Mrisho mpoto kamgusa nani hapa?

Mrisho mpoto kamgusa nani hapa?

Huey freeman

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2013
Posts
593
Reaction score
248
Nina wasi wasi nyimbo ya mrisho mpoto ni kuhusu katiba au vyama vya upinzani hasa hasa chadema walio itwa ikulu kutokana na mizozo ya katiba , wote nadhani tunajua jina la mjomba linamaanisha nani. pili nyimbo za mrisho mpoto zimekua zina husu jamii na siasa..mashairi yanasema hivi ;...................................... waite wakalishe chini, waambie wao hawamo japo walikula.....mjomba kuna baadhi michezo ukishindana mwenyewe lazima uwe mshindi lakini kwa mchezo ule uliwahitaji ili kuongeza mashabiki na washangiliaji walio na sauti zisizokauka...walivyoanza mjomba hakuna alie dhani kwanza walifika mapema mmoja wao aka andikisha jina lake kwa niaba ya wengine japo wote wanamajina yao na hayafanani....waliingia wakajipanga kwa sauti zao ya kwanza mpaka ya nne wakaanzisha mapambio watu wakilia wao wanatoa pole tu, na waandishi kwa utashi wao wakaandika msiba umefana kweli hakuna alie lia nje ya key...mjomba ushauri wangu waite....waambie muungwana hanuni kwa mashavu hununa moyoni....wao hawahusiki wala hawamo waje tu kua mashahidi kwakua nao walikuepo na walikula japo kua hawakujua wapi ulimtoa mbuzi yule.. mjomba ushahidi wao utakusaidia katika vitu viwili kuingia katika historia au kushinda kesi....................................bado sijajua kama niko sahihi sana ila nimeamua kuwaletea wana intelijensia wa jamii forum pamoja tutafakari maneno haya na myatolee ufafanuzi sababu mrisho mpoto mwenyewe kamwe hataweza kusema alichokimaanisha kwa sababu za kiusalama that is how he work and how he will always work. ahsanteni.
 
Hivi unadhani hii itadumu? Usanii hasa wa mashairi na uvaaji haviendi mbali. We sngalia tu
 
Usipoifahamu fasihi kwa undani huwezi kuichambua, hivo unapaswa Kuwa na weredi wa kuichambua fasihi hasa za mjomba.Tuambie kwanza umemwelewaje? "AULIZAE ANAJUA KITU".
 
Huwa namkubali sna huyu jamaa.mashairi yake yameenda shule
 
alijiunga na ccm mwaka huu hapa Mbeya japo hakuwep lakn jna lake lilisomwa na nape mapuye

Kama haujui kitu ni vema ukauficha ujinga wako Aliyejiunga na CCM kule Mbeya ni MBOTO (Mchekeshaji na sio MPOTO
**Huyo wa pili kutoka JB ndio MBOTO**


wasanii3.jpg
 
4 what i think jamaa katugeuka sasa ivi yuko upande wa mjomba .....kajiunga ccm kasaliti uanaharakati....pesa sabuni ya roho.
 
nilisoma kwenye gazeti pia mrisho mpoto sema yey hakwenda mbeya.....na rumors za yeye kutaka kugombea ubunge zilikuwepo siku nyingi
 
Usipoifahamu fasihi kwa undani huwezi kuichambua, hivo unapaswa Kuwa na weredi wa kuichambua fasihi hasa za mjomba.Tuambie kwanza umemwelewaje? "AULIZAE ANAJUA KITU".

Nimependa hiyo "AULIZAE ANAJUA KITU" lakini bwana kwenye wengi pana mengi maana "WENGINE HUULIZA ILI WASIKIKE KUWA NAO WAPO"
 
Jamani ameomba kusaidiwa kuchambua hayo mashairi Na sio stories
 
the more your curious the more you know better......nilioandika yote ni mawazo yangu nimeamua kuyatoa ili kama si sahihi nisikae nikiwa nimepotoka ila kama ni sahihi wapowatakao nufaika kupitia mimi
 
Back
Top Bottom