Msaada interview: are you currently working now??

Msaada interview: are you currently working now??

jokielias

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
1,210
Reaction score
363
Habari wadau,
poleni Kwa wale wote ambao tunatafuta Ajira.
Hii Mada nimeanzisha ili tuweze kusaidiana Katika kujibu hili swali.
Inaweza kuwa swali rahisi lakini ikawa swali la mtego, na wengi wamefeli interview Kwa hilo swali.
Are you currently working now??
Hili ni swali ambalo Kwa wakati mwingine, inabidi uwe mwangalifu kwasababu ukisema Ndio nafanya kazi lakini nimeapply kazi kwenu kwasababu mnatafuta mtu mwenye uzoefu wa kazi. Inaweza kuwa tayari umejichinja. Maana inawezekana mwajiri anatafuta mtu ambaye hana kazi.
Na hili swali, inawezekana HR wa private sector haitawasumbua Sana, kwasababu wanatafuta mtu mwenye experience.
Ila kama unafanya interview government na ukaulizwa hilo swali ukasema Ndio unafanya kazi kampuni X. Tayari wazee wa utumishi wanakufyekelea mbali.
Je, ni jibu gani inaweza kukuweka mahali salama kwenye interview.
Naombeni msaada hapo.
 
Hilo ni swali la kipuuzi sana ,,Mimi kuna katasisi kaliniitaga kwenye usaili wakauliza swali kama hilo nikawajibu kwani kwenye CV yangu hamjasoma?, wakauliza swali lingine la unataka tukulipe kiasi gani nikawajibu 3.5million, wakasema kwainini nikawajibu MTU mwenyewe degree, CPA(T) mnataka mulipe shingapi,, kadada kakasema 1.5mill nikawajibu tafuteni wenye diploma huko,,, lingine swali eti umeoa, unamiliki nini?, na mengine mengi ya kijinga tuu,,,,
 
Akikuuliza hivyo mwambie kwanza arudi akajifunze kingereza cha ufasaha, hawezi weka curently na now sehemu moja. Turudi kwenye swali, unaweza kujibu ndio nina fanya kazi na nimeomba kazi kwenye kampuni yenu sababu ninatafuta kuendeleza zaidi ujuzi wangu unaweza kutaja majukumu machache unayofanya ulipo na utakayoongeza hapo ulipoomba hiyo nafasi (according to JD) pia unaweza kuongelea proffesional growth, last kama una sababu binafsi unaweza kusema umeomba nafasi hapo kwao sababu labda unataka kuwa karibu na familia na vile itakufanya uweze kuwa calm na utaweza fanya kazi kwa ufanishi, labda sehemu kazi ilipo ni karibu na familia yako.
 
tatizo inakuja pale unapofanya interview serikalini na mnajua jinsi jamaa walivyokuwa hawana huruma. Ukisema ukweli tayari wazee wa utumishi wamekufyekelea mbali. Msaada hapo tafadhali
 
Ulifanikiwa kupata ajira hapo kweli???
Hilo ni swali la kipuuzi sana ,,Mimi kuna katasisi kaliniitaga kwenye usaili wakauliza swali kama hilo nikawajibu kwani kwenye CV yangu hamjasoma?, wakauliza swali lingine la unataka tukulipe kiasi gani nikawajibu 3.5million, wakasema kwainini nikawajibu MTU mwenyewe degree, CPA(T) mnataka mulipe shingapi,, kadada kakasema 1.5mill nikawajibu tafuteni wenye diploma huko,,, lingine swali eti umeoa, unamiliki nini?, na mengine mengi ya kijinga tuu,,,,
 
  • Thanks
Reactions: DVC
alafu kwa sababu hili swali linaulizwaga kingereza basi muweke majibu ya kingereza wakati mnatoa majibu. Msilete mambo ya walimu wa kingereza kutoka tz
 
alafu kwa sababu hili swali linaulizwaga kingereza basi muweke majibu ya kingereza wakati mnatoa majibu. Msilete mambo ya walimu wa kingereza kutoka tz
[/QUOTE

Hilo swali ni la mtego Mbaya Sana halafu ukute hio interview Mpo candidates 100. Aisee Inabidi utunge uongo Tu hamna namna.
wadau wengine nafakiri watakuja kutoa Msaada zaidi.
 
wakati mwingine tunatumia uwongo ili tufanikiwe, na sio dhambi kubwa maana, maisha ni sehemu ya mapambano.
 
Ulifanikiwa kupata ajira hapo kweli???
Sidhani kama alipata kwa haya majibu japo alikuwa sahihi, interviews nyingi especially ma HR wasiojielewa huwa wanauliza maswali ambayo ni irrelevant kabisa to the actual job function.
 
Msaada interview: are you currently working now??

Kwa Kiingereza chako kwenye heading ya thread yako, je, neno 'currently' na 'now' yana tofauti kweli?
 
  • Thanks
Reactions: a45
Mimi nimekuja kuangalia hii lugha uliyotumia


"ARE YOU CURRENTLY WORKING NOW?

mbona sentensi sio sahihi
 
  • Thanks
Reactions: a45
Keanu kila kazi lazima uipate?.. .nyengine zinakusaidia kuongeza experience
....kuwa mkweli hi.. ..
 
Mkuu nafikiri uungwana ni kumrekebisha kama amekosea au lah! mana yeye ameuliza swali na wewe umeuliza swali
Msaada interview: are you currently working now??

Kwa Kiingereza chako kwenye heading ya thread yako, je, neno 'currently' na 'now' yana tofauti kweli?
 
mi nadhani mada inaeleweka, pamoja kwamba ni broken english. ila ujumbe umefika, wadau wangemsaidia huyo mhanga na wahanga wengine, jinsi ya kujibu hio swali ili waweze kufaulu interview.
 
Back
Top Bottom