Tanzania tumelogwa na nani?

Tanzania tumelogwa na nani?

farfat

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2021
Posts
377
Reaction score
687
Kwanza kabisa, sitaki kuanza na wema, sababu huu wema tulionao ndio umepelekea mambo yanayoendelea sasa nchini.

Nimejaribu kuwaza kwa kina na kutazama vipaumbele tulivyo navyo kama nchi, nimeishia kulia na kujawa hasira. Hivi aliye toa wazo la kuandaa mashindano ya AFCON hapa Tanzania alikuwa nani, na aliwaza nini hasa?

Isitoshe, sio kama sisi pekee tutakuwa wenyeji. La hasha, hapa kuna wenyeji watatu. Sasa tuangalie faida sisi kama taifa tutapata vipi maana ya kuwa wenyeji ikiwa wageni watalazimika kwenda nchi zote tatu zilizo-host mashindano haya? Kulikuwa na haja gani hasa ya kuandaa?

Tunapita vipi nguvu ya kuandaa mambo ya starehe wakati hata huduma bora za maji zimetushinda? Yaani hatuna uhakika na huduma za maji, hatuna miundombinu bora ya barabara, sekta ya elimu haina msaada kwa taifa zaidi ya kusoma na kuandika. Taaluma imekuwa mzigo kwetu.

Imagine mpaka leo nchi yenye watu milioni 70 inaleta wakandarasi wa barabara kutoka nje. Huduma za usafiri jijini ni tatizo. Au ndio mnataka timu zikiwa zinaenda viwanjani mfunge barabara ili watu wenu wasifanye kazi kupisha misafara ya AFCON?

Anyway, viongozi, matako yenu.
 
Sasa hivi kuna upigaji mkubwa sana unaendelea kwenye ujenzi wa viwanja, lakini mwisho wa siku hiyo economic return tunayoitegemea itakuwa ndogo sana.
 
Sasa hivi kuna upigaji mkubwa sana unaendelea kwenye ujenzi wa viwanja, lakini mwisho wa siku hiyo economic return tunayoitegemea itakuwa ndogo sana.
Vipi kama pesa inayotengeneza viwanja iyo zingeelekezwa kwenye wizara ya afya. Tungesaidia watu wangapi. Fikilia watu wanaokwama hospital kwa kukosa kulipia huduma ambazo zimefanywa kuwa ngumu kwa maslahi ya watu.. au vipi kama tungeelekeza pesa izo kwenye wizara ya maji tungesaidia watanzania wangapi
 
Ngoja tusubiri itakuaje.
Inawezekana vipi uka host mashindano makubwa kiasi Cha AFCON wakati usafiri tu wa mwendo Kasi haujasimama ipasavyo.. je unataka wageni wakija wapande bodaboda🥺
 
Vipi kama pesa inayotengeneza viwanja iyo zingeelekezwa kwenye wizara ya afya. Tungesaidia watu wangapi. Fikilia watu wanaokwama hospital kwa kukosa kulipia huduma ambazo zimefanywa kuwa ngumu kwa maslahi ya watu.. au vipi kama tungeelekeza pesa izo kwenye wizara ya maji tungesaidia watanzania wangapi
Uko sahihi, unajua ujenzi wa uwanja tu wa Arusha pekee unagharimu zaidi ya shilingi bilioni 338 Achilia mbali ule wa Dodoma na ukarabati wa Zanzibar. Hizo fedha zingeelekezwa Wizara ya Afya tungeokoa maisha ya maelfu ya watanzania maskini wanaokufa kila siku kwa kukosa basic medical care kisa tu hawana hela ya kulipia huduma.

Ni vile tunaongozwa na vilaza!
 
Itakuja kutokea aibu nchi hii hutaamini.
Kwa sababu sisi watu weusi ni wajinga sana.. kulikuwa na haja gani ya maviwanja.. habari za viwanja achia Simba na yanga.. uwanja wa uhuru stadium,Benjamin stadium, CCM kirumba,jamhuri dodoma, lake tanganyika kigoma sijui kaitaba vyote vingetosha so how come wanatuletea usengerema alafu wanataka vijana wasitumike na siasa za kimagharibi
 
Yani mpaka wameandaa Ina maana wamejipanga.

Hakuna mgeni atapelekwa kwenye shida za maji na miundombinu.
Itakuwa ni kucheza mpira.
Kisha Mbuga za wanyama.
Na kurudi kwao.


Ukisubiri Kila kikae sawa.
Hutaweza kufanya kitu chochote.
 
Mchawi wa Tanzani ni unafiki na u snitch
 
Sijasoma, wenzio wakiwa wanasoma hati na kaida za uandishi wewe ndio ulikuwa unammulika mwalimu na kioo ?
 
Yani mpaka wameandaa Ina maana wamejipanga.

Hakuna mgeni atapelekwa kwenye shida za maji na miundombinu.
Itakuwa ni kucheza mpira.
Kisha Mbuga za wanyama.
Na kurudi kwao.


Ukisubiri Kila kikae sawa.
Hutaweza kufanya kitu chochote.
Tunajifunza kupitia watu waliofanikiwa ama kufeli.. sisi tumejifunza Nini kwa watu walioandaa kombe la Dunia. Unaona USA na Canada wamevunja viwanja vilivyotumika. Utaona hata kimtazamo na kifikra hatupo sawa nayo.. mambo ya maviwanja waachie Simba na yanga, namungo na mtibwa vilivyopo chini ya selikali vinatosha tuangalie mambo ya msingi na sio kupoteza muda na pesa
 
Yani mpaka wameandaa Ina maana wamejipanga.

Hakuna mgeni atapelekwa kwenye shida za maji na miundombinu.
Itakuwa ni kucheza mpira.
Kisha Mbuga za wanyama.
Na kurudi kwao.


Ukisubiri Kila kikae sawa.
Hutaweza kufanya kitu chochote.
Nnchi bado Ina changamoto muhimu zaidi kama,
Upatikanaji wa Maji
Ubora wa miundo mbinu
Elimu
Huduma za afya
Ajira
Na utegemezi wa wakandarasi tunaolazimika kuwalipa pesa nyingi kwanini tusiweke vipaumbele hata ktk elimu za ufundi.. je kipaumbele chetu ni nini labda wewe unaelewa
 
Nnchi bado Ina changamoto muhimu zaidi kama,
Upatikanaji wa Maji
Ubora wa miundo mbinu
Elimu
Huduma za afya
Ajira
Na utegemezi wa wakandarasi tunaolazimika kuwalipa pesa nyingi kwanini tusiweke vipaumbele hata ktk elimu za ufundi.. je kipaumbele chetu ni nini labda wewe unaelewa
Mbona Kila Kiko fresh huku kwetu.
Sijui huko kwenu
 
Hii
Kwanza kabisa sitaki kuanza na wema sababu huu wema tulionao ndio umepelekea mambo yanayoendelea sasa nnchini.. nimejaribu kuwaza kwa kina na kutazama vipaumbele tulivyo navyo kama nnchi nimeishia kulia na kujawa hasira.. hivi alietoa wazi la kuandaa mashindano ya Africa (AFCON) hapa Tanzania ni alikuwa nani na aliwaza Nini hasa. Isitoshe sio kama sisi pekee tutakuwa wenyeji. La hasha hapa Kuna wenyeji 3.. sasa tuangalie faida sisi kama taifa tutapata vipi maana ya kuwa wenyeji ikiwa wageni watalazimika kwenda nnchi 3 zilizo host mashindano haya.. kulikuwa na haja gani hasa ya kuandaa... Tunapita vipi nguvu ya kuandaa mambo ya starehe kwenye ambayo hata huduma Bora maji zimetushinda.. Yani hatuna uhakika na huduma za maji.. hatuna miundo mbinu Bora ya balabala, sekta ya elimu Haina msaada kwa taifa zaidi ya kusoma na kuandika Yani taaluma imekuwa mzigo kwetu.. imagine mpaka Leo nnchi yenye watu million 70 inaleta wakandarasi wa balabala kutoka nnje. Huduma za usafiri jijini ni tatizo au ndio mnataka timu zikiwa zinaenda viwanjani mfunge balabala watu wenu wasifanye kazi kupisha misafara ya AFCON.. anyway.. viongozi matako yenu
Hii nchi ni ya ajabu sana, mambo ya afcon wameyavalia njuga wakati mashuleni miaka 60 ya uhuru bado watoto wanakaa chini.
 
Back
Top Bottom