Msaada: Baba amekuwa "mtumwa wa pombe", familia inaangamia

Nyendeke

JF-Expert Member
Jul 21, 2013
1,552
2,844
Poleni na majukumu Wanajanvi..,

Kama kichwa cha habari kinavyo jieleza, kuna dada mmoja ambae ni rafiki yangu alikuja kuniomba ushauri juu ya Mume wake ambae ni Mlevi kupindukia yaani hana muda wa kuijali familia kwa chochote kile kunzia Lishe, Mavazi, Malazi, Ada za Shule za watoto n.k, yeye anachojali ni Pombe tu, dada anazidi kulalamika kua Mumewe ana Mshahara mkubwa kiasi kama ungetumika kwa malengo basi mipango yao yote ingekwenda vizuri ila ndio hivyo tena jamaa kila akitoka kazini anapitia Bar anarudshwa usiku wa manane kwenye Mkokoteni akiwa ameutwika vilivyo na hajitambui.

Dada nae kipato chake ni kidogo kiasi hawezi kumudu majukumu hayo na amejaribu kwenda hata kazini kwake na kukutana na Bosi wa huyo Mume wake ili kama inawezekana apewe asilimia kadhaa katika Mshahara wake ila hajapata ushirikiano wowote kutoka kwa huyo Bosi ambae ni Mkurugenzi katika taasisi kubwa ya Serikali.

Pia familia yake imejaribu kukaa nae vikao takribani vitano kuhusiana na swala hilo Jamaa anakuwa muungwana na kuahidi kuwa ataacha ila akirudi kesho yake ameutwika zaid ya jana.

Hivyo Wandugu nisiwachoshe sana dada anahitaji msaada wenu wakupata dawa ya kumuachisha Pombe ama Ushauri utakaoweza kuinusuru familia yake.

Natanguliza shukrani Wakuu!!
 
Hili tatizo wanalo wengi.
Mie nakushauri kipundapunda.
Kwa mifano nimeyoiona.
-Kwanza wao wangemkodia wahuni siku moja wakampa kichapo cha maana.
Basi kila akirudi angejua kwamba Pombe sio soda.
-Pili,Ulevi na uzinzi ni baba na mama,pangeni na Demu wake siku moja mumpigishe picha za kimeo kisha muone.
Atakuwa hata baa haendi kwa aibu.
-Huyo mama akaombe Talaka mapemaa,maana Ukimwi huoooooo,
Maana hapo hakuna tena tafsiri ya Mume na Mke .
Na walevi kama hao nimewahi kuona wakirudi nyumbani ni matusi mwanzo mwisho,na wengine analazimisha umpe mbunye kwa zogo,hata ukumibini huku watoto wakifuatilia vurugu hilo mpaka wanazoea,wakiisha pevuka na wao wanaingia kwenye chama
 
Poleni na majukumu Wanajanvi..,

Kama kichwa cha habari kinavyo jieleza, kuna dada mmoja ambae ni rafiki yangu alikuja kuniomba ushauri juu ya Mume wake ambae ni Mlevi kupindukia yaani hana muda wa kuijali familia kwa chochote kile kunzia Lishe, Mavazi, Malazi, Ada za Shule za watoo n.k, yeye anachojali ni Pombe tu, dada anazidi kulalamika kua Mumewe ana Mshahara mkubwa kiasi kama ungetumika kwa malengo basi mipango yao yote ingekwenda vizuri ila ndio hivyo tena jamaa kila akitoka kazini anapitia Bar anarudshwa usiku wa manane kwenye Mkokoteni akiwa ameutwika vilivyo na hajitambui.

Dada nae kipato chake ni kidogo kiasi hawezi kumudu majukumu hayo na amejaribu kwenda hata kazini kwake na kukutana na Bosi wa huyo Mume wake ili kama inawezekana apewe asilimia kadhaa katika Mshahara wake ila hajapata ushirikiano wowote kutoka kwa huyo Bosi ambae ni Mkurugenzi katika taasisi kubwa ya Serikali.

Pia familia yake imejaribu kukaa nae vikao takribani vitano kuhusiana na swala hilo Jaa anakuwa muungwana na kuahidi kuwa ameacha ila akirudi kesho yake ameutwika zaid ya jana.

Hivyo Wandugu nisiwachoshe sana dada anahitaji msaada wenu wakupata dawa ya kumuachisha Pombe ama Ushauri utakaoweza kuinusuru familia yake.

Natanguliza shukrani Wakuu!!

mambo ya familia bana huwa yananichanganya kweli,unaweza ukadhani yako makubwa kumbe ya mwenzako ndo makubwa zaidi
 
ukitaka kuacha kwa utashi wako unaweka pombe mdomoni unaenda kuitemea kwenye tundu la choo...mama mmoja alinieleza ila sijawahi kuijaribu.
 
Mfundishe kuvuta ganja ataacha maana stimu ni ileile sema hii haichukui pesa nyingi.Puli unanunua sh 3000 unaivuta karbu wiki lakini pombe kwa siku karibu 20000/= Tena ganja ni dawa ya magonjwa kama15 hivi lakini pombe inaathari ikitumika kwa wingi.Tena ganja akivuta anabaki anajielewa lkn pombe siyo
 
Mmm,hii kali, yaani ya kipepo kabisa!
Mfundishe kuvuta
ganja ataacha maana stimu ni ileile sema hii haichukui pesa nyingi.Puli
unanunua sh 3000 unaivuta karbu wiki lakini pombe kwa siku karibu
20000/= Tena ganja ni dawa ya magonjwa kama15 hivi lakini pombe
inaathari ikitumika kwa wingi.Tena ganja akivuta anabaki anajielewa lkn
pombe siyo
 
Mfundishe kuvuta ganja ataacha maana stimu ni ileile sema hii haichukui pesa nyingi.Puli unanunua sh 3000 unaivuta karbu wiki lakini pombe kwa siku karibu 20000/= Tena ganja ni dawa ya magonjwa kama15 hivi lakini pombe inaathari ikitumika kwa wingi.Tena ganja akivuta anabaki anajielewa lkn pombe siyo

Daaa!! kaka huu ushauri wako sasa Majanga ndo yatazid ila nashkuru kwa kutia neno!
 
Hili tatizo wanalo wengi.
Mie nakushauri kipundapunda.
Kwa mifano nimeyoiona.
-Kwanza wao wangemkodia wahuni siku moja wakampa kichapo cha maana.
Basi kila akirudi angejua kwamba Pombe sio soda.
-Pili,Ulevi na uzinzi ni baba na mama,pangeni na Demu wake siku moja mumpigishe picha za kimeo kisha muone.
Atakuwa hata baa haendi kwa aibu.
-Huyo mama akaombe Talaka mapemaa,maana Ukimwi huoooooo,
Maana hapo hakuna tena tafsiri ya Mume na Mke .
Na walevi kama hao nimewahi kuona wakirudi nyumbani ni matusi mwanzo mwisho,na wengine analazimisha umpe mbunye kwa zogo,hata ukumibini huku watoto wakifuatilia vurugu hilo mpaka wanazoea,wakiisha pevuka na wao wanaingia kwenye chama
Zanzibar Spices, nashkuru sana kwa ushauri wako ndugu!
 
Kuacha pombeinahitaji msaada wa kitaalamu. Muambie mkewe ampeleke counselling.

Ila Ana mshahara mkunwa na anabebwa kwa mkokoteni? Hana gari?
 
Swala la mkokoteni linatia mashaka; hata hivyi jiulizeni ni kwa nini analewa? Huko ndoani kuna mengi!
 
Kuacha pombeinahitaji msaada wa kitaalamu. Muambie mkewe ampeleke counselling.

Ila Ana mshahara mkunwa na anabebwa kwa mkokoteni? Hana gari?
Ok, nashkuru kwa ushauri ndugu, ila kumbuka kwamba kua na gari kunahtaji Mipango na utekelezaji wa hiyo Mipango kama hicho kitu hakipo sahau gari, pia hao wanao mleta na Mkokoteni wanamfkisha akiwa hana hata Mia ss hatujui kama hua wanamchukua akiwa tayari ameshafokolewa Mifukoni ama vp?
 
Back
Top Bottom