Msaada Chumvi kwenye Engine ya Pikipiki

mzizi1

JF-Expert Member
Oct 9, 2017
255
692
Wasalaam ndugu zangu.

Aiseh haya maisha akili ni kitu ambacho hupaswi kukosa kabisa.

Kifupi niko na pikipiki tatu zote za mkataba. Kuna pikipiki moja ina mwezi wa tatu sasa, lakini imekumbwa na hii shida.

Huyu nilomkabidhi kuendesha alikua mzito kurejesha pesa na sababu kuu aliugua kwa muda karibu siku 20, lakini pikipiki alidai kuwa aliipark lakini ukweli ni kua ilikua inapiga kazi, namimi sikutaka kuharibu mipango yake ukiangalia alikua mrejeshaji mzuri wa pesa.

Majuzi akaomba kusitisha mkataba maana deni lilikua kubwa. Tuliandikishana marejesho ya deni. Siku ya juzi nilipokua nafanya service ili nimakabidhi boda mwingine ndo nikagundua kuwa engine imewekewa chumvi. Taratibu za kisheria zikachukua mkondo wake na jamaa yuko ndani (maisha yake ni magumu, sioni uwezekano wa kulipwa gharama za matengenezo bali naiona jela mbele yake tu endapo nitaamua kusimamia kidete).

NAOMBA MWONGOZO JINSI NINAVYOWEZA KUTOA HILI TATIZO NA PIKIPIKI IENDELEE KUFANYA KAZI KAMA KAWAIDA.

NB.
Wale wataosema ni biashara kichaa, niwambie tu hii biashara kwangu mimi inalipa na imenitengenezea faida.

Pikipiki inatembea vyema tu, shida ni hili tatizo.

Nawasilisha
 
naona faida ya biashara yako ni kuweka watu ndani na kutiliwa chumvi injini imekua kitimoto skuhzi
alaf umepata dereva muoga huna ushahidi kwamba yy ndiye aliyeweka chumvi kwahyo kumfunga huwez labda uhonge wakatishe haki yake ila mabos wa pikipiki akili zao kama za bodaboda tu
 
tatzo nyie watu mnaotoa pkpk za mikataba mna roho za ajabu sana hamtak kumskilza mtu wala kujal changamoto anaxoptia nyie mnachotaka n hela tu
Kweli we ni mbeba lawama, hivi kama ingekua mkataba unamfunga, ningeweza vumilia siku 20 mtu akiwa anaumwa na hakuna taarifa za msingi za kuumwa kwake?
 
naona faida ya biashara yako ni kuweka watu ndani na kutiliwa chumvi injini imekuabkitimoto skuhzi
alaf umepata dereva muoga huna ushahidi kwamba yy ndiye aliyeweka chumvi kwahyo kumfunga huwez labda uhonge wakatishe haki yake ila mabos wa pikipiki akili zao kama za bodaboda tu
Uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana ndugu.

Pikipiki alikabidhiwa kwa maandishi na yeye ndo mlinzi wa hiyo mali, imerudishwa na kabla ya makabidhiano ikakaguliwa garage unakuta chumvi, then wataka kusema niliiweka mwenyewe?

Kumfunga ndani sio solution maana hii ni biashara ya ziada tu kwangu, matengenezo yake hayagharimu pesa ndefu ni usumbufu tu alonipatia na ukiangalia pikipiki ni mpya yenye kila kitu.

Sifanyi kumkomoa, ila nataka tu kujua sababu ya msingi ya yeye kufanya vile ni nini hasa
 
Changamoto inahusiana vipi na mkataba, ukiruhusu tu hio kitu changamoto mwenzio atakuachia screpa ananunua nyingine
Hili ni tatizo kubwa kabisa Tanzania. Nazungumzia hili neno ''changamoto'' hili.

Utamkopesha mtu fedha na ataahidi kulipa, siku ya kulipa atasingizia changamoto. Utamkabidhi mtu biashara, siku ya mahesabu atasingizia changamoto.

Kitu ambacho hawajui ni kuwa kutekeleza mkataba wowote maana yake ni kukabiliana na changamoto.

Ina maana ukiweka mkataba na mtu umeahidi kukabiliana na changamoto mpaka uzishinde.
 
Uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana ndugu. Pikipiki alikabidhiwa kwa maandishi na yeye ndo mlinzi wa hiyo mali, imerudishwa na kabla ya makabidhiano ikakaguliwa garage unakuta chumvi, then wataka kusema niliiweka mwenyewe???
Wajinga kama hawa wako wengi sana.

Halafu kesho utasikia analia hakuna ajira na maisha ni magumu.

Kuna kitu kimoja kuhusu kufanya biashara Tanzania. Kikwazo kikubwa kabisa cha kufanya biashara Tanzania ni uaminifu wa wafanyakazi.

Ukiweza kukikwepa hiki unakuwa umemaliza asilimia 70 ya vikwazo vya kufanya biashara.
 
Back
Top Bottom