Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Wana JF
Habari za masiku. Kuna binti mmoja rafiki yangu ( msinishambulie sio mpenzi wangu ni rafiki tu basi) amekwisha mpata wake na wameamua kuishi pamoja. Binti ni muislamu na kijana mkatoliki. Kimsingi wamekwisha kukubaliana kuwa mke na mme. Binti alimpa baba yake taarifa kitambo sana. Baba alileta ubishi kwa kuzingatia tofauti ya udini. Binti alisimamia msimamo wake na pia aliahidi kuwa hatobadilisha dini na kuwa mkiristu. Baba alikubaliana na binti yake. Tarehe zikasonga mbele na binti akawa anamwambia baba yake kuwa upande wa kiumeni wanataka kuja kujitambulisha. Danadana zikaanzia hapo. Mara keshokutwa mara mtondogoo. Binti alivyoona ubabaishaji unazidi akamwambia kuwa mume wake mtarajiwa anataka kufungoa harusi mapema mwakani ( Yaani January 2012 mwanzoni). Binti akaweka msimamo kuwa hatohitaji makuu ila anaomba baraka zake. Mzee akajitutumua akamwambia binti kuwa hawezi kuolewa mpaka amfanyie send off! Binti akamtii baba yake! Vikao vikaanza vya hapa na pale! Tarehe zimefika mzee anaulizwa anasema kuwa anazo ka shs laki nne tu! Kuwa rafiki zake hawakumchangia na mbaya zaidi naye kakimbilia kwa mkewe Nairobi. Na hata hiyo laki nne anayo yeye. Binti amebakia njia panda anaomba ushauri wenu afanyeje?
Anasubiri ushauri wenu.
Habari za masiku. Kuna binti mmoja rafiki yangu ( msinishambulie sio mpenzi wangu ni rafiki tu basi) amekwisha mpata wake na wameamua kuishi pamoja. Binti ni muislamu na kijana mkatoliki. Kimsingi wamekwisha kukubaliana kuwa mke na mme. Binti alimpa baba yake taarifa kitambo sana. Baba alileta ubishi kwa kuzingatia tofauti ya udini. Binti alisimamia msimamo wake na pia aliahidi kuwa hatobadilisha dini na kuwa mkiristu. Baba alikubaliana na binti yake. Tarehe zikasonga mbele na binti akawa anamwambia baba yake kuwa upande wa kiumeni wanataka kuja kujitambulisha. Danadana zikaanzia hapo. Mara keshokutwa mara mtondogoo. Binti alivyoona ubabaishaji unazidi akamwambia kuwa mume wake mtarajiwa anataka kufungoa harusi mapema mwakani ( Yaani January 2012 mwanzoni). Binti akaweka msimamo kuwa hatohitaji makuu ila anaomba baraka zake. Mzee akajitutumua akamwambia binti kuwa hawezi kuolewa mpaka amfanyie send off! Binti akamtii baba yake! Vikao vikaanza vya hapa na pale! Tarehe zimefika mzee anaulizwa anasema kuwa anazo ka shs laki nne tu! Kuwa rafiki zake hawakumchangia na mbaya zaidi naye kakimbilia kwa mkewe Nairobi. Na hata hiyo laki nne anayo yeye. Binti amebakia njia panda anaomba ushauri wenu afanyeje?
Anasubiri ushauri wenu.