Namshakende
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 771
- 1,903
Siku za hivi karibuni nilishirikisha hapa kisa changu kuhusu changamoto niliyopitia na mwanamke niliyekuwa naye kwenye Mahusiano. https://www.jamiiforums.com/threads/wake-zetu-shida-ni-nini.2333968/Wake . Tumeishi pamoja kwa muda, lakini tabia zake ziliniletea msongo wa mawazo na maumivu ya kihisia. Kwa bahati mbaya, mgogoro wetu ulifikia hatua ya kulumbana na mvutano mkali uliosababisha vurugu ( kichapo).
Baada ya tukio hilo, alikusanya vitu vyake na kurudi kwa mama yake. Jana amenitumia ujumbe akidai hajapata siku zake, na ana hofu kuwa huenda ni mjamzito. Akanitaka nitoe msimamo wangu kuhusu hali hiyo.
Msimamo wangu uko wazi: Kama hiyo mimba ipo, nitaitunza akiwa kwao. Mtoto akizaliwa, nitamchukua na kumpa malezi anayostahili. Lakini kuhusu yeye, safari yake kwenye maisha yangu imeishia hapo.
Sina muda wa kulea mtu mzima asiyeheshimu wala kuelewa thamani ya mwanaume. Mwanaume naye ni binadamu, ana moyo, ana mipaka. Usifikirie kila siku ni wewe tu unapaswa kuhurumiwa. Kuna wakati mtu anafunga kitabu na kusema imetosha!
Nimepigiwa simu na upande wa kwao, lakini nimewaambia kuwa nipo busy na shughuli zangu. Wamsikilize binti yao chochote atakachosema kina ukweli ndani yake. Sina muda wa kujadiliana nao, wajadiliane na mtoto wao.
Mimi najielekeza kwenye maisha yangu mapya.
Baada ya tukio hilo, alikusanya vitu vyake na kurudi kwa mama yake. Jana amenitumia ujumbe akidai hajapata siku zake, na ana hofu kuwa huenda ni mjamzito. Akanitaka nitoe msimamo wangu kuhusu hali hiyo.
Msimamo wangu uko wazi: Kama hiyo mimba ipo, nitaitunza akiwa kwao. Mtoto akizaliwa, nitamchukua na kumpa malezi anayostahili. Lakini kuhusu yeye, safari yake kwenye maisha yangu imeishia hapo.
Sina muda wa kulea mtu mzima asiyeheshimu wala kuelewa thamani ya mwanaume. Mwanaume naye ni binadamu, ana moyo, ana mipaka. Usifikirie kila siku ni wewe tu unapaswa kuhurumiwa. Kuna wakati mtu anafunga kitabu na kusema imetosha!
Nimepigiwa simu na upande wa kwao, lakini nimewaambia kuwa nipo busy na shughuli zangu. Wamsikilize binti yao chochote atakachosema kina ukweli ndani yake. Sina muda wa kujadiliana nao, wajadiliane na mtoto wao.
Mimi najielekeza kwenye maisha yangu mapya.