu,,,,
 
Hilo swali kama ana nia nzuri na mahusiano yenu ungemuuliza yeye angekupa jibu zuri na la uhakika zaidi.
 
Kweli Mapenzi hayana adabu,,,,,kwamba shy na mikoa jirani hawajamuona huyo mdada mpaka uje umkute wewe wa dar???
 
Stuka!!! Chapa lapa kabla hujachunwa zaidi.
 
Hilo swali kama ana nia nzuri na mahusiano yenu ungemuuliza yeye angekupa jibu zuri na la uhakika zaidi.

Hilo nilimuuliza akajibu simple kua asingekua ananitafuta mara kwa mara
 
Back
Top Bottom