Topic ya kiswahili kingereza cha nini? au unataka tujue na wewe unakijua.
kumbukumbu la torati 21:15-16
iwapo mtu yu na wake wawili mmoja hampendi mwingine ywampenda na wote wamemzalia wana isije ikatokea huyu ambae hapendwi akanyimwa mtoto wake urithi wa mzaliwa wa kwanza.
maneno siyo rasmi ila nimeona biblia inatambua ndoa ya wake wengi. labda kwa anayetaka kuwa askofu
YOHANA 4:16-18
16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. 17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume. 18 Kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.
kanisa gani litakuwa tayari kukufungisha ndoa ya pili?labda udanganye tu au huyo wapili mweke hawara yako mzini vizuri na kama ungekuwa mkristo na unaijua dini yako na biblia vizuri tangu sunday school sidhani kama ungeuliza huu utumbo hapa.nna mashaka we sio mkristo au ni wale mwaka mzima unawapita bila kushika bible! upuuzi mtupu!!!
Habarini wadau,
Wakristo wengi wanaamini kuoa mke mmoja ndiyo sahihi kulingana na imani yao lakini biblia hiyohiyo inasomeka dhahiri jinsi Suleimani na Daudi waliokuwa vipenzi wa Mungu walivyooa wake wengi sana.Si hao tu ila wapo wengine pia.
Ni wapi Mwenyezi Mungu alipolazimisha uoaji wa mke mmoja tu? Yeye Muumba hajui kuwa idadi ya wanawake kubwa sana kuliko wanaume? Je ni dhambi kuoa wake wawili au zaidi ikiwa naweza kuwahudumia vyema? Hili si ni bora zaidi kuliko kufanya zinaa na michepuko? Tujadiliane
Msaada wenu nauhitaji.