Hao wote uliowataja huongea Kiingereza kwa kuwa inawalazimu kuongea Kiingereza na kama wasipoongea basi huwa na mkalimani...
Kumbuka maisha yao ya kisoka wanayaendesha katika nchi itumiayo lugha ya Kiingereza...
Hata huyo Teves wakati akiwa Uingereza alikuwa ni mgumu kujifunza kiingereza ikabidi awe na mkalimani/mkufunzi kumpa msaada...
....lakini huyu Ngassa lugha yake ya kwanza tunaijua ni Kiswahili na yupo katika nchi ambayo lugha ya kwanza ni Kiswahili.
Sasa kwa nini anahangaika kuzungumza lugha ambayo hana ubobezi nayo na kukacha lugha ambayo ndio lugha mama?
Mtu huyu akikosea lazima anyooshewe vidole tu, ujinga ni hali ya kudhani unajua kitu usichokijua....