Msaada: Faida za kusoma masters Ulaya/USA

Msaada: Faida za kusoma masters Ulaya/USA

Mkuu kusoma nje kuna faida yake
Achana na kubeba boksi
labda nitoe mfanokama watu wanaosoma IT
NA MAMBO MENGINE NI RAHISI SAANA PRACTICAL kuliko kwetu huko ambako unasoma IT hata PC ya mwalimu kufundishia hakuna
Japo kuwakuna disadvantage zake.
lakini faida ni nyingi kuliko hasara
Angalizo kama wataka kumleta Binti yako asome undergraduate nakushauri Fikilia mara mbili mbili
ila kama anakuja Kupiga masterz basi faster mwache aje apige msuli
 
Dont think twice....pack ur bags kwea pipa arifu......
 
Ee bana elimu ya huku mazee imetulia, sababu ni kama zifuatavyo:

1. Walimu wako makini na kazi yao na wamejikita katika kufundisha: bongo mwalimu mara afuge kuku, nguruwe, mara jioni aende kusimamia baa yake, research ndio hawafanyi kabisaaaa!

2. Vitabu mzee hapa tunatumia latest versions na upatikanaji ni rahisi sana tofauti na nyumbani. Mie nimepiga degree moja bongo lakini nilipokuja huku kwa masomo zaidi, tofauti haipimiki mazee!

3. Technolojia ndugu huku ndiko ilikotokea!

4. Pia unaweza kuongeza "fluency" ya ngeli (ingawa siyo guarantee, kuna wengi tu wamerudi na vingereza vyao vilevileeee)

5. Kama wanavyosema "mjini shule" basi kaka "ulaya/USA nako shule" mfumo tu wa maisha unaweza ukabadilisha sana mtazamo wako.
 
Ee bana elimu ya huku mazee imetulia, sababu ni kama zifuatavyo:1. Walimu wako makini na kazi yao na wamejikita katika kufundisha: bongo mwalimu mara afuge kuku, nguruwe, mara jioni aende kusimamia baa yake, research ndio hawafanyi kabisaaaa!2. Vitabu mzee hapa tunatumia latest versions na upatikanaji ni rahisi sana tofauti na nyumbani. Mie nimepiga degree moja bongo lakini nilipokuja huku kwa masomo zaidi, tofauti haipimiki mazee!3. Technolojia ndugu huku ndiko ilikotokea!4. Pia unaweza kuongeza "fluency" ya ngeli (ingawa siyo guarantee, kuna wengi tu wamerudi na vingereza vyao vilevileeee)5. Kama wanavyosema "mjini shule" basi kaka "ulaya/USA nako shule" mfumo tu wa maisha unaweza ukabadilisha sana mtazamo wako.
nilikuwa nawasubiri watu kama nyie, kuna scholarship ya masters in logistics huko Ulaya, qualification ninazo japo masharti yao ni kurudi kufundisha hapa bongo
 
Kama utasoma Masters huko Majuu utapata faida nyingi tu baadhi ni: -
(1) Muda wa masomo ni mwaka mmoja ukilinganisha na mwaka 1 na nusu hadi miaka 2 hapa kwetu
(2) Shule ya kule ni nyanya, huhitaji kukomaa kama hapa kwetu. Kule Prof anapenda ufaulu wakati hapa kwetu ukifeli Prof anachekelea
(3) Kiingereza chako kitaimarika na kuacha na the the ..., I mean etc
(4) Kupiga deki vyooni na kubeba mabox ya wazungu hakuepukiki kwa vile utakuwa huna fedha za kutosha kuishi maisha yale
(5) Ukirudi Bongo utajisikia Mjanja zaidi ya wale uliowaacha nao wataamini hivyi hivyo
(6) Faida nyingine ni kama zilivyoelezwa hapo juu japo ni kwa utani.

Tafadhali zingatia na kama unayo mawe angalau ya kukufikisha huyo songa mbele, mambo si mabaya sana.
 
1. mkuu ni kwamba unaposoma nje unajifunza current and future issues regarding ur study with real world examples (eg. how microsoft operates/succeeds/their supply chain etc) tofauti na tz ambapo unasoma vitabu/vitu vya 1980's

2.malecturer wengi wameshafanya sana kazi kabla ya kuanza kufundisha (wenzetu kufundisha ni hobbie) eg unaweza ukakuta lecturer alikuwa/ni marketing manager for 20 yrs imagine na wewe unasoma marketing tofauti na tz ambapo unafundishwa na lecturer ambaye hajawahi kufanya kazi nyingine zaidi ya kufundisha

3. unasoma biashara tz wakati tz yenyewe ipo mkiani kidunia ktk maswala ya biashara
 
Inaonekana memba wegi wa JF wanapenda mizaha mwenzetu kauliza swali la msingi sana.Binafsi nijuavyo faida za kusoma ulaya hasa katika shahada za juu ni kule kupata fursa za kulinganisha maarifa na mazingira katika fani fulani mf kama ni economics utaweza kulinganisha sera,mitazamo,mbinu na jinsi wengine wanavyoshughulikia masuala ya uchumi(na fani yeyote nyingine).lakini pia utaweza kubainu nyongeza au mapungufu yaliyopo katika mtaala wa fani hiyo(kwa kuangalia course description ya hukuo ulaya na ya nyumbani )je zinakidhi matarajio au malengo yako ya kitaaluma? mambo mengine ni mazingira ya kujifunzia hususani vifaa,hapa nyumbani asilimia kuwa ya fani zetu hata zile zenye kuhitaji vifaa vya vitendo hufundishwa kwa nadharia lakini unaweza kukuta huko nje wamewekeza sana katika vifaa hii inasaidia kuyaona mazingira halisi ya fani husika.
 
Faida yake ni kwamba utasoma kwa kutumia teknolojia na mazingira rafiki basi, hamna zaidi.
 
Ni wazi pia kuwa utaongeza ufahamu wa mazingira nje ya bongo.
 
Mkuu nje kama Ulaya na Marekani,ile kuishi tu maisha yale,na kukutana na watu wa aina mbalimbali,bila hata kwenda shule,basi ni degree tosha kabisaa.Naamini mtu aliyekwenda Marekani kwa mfano na form 4/6 yake,hata kama hajajiendeleza,lakini kule kuishi kwake tu pale kwa mfano kwa miaka 3,anaweza akawa na ufahamu mkubwa wa mambo mbalimbali ya maisha na maendeleo kuliko muhitimu wa shahada ya UDOM.
Hili suala siyo la mjadala mkuu,nenda kasome na hutajuta.Utajifunza mengi sana sana ya kukujenga kimaisha na kielimu nje ya elimu ya darasani utakayoipata.
Hakuna elimu nzuri kama ya UZOEFU(exposure).
 
hakuna faida yeyote huko maana elimu ni ileile na watu wanarudi na ujuzi uleule ambao hakuna tofauti na hapa kwetu na ukirudi mishahara yote ni sawa. sana sana utakuwa umepanda ndege, utarudi umenunua simu, kamera, laptop kwa bei nafuu.

mi nafikiri kama hawajui wangenyamaza tu wasubirie wanaojua waseme. Wanajiaibisha. Lol!
 
yutong;hakuna faida yeyote huko maana elimu ni ileile na watu wanarudi na ujuzi uleule ambao hakuna tofauti na hapa kwetu na ukirudi mishahara yote ni sawa. sana sana utakuwa umepanda ndege, utarudi umenunua simu, kamera, laptop kwa bei nafuu.

Kama elimu ni ileile kwa nini kukicha watu wanasaka scholarship kwenda huko US au Ulaya? Au wanatafuta sifa? Kama elimu ya ulimwengu wa kwanza na wa tatu ni sawa Kwa nini wasisome hapa UDSM, Mzumbe, SUA au IFM na wanaamua kutoa pesa nyingi kwenda huko? Kwa hiyo ubora wa Elimu ya Harvard, Cambridge, OXford, MIT, au Princenton ni sawa na ya UDSM, Mzumbe au IFM?

Yutong, naona hayo ni maneno ya mkosaji tu.








 
hakuna faida yeyote huko maana elimu ni ileile na watu wanarudi na ujuzi uleule ambao hakuna tofauti na hapa kwetu na ukirudi mishahara yote ni sawa. sana sana utakuwa umepanda ndege, utarudi umenunua simu, kamera, laptop kwa bei nafuu.

Hutasoma kwa madesa wala kukariri
Critical thinking capacity yako itaimarishwa.
Hutasoma huku umekaa chini ya sakafu ama ukiwa unasikiliza lecture uliwa nje ya darasa
Hakuna kunji
Utapata exposure ya vitu vingi sana na itakuongezea confidence
Walimu wenye akili za mgando hakuna
Utaweza ku-polish your language and communication skills
You'll get the opportunity to see the world na mengine mengi
 
ujiko na rahisi kupata kazi bongo, kama utakuwa unmwaga slang
 
Asanteni kwa kusaidia nadhani ni kwamba ilibidi kuchambua majibu kama walivyosema hapo exposure,money making,more knowledge in terms of quality education, wide network na reputation hasa kwa sie waafrika tunaoamini kuwa kizuri ni cha mzungu peke yake. Nadhani haya mambo yanajidhihirisha hata kwenye ajira zetu kwani malipo pia yanatofautiana kwa mtindo huo. Naomba hoja hii ipokelewe otherwise kama mtu anataka ufafanuzi aseme tena.
 
nazani oportunities bt siku hizi wazungu nao wamekua bahiri,pili;i exposure,maana ushindwe wewe tu ila vitendea kazi vipo,na may be it depend unajisomesha au unasomeshwa,km unajisomesha ujipange kweli kweli,km unasomeshwa welldone u need to go,tatu nazani kuna kozi nyingi (varieties) hata ambazo bongo hazijaanzishwa
 
Wewe unaongea vitu kwa kujifurahisha wewe kama ungekanyaga angalau malaysia ukiachilia mbali uk au usa usingeongea vitu vya ajabu km hiyo mimi mwenyewe niikuwa na mawazo km yako lakini baada ya kukanyaga uk kwa mwaka mmoja tu kwa advance diploma ya masoma ya ICT niliona kweli TZ nilikuwa nacheza tu kwani walimu wote walikuwa wanahakikisha wanachokifundisha unakielewa na facilities ni za kueleweka ingawa kufanya kazi za vibarua kuko palepale lakini ukirudi hakuna atakaejua kama ulikuwa unaosha vyombo
hakuna faida yeyote huko maana leule ambao hakuna tofauti na hapa kwetu na ukirudi mishahara yote ni sawa. sana sana utakuwa umepanda ndege, utarudi umenunua simu, kamera, laptop kwa bei nafuu.
 
Wewe unaongea vitu kwa kujifurahisha wewe kama ungekanyaga angalau malaysia ukiachilia mbali uk au usa usingeongea vitu vya ajabu km hiyo mimi mwenyewe niikuwa na mawazo km yako lakini baada ya kukanyaga uk kwa mwaka mmoja tu kwa advance diploma ya masoma ya ICT niliona kweli TZ nilikuwa nacheza tu kwani walimu wote walikuwa wanahakikisha wanachokifundisha unakielewa na facilities ni za kueleweka ingawa kufanya kazi za vibarua kuko palepale lakini ukirudi hakuna atakaejua kama ulikuwa unaosha vyombo
Yan advance diploma ndo ukasome kote huko,c bora ungesoma 2 hapa hapa bongo?
 
hilo ndo jibu, mtu anajua Tanzania ni elimu duni na haina soko kubwa halaf anauliza swali kama hilo, the issue here is that he is informing us of his intention/ plan to go there!!!😛hoto::der::der:bye bye! nenda Denmark!
Utapata nafasi ya kuosha vyoo vya wazungu
 
Back
Top Bottom