Msaada: Exporting unga wa sembe to UK

MURUSI, bagamoyo, Bavaria, @sulsmael, chikira mtabari, misasa and the rest hebu tusaidiane kwa hili nini haswa ni vikwazo watanzania tunashindwa kupeleka bidhaa zetu nje ya nchi, je ni serikali na mamlaka zake au ni sisi wenyewe watanzania......
Mkuu,
Kuna mambo mengi ya kuendelea kujiuliza na kufanya utafiti wa kutosha.
Mfano: Kuna kampuni/jamaa wanakuja nchini kutokea nje ya nchi na sanasana ni Wahindi, wanaweka kambi humu nchini na hasa mashambani huko, wananunua mazao kama Ufuta, Choroko, Mbaazi, Dengu na mazao mengine ya jamii ya Mikundekunde, wanapopeleka huwa hatupajui na hakuna anayejishughulisha kujua huwa wanayapeleka wapi, kwa kifupi hapa namaanisha MASOKO.
Kama bidhaa hizi zipo hapa nchini kwetu kwanini sisi tunaishia tu kuwauzia hawa wanaotulangua, ina maana sisi hatuwezi kupeleka huko wanapopeleka wao.
Hebu tufunguke vijana. Na kwa sasa nina imani na serikali tulonayo.
 
Mimi sidhani kama kuna market ya unga wa sembe England,wazungu hawatumii hii kitu- South Africa wanapeleka sembe uk,trade name Iwisa,Azam nae anapeleka lakini naona ni quantity ndogo sana
 
Mimi sidhani kama kuna market ya unga wa sembe England,wazungu hawatumii hii kitu- South Africa wanapeleka sembe uk,trade name Iwisa,Azam nae anapeleka lakini naona ni quantity ndogo sana
Lakini mleta mada kasema kuna kaka yake huko ndo aliyemwambia kuwa demand ni kubwa mahali alipo.
 
Mkuu s

Soko kubwa la hao wahindi wanaonunua nafaka sana sana ni Uk Mkuu.
 
Mkuu s

Soko kubwa la hao wahindi wanaonunua nafaka sana sana ni Uk Mkuu.
 
mwambie aende supermarket za ASDA,umejaa tele,unless hiyo sehemu hamna waafrika
Jackline unatuchanganya sasa, mwanzoni umesema Wazungu hawatumii hiyo kitu na ukadai hata Azam na kutoka South Africa wanapeleka kwa kiwango kidogo sana, sasa hivi unasema Sembe imejaa supermarkets, so which is which maana kama Sembe ni nyingi kwenye hizo supermarkets unazosema maana yake uhitaji ni mkubwa. It's just a simple science.
 
Funguka Kamanda, kama una details ndo tunazihitaji hapa. Kwani sisi hatuwezi kukomaa kuzifukuzia hizo fursa huko UK!!?
Tiririka hapa mkuu.
Sina details nyingi. Ila kama unaweza kupata watu wanaofanyakazi kwenye kampuni za ukaguzi wa mizigo bandarini, hawa watakuwa na info za kutosha. Sisi kufanya biashara hii inawezekana kabisa ukishapata soko na mtaji.
 
Kwa kifupi,supermarket zote za ASDA,ambazo ziko kwenye maeneo yenye Waafrika na Wahindi zina uza Asda branded maize flour exception ni Asda ambazo ziko maeneo ya wazawa.mimi ni msukuma,kwangu sembe ni petrol,kila nikiingia UK hiyo ni top priority
 
Bavaria nikushukuru tu kwa kweli kwa miongozo, hapo nimekusoma, vipi juu ya mode of transport that reliabe, safet from pirates , easy to access and yenye bima kwa kusafirisha mzigo mkubwa.....

Hakuna zaidi ya meli. Ukitaka kutumia ndege ni gharama kidogo labda itokee unatuma perishable products.

Kumbuka ukishafikisha mzigo bandarini na umeshakabidhi kwenye meli huo mzigo sio wako tena unless itokee issue ya kuwa chini ya specifications au kiwango.

Ila kama mzigo umeibiwa au kupotea mwenye meli ambaye ana bima ataulipa huo mzigo.
 
MURUSI, bagamoyo, Bavaria, @sulsmael, chikira mtabari, misasa and the rest hebu tusaidiane kwa hili nini haswa ni vikwazo watanzania tunashindwa kupeleka bidhaa zetu nje ya nchi, je ni serikali na mamlaka zake au ni sisi wenyewe watanzania......

Kuna wakati serikali inazuia kusafirisha nje bidhaa muhimu hasa mahindi endapo itajihisi chakula hakitatosha kwa mwaka huo.

Kingine ni sisi watanzania tunakosa exposure kabisa. Hatuna ile hali ya kutoka nje ya comfort zone yetu na kufanya makubwa.
 
Mawazo na malengo mazuri. Zingatia yafuatayo kabla ya kufikiria mtaji.

Umoja wa Ulaya unafanya kazi kwa viwango na afya ya jamii kwao ni sehemu ya kipaumbele hivyo kwanza soma sheria ya uingizaji vyakula katika nchi hizi.

Ukijiridhisha na uwezo wako wa kutimiza vigezo hivyo nadhani mengine hayo yatakuwa historia. By the way, unga juzi kati nilinunua kilo moja 6€ sawa na 14,000/= kama sijakosea alafu hauna ladha kama unga wetu.

Inawezekana ukiamua
 
Kweli mkuu nakubaliana na wewe
 



Mkuu Toxic9,

Kampuni yetu ya Premier Freights inaweza kushughulikia swala lako ila unayotakiwa kujua kwamba unga wa Azam mara nyingi hawana guarantee ya mwaka mmoja na kama wakikwambia wanayo basi waambie wakupe kwa maandishi wasikwambie kwa mdomo ili chochote kitakachotokea basi unaweza kwenda kudai compensation, kama utasafirisha kwa meli basi itachukua takriban kama mwezi kuuweka store na kutafuta soko mwezi mwengine mmoja unless bro wako tayari ana kampuni ameshaongea nao tayari ila kama utaamua kuusafirisha kwa ndege basi inakua ni kama wiki ama wiki mbili baada ya booking.

Na kama utakua tayari basi inakubidi utafuta agent wa meli ama wa ndege afanye booking huko halafu sisi hapa tunafanya clearing na delivery kama ukipenda. lakini please make sure kila detail iko sawa (correct) ili kuondosha confusion katika clearing
kuna paper works za kusafirisha nafaka hizo Azam export wataku guide namna ya kusafirisha na packaging na pamoja na meli huwa wanalishuhulika wao then wanakupa hesabu yako tu.
 

Attachments

  • Screenshot_2016-06-26-17-55-32.png
    32.1 KB · Views: 72
  • Screenshot_2016-06-26-17-56-36.png
    34.1 KB · Views: 75
Okey kwanza ninawashukuru wachangiaji wote waliopita kwenye uzi na kutoa mawazo yao nilikuwa offline kidogo, ngoja nianze kujibu, nitaanziana mkuu hapa...

Premierfreights team nashukuru kwa kunifanya kuona zoezi langu litakuwa rahisi hasa kwenye swala la usafirishaji maana katika vitu vilinifanya kuwaza ni namna ya kusafirisha mzigo,

Kabla ya yote ningependa kujuwa PREMIERFREIGHT ni wakina nani,mnapatikanika wapi hapa Tanzania, how reliabe are you? mnautaratibu gani mtu akitaka kusafirisha mizigo yake eg nafaka hususani nje ya nchi, na je mnatoa bima ama warrant kwa mzigo naosafirisha, na je gharama zenu zikoje, hebu tuanzie hapo,


Kwa upande wangu mzigo utatoka hapa utapokelewa na ndugu yangu destination ni UK_Middlesbrough...
 
You will need a lot of money that's it
Biashara gani hiyo mtu atafanya bila feasibility study ili kupata kadirio la mtaji, cost of operations etc, Watanzania kwa kurudishana nyuma, naamini ni mawazo yako unataka yakae kwenye kichwa changu pia kitu ambacho ni never, shule pia zitusaidie sio kwenda kujaza darasa bure
 
Reactions: amu
Mkuu, hii ni discouraging contribution.
A lot of money that you are talking about is how much??!!
Ahsante mkuu kwa kuliona hilo, huyu jamaa anasema nitahitaji hela nyingi bila kuweka figure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…