Mrejesho: Uso kwa uso na shemeji gesti

Mrejesho: Uso kwa uso na shemeji gesti

Joined
Apr 21, 2015
Posts
11
Reaction score
21
Wakuu habari za ujenzi Wa taifa
Mtakumbuka 2 weeks ago nilikuja kuwaomba Ushauri baada ya kugongana uso kwa uso na mke Wa Rafiki yangu guest akitoka room na zee moja hivi huku na mm nikiwa na mchepuko ambao yy hakuuona .
Hivyo akaniomba nimfichie siri bado anaipenda ndoa yake
Rejea post hiyo kwa Maelezo zaidi.

Mazungumzo
Alikua amependekeza tumalizane kiutu uzima ili nikae kimya forever, nilimuita sehemu iliyotulia kwa mazungumzo nikamwambia nimekusamehe sitatembea na wewe na pia sitamwambia mumeo
Kwa sharti la kuacha tabia hiyo
Akakiri na kujutia tabia hiyo na kuahidi kuiacha kabisa
Kwa kweli alifurahi sana akanishukuru kupita Maelezo
Ila bahati mbaya laki tano yake niliila
Pia nimemsisitiza sana mumewe kwa simu afanye awezavyo atafute kazi nyingine hapa dar kama uhamisho ukishindikana

Kuhusu mchepuko wangu
Mlinishauri mm pia niache uzinzi niachane na huo mchepuko wangu Wa arusha ambao nilikua nao siku tumegongana na shemeji guest

Ushauri huu umenishinda kwa kweli maana mchepuko huu ni asset kubwa kwangu
Mke nilie nae ni mama Wa nyumbani ambae nililetewa na wazazi kutoka nyumbani nikawatii wazazi na kumuoa

Mchepuko wangu nilisoma nao chuo na tulikua na ndoto za kuoana bahati mbaya destiny haikutaka hivyo ndipo yakatokea hayo ya baba kuniletea mke
Huu mchepuko unanipenda sana ukasema hata kama mm naoa tuendeleze tu uhusiano wetu, basi nikawa nimeoa,
Bahati mbaya mchepuko ulienda nje ya nchi kwa masters program na ulikaa huko karibu miaka 5 na ndipo ukarudi hapa na kupata kazi arusha

Kiuchumi
Kutokana na gharama za maisha kupanda na familia yangu kupanuka mchepuko huu umekua Msaada mkubwa kwangu
Hii ni kutokana na ukweli kuwa nimekopa mikopo mingi kazini na hivyo napokea mshahara kidogo sana uliobaki
Mchanganuo Wa makato au marejesho upo hivi:-

(1)salaried workers loan=250,000
(2)Credit union loan=
250,000
(3)departmental loan=250
(4)blue financial services=250
Total=1,000,000/=

Salary. Loans. Difference 1,500,000-1,000,000=500,000

Baada ya makato ya mikopo yote inabaki laki tano tu
Kiasi hiki ni kidogo mno kwa mahitaji ya familia yangu ambayo ni extended, wife ni Msukuma hivyo ana ndugu nane ninaokaa nao kwangu maana Wali ukipikwa ni kilo 3 kila siku
Kila ninapofanya jaribio la kuwaondoa ndugu hao wife hununa wiki mbili na hulala na suruali tatu za jeans, na skin tight na kufuli hivyo mm husalim amri na kuacha kuwaondoa
Hivyo Nina majukum mazito sana na mikopo yote imeshafanya maendeleo ikiwemo ujenzi

Kwa hali hiyo mchepuko wangu unakua na maana kubwa sana kusaidia gurudum pale ninapokwama
Mathalan January sikua na ada za watoto hata senti tano na kazini sikopesheki tena
Mchepuko wangu ulinisaidia kulipa ada ya watoto wote watatu ya shs 4,200,000
Kwa ahadi ya kuzirudisha ingawa sijarudisha hadi sasa

Mchepuko huu umeshiriki shughuli nyingi za kifamilia I.e harusi na misiba kwa hali na Mali kwa kuchangia pesa nyingi tu ingawa wife huwa anakutana nao katika hizo shughuli bila kuufahamu

Nikimpigia simu kuna jambo lolote lile yy huondoka fasta arusha na kufika haraka
Dar
Hivyo wakuu Nina upenda sana mchepuko huu ambao umenizalia mtoto mmoja kwa sasa na hauna mpango Wa kuolewa na mtu mwingine

Mlinishauri niuache mchepuko lakin nadhan hiyo ni suicide mission kwangu
Ndo maana huwa naupenda uislam kwenye hili la wake wengi basi tu kwa kuwa mm ni mkristo sina jinsi ngoja niende wote wawili ilimradi tu wife asifaham

Huenda kama kuna mtu ana idea nifanyeje au yeyote mwenye mchepuko Wa namna hii anidaidie alifanyaje akaachana nao
 
Aisee we kiboko ila nakuambia kitu kimoja na ndio discipline ya maisha, hatukuoa ili tupeane matatizo huyo mkeo kama ni kweli amewaleta ndugu zake wote hapo amefanya mistake kubwa sana. Ila swali la kuuliza utaendelea na mchepuko hadi lini? na je umeona mchepuko wako ndio suluhu ya matatizo uliyonayo?
 
Siku wife akijua unapigwa chini aisee...hebu vaa viatu vya wife afu jitathmini


Baada ya hlo NATOA ushauri wa buree maana stori yako inafanana na brother angu
 
duu wanaume kama mabinti.

eti laki tano tuu kweli uko serious mkuu ishi kulingana na mshahara wako hao ndungu walojaa hapo kama kuna msiba wale utachopata wakitaka mboga tatu wanunue looo
lazima wew na mkeo muwe na maamuz ya life style ya maisha yakipato chenu.

unaonaje mkeo naye atafute mchepuko wenye hela maana hela yako haitoshi ?
 
Duuuhh, pole sana. Na jaribu kujiweka kwenye viatu vyako naona una wakati mgumu. Hongera kwa kumsamehe shemeji yako na kukubali kumrindia heshima yake. Kuhusu mkeo jitahidini umtafutie hata biashara au shughuli yoyote ya kufanya. Usifanye hiyo kwa lengo la kutaka kupata pesa au kuongeza kipato, la hasha. Bali Hilo litamfanya atambue ugumu wa kupata hela na ataweza kuwa na nidhamu ya pesa na pengine hao nduguze atakubali waondoke. Kuhusu mchepuko nenda katoe mahali awe mke wako halali. Mimi hua naamini "nothing is good or bad but your thinking make it so". Wakati mwingine yatupasa kuishi ktk uhalisia.
 
Wasukuma ni noma sana
Kuna jamaa jirani yangu kwenye sehemu ya biashara yeye huwa saa 12 ameshafika kufungua wakati maduka yanafunguliwa saa mbili hadi tatu hapa mwanza mjini
Na yeye tukishafunga saa 12 jioni anatafuta vijiwe vya kupoteza muda hadi saa sita usiku nikaja siku moja kumuuliza kwanini hupendi kukaa na family yako?
Akaniambia mke wake ni msukuma ameleta ndugu zake watano wamejazana huko home kwa hiyo hana hamu ya kuwahi na walikuja na mchele gunia wamekaa hadi limeisha na hawaondoki eti wamekuja tu kusalimia
 
najaribu kuunganisha dots na uzi wako wa kwanza kabisa kuhusu uume wako, mkeo ni mfanya kazi wa bank au aliacha? na inaonekana kwao mambo safi dnio maana mamake alikutafutia kazi Tabora...ain't judging lakini ukiwa muongo uwe na kumbukumbu
 
najaribu kuunganisha dots na uzi wako wa kwanza kabisa kuhusu uume wako, mkeo ni mfanya kazi wa bank au aliacha? na inaonekana kwao mambo safi dnio maana mamake alikutafutia kazi Tabora...ain't judging lakini ukiwa muongo uwe na kumbukumbu

Ndo maana nimemwambia pale juu kaweka chumvi nyingi saaana kwenye story yake ya kijiweni
 
Kwa hiyo dume zima unakubali kuwa gigolo to suppliment your living [what a shame]
Mwanamume rijali ni yule ambaye anapambana na mazingira yake na kuyashinda.
Jee kwa mfano naye mkeo [nakuomba radhi kwa hili] akaona maisha yenu ni magumu na kuamua
kuji attach kwa pedeshee utajisikiaje??????
 
najaribu kuunganisha dots na uzi wako wa kwanza kabisa kuhusu uume wako, mkeo ni mfanya kazi wa bank au aliacha? na inaonekana kwao mambo safi dnio maana mamake alikutafutia kazi Tabora...ain't judging lakini ukiwa muongo uwe na kumbukumbu

Wapi Tyta aje atuwekee mtiririko wa post zake za nyuma
 
Last edited by a moderator:
Wasukuma ndo walivyo...Ukimuoa...jiandae....yeye atawaleta ndugu zake hata wale wa mbali sana...hii tabia siyo nzuri sana...kuna wanaume huwa wanakosa la kufanya na kuishia kubeba majukumu yote ya kuwatunza, kuwasomesha, na kuwatafutia kazi....wengine wakifeli unaombwa mtaji...wengine hasa mashemeji wanaweza kuchukua vitu vyako ndani na kwenda kuuza au kama una gari ndo itakuwa kila siku kuliendesha hata kwa fujo na likiharibika wewe ndiye unayetengeneza...."wanaume tumeumbwaaaaaa "mateso"...."matesoo" "Kuhangaika"
 
Back
Top Bottom