Msaada hatua za kufuata ili kubadili jina kisheria

mFuKuZa nDoTo

JF-Expert Member
Jan 17, 2021
492
635
Wakuu, Poleni na majukumu ya kila siku, nisiwe na maneno mengi naomba nijikite moja kwa moja kwenye mada husika. Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza, binafsi kadri siku zinavyosonga najikuta nahusudu zaidi uafrika na kutupia mbali uzungu.

Spirit hii imeanza kunikaa kwa kiasi cha kutisha lakini kinachonipa raha sana. Unapozungumzia kuachana na uzungu watu wengi huja na hoja mbalimbali ambazo mara zote kwangu huwa naona hazina mashiko, mfano mtu anasema kama hutaki uzungu basi acha kutumia simu zao, acha kuvaa nguo zao, acha kupanda magari yao, usitumie kijiko nk.

Siwezi kuacha kutumia simu kwa sababu hata wazungu wasingekuja bado tungefika huku maana ni maendeleo ya kiteknolojia na ikumbukwe tulikuwa na teknolojia yetu, viwanda, imani na mfumo wetu wa elimu ambapo walilazimika kuviua ili kunyanyua vyao. Kwahiyo hata wasingekuja bado tungetransform kutoka kuvaa magome na kuvaa nguo, tungeacha punda na kuendesha magari tena pengine tungekuwa mbali zaidi.

Hivyo Basi, kwa mtazamo wangu (Narudia tena KWA MTAZAMO WANGU...maana kuna watumwa wa kifikra watadandia tu mjadala utafikiri tunapangiana) nikaona vita kubwa nielekeze katika mfumo wao wa kiimani hasa kuabudu, huko nilishafanikiwa kuachana na dini za kimapokeo na niko very proud kufanikisha hilo.

Pili niliamua kuachana na majina ya kizungu, kwa kuwa mimi sio mtu wa maneno bali vitendo nilianza kwa kuwapa wanangu majina ya asili ya kabila langu, nikishindwa kabisa nitawaita majina ya kiswahili. Kilichonishangaza kila mmoja ananishangaa kijana kabisa naita majina ya ajabu watoto na kuna majina mazuri kabisa ya kizungu, Nikiri wazi kabisa hili suala lilinisikitisha kuliko kawaida na kila nikitembea bado linavinjari kichwani kwangu, ni kwa kiwango gani waafrika tumekuwa malofa na wapumbavu kiasi hiki, Yaani kuna mtu mweusi kona moja ya Afrika katika zama hizi anaamini jina la kizungu ni bora kuliko la kiswahili.

Sasa nijielekeze kwenye hitaji la uzi huu, nina majina matatu, langu la kilugha, la katikati la kizungu, la mwisho la kilugha
Shida iko hapo katikati, hilo jina linanikera mno, silipendi kabisa kwahiyo naomba msaada wenu juu ya hatua ya kuchukua katika haya

(A)
Je, kuna haja ya kumjulisha mwenye jina?(Mzazi)
Je, anaweza kukubali?
Je, akikataa naweza kulazimisha?
Je, nikilazimisha naweza kupatwa na laana?

(B)
Naomba kuelekezwa hatua za kisheria kwa ujumla, gharama na muda wa kutimia kwa jambo

Nawasilisha.
 
Hata mimi nina jina la "Kiarabu" katikati linanikera kama nini.,

Mimi mwenyewe nimeweza kama wewe ila shida ipo hapa katika kuna katiba ka Kiarabu eti SEFU pumbavu
 
Pole Sana mkuu, jina si chochote si lolote katika uhalisi wa maisha na hasa katika swala la namna ya kuwa mwafrika! Naskitika kwamba u mtumwa wa Uafrika kiasi kwamba unaamini ukiitwa Mangungo na si John ndo Uafrika huo!

Mwisho unaweza ukawa Ngonyani lakini ukawa na tabia za hao unaohisi kwamba Ni wao walioturudisha nyuma kiteknolojia.

Ohh Afrika na mwafrika tunakwama wapi Ni miaka karibu 60 Sasa Afrika ( sehem kubwa) iko huru lakini tupo wapi?

Tunaagiza Hadi vikombe vya udongo! Wembe! Ha ha na mipira ya kule sirini.

Umbumbumbu kiasi gani.
 
Pole Sana mkuu, jina si chochote si lolote katika uhalisi wa maisha na hasa katika swala la namna ya kuwa mwafrika! Naskitika kwamba u mtumwa wa Uafrika kiasi kwamba unaamini ukiitwa Mangungo na si John ndo Uafrika huo!
Mwisho unaweza ukawa Ngonyani lakini ukawa na tabia za hao unaohisi kwamba Ni wao walioturudisha nyuma kiteknolojia..
Ohh Afrika na mwafrika tunakwama wapi Ni miaka karibu 60 Sasa Afrika ( sehem kubwa) iko huru lakini tupo wapi?
Tunaagiza Hadi vikombe vya udongo! Wembe! Ha ha na mipira ya kule sirini.
Umbumbumbu kiasi gani.
Shida sio madhara yatokanayo na jina la kizungu, najua hakuna shida yoyote

Lakini kwa mapenzi tu sitaki jina la kizungu

Kutotaka jina la kizungu ni tatizo?
 
Kama umri wako bado unaishi chini ya wazazi endelea kutumia chini ya kifungu.

Ila umri ukiwa ni ule wa kujitambua na kunajitegemea basi fanya unaloona ni haki ya nafsi yako ili mradi hauvunji sheria za nchi yako.
Amen
 
Fanya kile kinakufurahisha

Nakumbana na kadhia kama yako

Nikipata upenyo nabadili jina la katikati
 
Mkuu nkupongeze kwa kuamua kirudi ktk uafrika nowdays kumekuwa na idadi kubwa ya watu ambao wameanza kujitambua kifikra... na kutaka kirud kwenye uafrika wetu mm ni mmoja wapo...Na hapa npo ktk mchakato wakutaka kubadili majina yangu..

Majina ye2 ya kiafrika yana nguvu sana na nisehem ya mafanikio ktk maisha... nikupe mfno nguvu ilyo kwenye majina ye2 ya asili ukikuta mtu anatumia majina ya kiarabu au yakizungu lkn katkat ya majina hayo kukawa na jina la kiafrika bac mtu huyo utakuta jina analoitwa na watu wengi ni lakiafrika mfano january makamba unakuta makamba ndio lenye nguvu zaid sasa nguvu hz pia hupekelekea kwenye bahati na mafanikio maisha...

kuhusu hilo la teknologia nenda kachimbue habari za kabila linaloitwa Dogon hawa jamaa wako pale mali na wamejitenga wapo jangwani kabisa hawataki kuchanyana na waarabu wala wazungu weusi hawa jamaa asili yao ni Misri baada ya waarabu kuingia Misri na kuanza kulazimisha watu kuacha asili zao na kuingia ktk dini ya uislam hawa jamaa waligoma na kuamua kuondoka misri kufupi story...hawa jamaa wanaelemu kubwa sana vtu ambavyo dunia ya leo wanaangaka navyo wao elimu hyo walikuwa nao ktambo na walishagundua v2 kama simu karne nyingi sana zilipita lkn hutokaa usikie habari hz bila kuwa mfuatiliaji...matokeo yke watu wanaamin kila ki2 kinatoka kwa mzungu. Ila habari mbaya ni kwamba inatumika nguvu kubwa kuwauwa hawa jamaa wakiwatumia waarabu weusi(waafrika waislam) wa pale mali kwa jina la jihadi.
 
Mkuu nkupongeze kwa kuamua kirudi ktk uafrika nowdays kumekuwa na idadi kubwa ya watu ambao wameanza kujitambua kifikra... na kutaka kirud kwenye uafrika wetu mm ni mmoja wapo...Na hapa npo ktk mchakato wakutaka kubadili majina yangu..

Majina ye2 ya kiafrika yana nguvu sana na nisehem ya mafanikio ktk maisha... nikupe mfno nguvu ilyo kwenye majina ye2 ya asili ukikuta mtu anatumia majina ya kiarabu au yakizungu lkn katkat ya majina hayo kukawa na jina la kiafrika bac mtu huyo utakuta jina analoitwa na watu wengi ni lakiafrika mfano january makamba unakuta makamba ndio lenye nguvu zaid sasa nguvu hz pia hupekelekea kwenye bahati na mafanikio maisha...

kuhusu hilo la teknologia nenda kachimbue habari za kabila linaloitwa Dogon hawa jamaa wako pale mali na wamejitenga wapo jangwani kabisa hawataki kuchanyana na waarabu wala wazungu weusi hawa jamaa asili yao ni Misri baada ya waarabu kuingia Misri na kuanza kulazimisha watu kuacha asili zao na kuingia ktk dini ya uislam hawa jamaa waligoma na kuamua kuondoka misri kufupi story...hawa jamaa wanaelemu kubwa sana vtu ambavyo dunia ya leo wanaangaka navyo wao elimu hyo walikuwa nao ktambo na walishagundua v2 kama simu karne nyingi sana zilipita lkn hutokaa usikie habari hz bila kuwa mfuatiliaji...matokeo yke watu wanaamin kila ki2 kinatoka kwa mzungu. Ila habari mbaya ni kwamba inatumika nguvu kubwa kuwauwa hawa jamaa wakiwatumia waarabu weusi(waafrika waislam) wa pale mali kwa jina la jihadi.
Nafurahi unafahamu ukuu wa jina katika ulimwengu wa kiroho
Wapo wanaosema jina halibadili chochote, si kweli jina lina uwezo wa kuathiri maisha ya mhusika moja kwa moja, jina humuunganisha mhusika na mizimu ya babu zake na hapa watu wanaleta imani za kishirikina lakini ndio ukweli, kuna wakati huwa nahisi huenda bara letu haliendelei sababu hatuna connection na Miungu wetu kwa kuwa tumewatelekeza.
Mistari minne ya mwisho ni habari mbaya zaidi

Binafsi nataka jina nitakalofahamu maana yake, lenye asili yangu

Nisipotekeleza hili sitakuwa na amani, nafsi yangu inanidai sana
 
Wakuu, Poleni na majukumu ya kila siku, nisiwe na maneno mengi naomba nijikite moja kwa moja kwenye mada husika. Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza, binafsi kadri siku zinavyosonga najikuta nahusudu zaidi uafrika na kutupia mbali uzungu.

Spirit hii imeanza kunikaa kwa kiasi cha kutisha lakini kinachonipa raha sana. Unapozungumzia kuachana na uzungu watu wengi huja na hoja mbalimbali ambazo mara zote kwangu huwa naona hazina mashiko, mfano mtu anasema kama hutaki uzungu basi acha kutumia simu zao, acha kuvaa nguo zao, acha kupanda magari yao, usitumie kijiko nk.

Siwezi kuacha kutumia simu kwa sababu hata wazungu wasingekuja bado tungefika huku maana ni maendeleo ya kiteknolojia na ikumbukwe tulikuwa na teknolojia yetu, viwanda, imani na mfumo wetu wa elimu ambapo walilazimika kuviua ili kunyanyua vyao. Kwahiyo hata wasingekuja bado tungetransform kutoka kuvaa magome na kuvaa nguo, tungeacha punda na kuendesha magari tena pengine tungekuwa mbali zaidi.

Hivyo Basi, kwa mtazamo wangu (Narudia tena KWA MTAZAMO WANGU...maana kuna watumwa wa kifikra watadandia tu mjadala utafikiri tunapangiana) nikaona vita kubwa nielekeze katika mfumo wao wa kiimani hasa kuabudu, huko nilishafanikiwa kuachana na dini za kimapokeo na niko very proud kufanikisha hilo.

Pili niliamua kuachana na majina ya kizungu, kwa kuwa mimi sio mtu wa maneno bali vitendo nilianza kwa kuwapa wanangu majina ya asili ya kabila langu, nikishindwa kabisa nitawaita majina ya kiswahili. Kilichonishangaza kila mmoja ananishangaa kijana kabisa naita majina ya ajabu watoto na kuna majina mazuri kabisa ya kizungu, Nikiri wazi kabisa hili suala lilinisikitisha kuliko kawaida na kila nikitembea bado linavinjari kichwani kwangu, ni kwa kiwango gani waafrika tumekuwa malofa na wapumbavu kiasi hiki, Yaani kuna mtu mweusi kona moja ya Afrika katika zama hizi anaamini jina la kizungu ni bora kuliko la kiswahili.

Sasa nijielekeze kwenye hitaji la uzi huu, nina majina matatu, langu la kilugha, la katikati la kizungu, la mwisho la kilugha
Shida iko hapo katikati, hilo jina linanikera mno, silipendi kabisa kwahiyo naomba msaada wenu juu ya hatua ya kuchukua katika haya

(A)
Je, kuna haja ya kumjulisha mwenye jina?(Mzazi)
Je, anaweza kukubali?
Je, akikataa naweza kulazimisha?
Je, nikilazimisha naweza kupatwa na laana?

(B)
Naomba kuelekezwa hatua za kisheria kwa ujumla, gharama na muda wa kutimia kwa jambo

Nawasilisha.
Mkuu ni rahisi tu
Nenda mahakamani kaape kisha chukua hicho kiapo peleka pale wizara ya ardhi kaombe Deed Poll ya kukana jina hilo usilotaka. Kisha utajaza majina unayotaka uitwe
1. Nenda na copy ya kitambulisho cha Taifa au passport vema ukicertify, passport size
2. Gharama nakumbuka kwa mwaka jana ilikuwa around 30k (nisahihishwe) kwa hk wizara ya ardhi

Ndani ya siku 7 utapata majibu
 
Mkuu ni rahisi tu
Nenda mahakamani kaape kisha chukua hicho kiapo peleka pale wizara ya ardhi kaombe Deed Poll ya kukana jina hilo usilotaka. Kisha utajaza majina unayotaka uitwe
1. Nenda na copy ya kitambulisho cha Taifa au passport vema ukicertify, passport size
2. Gharama nakumbuka kwa mwaka jana ilikuwa around 30k (nisahihishwe) kwa hk wizara ya ardhi

Ndani ya siku 7 utapata majibu
Shukrani, wizara ya ardhi inahusikaje hapo au ni iwapo nina ardhi?
 
Shukrani, wizara ya ardhi inahusikaje hapo au ni iwapo nina ardhi?
Kuwa makini, kuna makanjanja wa kutosha humu!

Fika kwa wakili atakuandalia nyaraka zote muhimu ikiwemo viapo nk, kisha zitasajiliwa kwenye mamlaka husika.

Baada ya hapo, nyaraka zako binafsi kama hati za umiliki wa mali, hisa, vyeti mbalimbali nk nazo zinaweza kufanyiwa mabadiliko.

Utapaswa kufika kwenye mamlaka mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha hilo (banks, kazini, vikundi mbalimbali vya ushirika, kanisani, taasisi za elimu nk)

Fika kwa wakili akusaidie!
 
Kuwa makini, kuna makanjanja wa kutosha humu!

Fika kwa wakili atakuandalia nyaraka zote muhimu ikiwemo viapo nk, kisha zitasajiliwa kwenye mamlaka husika.

Baada ya hapo, nyaraka zako binafsi kama hati za umiliki wa mali, hisa, vyeti mbalimbali nk nazo zinaweza kufanyiwa mabadiliko.

Utapaswa kufika kwenye mamlaka mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha hilo (banks, kazini, vikundi mbalimbali vya ushirika, kanisani, taasisi za elimu nk)

Fika kwa wakili akusaidie!
Shukrani kwa ushauri wako mzuri bosi
 
Kuwa makini, kuna makanjanja wa kutosha humu!

Fika kwa wakili atakuandalia nyaraka zote muhimu ikiwemo viapo nk, kisha zitasajiliwa kwenye mamlaka husika.

Baada ya hapo, nyaraka zako binafsi kama hati za umiliki wa mali, hisa, vyeti mbalimbali nk nazo zinaweza kufanyiwa mabadiliko.

Utapaswa kufika kwenye mamlaka mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha hilo (banks, kazini, vikundi mbalimbali vya ushirika, kanisani, taasisi za elimu nk)

Fika kwa wakili akusaidie!
Kwa nn aingie gharama kubwa ilhali hili jambo limenyooka kabisa. Haya masuala twafanya mara kwa mara hakuna ukanjanja wala nini.

Afanye research ndogo tu hk kwa wakili ataambiwa gharama zake ni 250k wakati huko nimempa njia nyepesi kabisa haitazidi 50k. Naamini atarudi hapa na kushukuru kwa hii njia

Huko benk na mamlaka nyingine atakuwa anatoa taarifa tu juu ya kubadilisha jina akiambatanisha na Deep Poll. Hana haja ya kwenda kwanza hk ktk mamlaka hz
 
Back
Top Bottom