Mrejesho safari ya India

MONA WA KYEN

JF-Expert Member
Dec 23, 2016
340
271
Wakuu naamini mnaendelea vema na majukumu
nakumbuka mapema mwezi januari nilileta uzi hapa kuhusu kuhitaji msaada kwani tulikuwa na safari ya kwenda india kumsindikiza ndugu yangu aliekuwa na tatizo la figo.

Ninapenda kuwashukuru wanajamii forum wote kwa michango yenu mizuri ya mawazo yenye tija katika ule uzi. Kiufupi utaratibu wa serikali ni kwamba alitakiwa kwenda mgonjwa na donor halafu baadae ndo angetakiwa kwenda msindikizaji ambaye ndie mimi.

KUELEKEA INDIA
Katika safari hii ya india walienda yule ndugu yangu pamoja na donor wake. siku hiyo waliondoka ghafla kwani walikuwa wamechelewa ndege kutokana na utaratibu wa serikali kuwa mrefu kidogo na wao kuchelewa kuukamilisha mapema pamoja na changamoto mbalimbali za wafanyakazi wa wizara ya afya waliokuwa wanashughulikia hilo swala lao.

Katika hiyo siku waliondoka ghafla na nilitamani sana kuprint angalau comment zenu hapa nimpe aende nazo lakini ilishindikana kwani tangu anatoka wizarani siku hiyo ilikuwa tunakimbizana na wakati kumsaidia asichelewe ndege.

KUWASILI INDIA NA KWENDA HOSPITALI
walifika salama salimini huko india na walifanyiwa vipimo upya huko hospitali ya APPOLO NEW DELH India na ikawa imehakikiwa kuwa alikuwa na tatizo la figo na alitakiwa kubadilishiwa nyingine kama vipimo vya hospitali za hapa nyumbani Tanzania vilivyoonesha.

Wakati nikisubiri kwenda nilijulishwa na wao kuwa ubalozi wa Tanzania kule India uliwataarifu kuwa asingehitajika msindikizaji kwani kuna ma-nesi wa kutosha kuwahudumia kwa hiyo safari yangu ya India ikawa imeisha pale.

OPARESHENI
Ndugu yangu alifanyiwa oparesheni kwa mafanikio makubwa.

KUWASILI NYUMBANI NA HALI YA MGONJWA
Ndugu zangu hawa donor pamoja na alikuwa mgonjwa wote waliwasili nyumbani tarehe 25/04/2017, akitanguliwa na donor maana hali yake pamoja na mgonjwa ilionekana kutengemaa.

Ninapenda kumshukuru Mungu sana kwa ajili ya ndugu yangu huyu kwani maendeleo yake ni mazuri mno na vidonda alivyokuwa navyo miguuni hapo mwanzo vimekauka kabisa. anaonekana mwenye furaha iliyopitiliza tofauti na mwanzoni alikuwa ni mtu mwenye hasira kila dakika. Afya yake imeimarika sana kiukweli tumefarijika mno na hali yake.

Ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa wanajamvi wote kwa ushauri wenu, ninapenda kuishikuru serikali kwa msaada wao mkubwa maana gharama za zaidi ya milioni mia moja tusiweza kuzimudu. asanteni sana wote waliohusika Mungu awabariki
 
So touching. Kwenye masuala ya magonjwa au kuugua, Jf imekuwa ni the best jovial family kwenye kupeana msaada wa hali na mali.

Poleni mkuu, na pia Mwenyezi Mungu amtangulie mgonjwa na kuendelea kuimarisha afya yake.

Zangu dua.

-Kaveli-
 
Very minor error. Sidhani kama error hiyo inabadilisha au kubatilisha maudhui ya bandiko lake.

Sitaki kuamini kuwa as a prudent person, hiyo date error ndo ulichokiona pekee cha msingi mpaka unaamua kukishikia bango.

-Kaveli-
ni kweli wakuu nimerekebisha ilikuwa typing eror samahani kwa usumbufu uliojitokeza
 
So touching. Kwenye masuala ya magonjwa au kuugua, Jf imekuwa ni the best jovial family kwenye kupeana msaada wa hali na mali.

Poleni mkuu, na pia Mwenyezi Mungu amtangulie mgonjwa na kuendelea kuimarisha afya yake.

Zangu dua.

-Kaveli-
nashukuru sana mkuu jamii forum is best among the best. kila wakati hat unbgemuuliza kitu kidogo alikuwa anabadilika na kuwa mwenye hasira sana ila sasa hivi du huwezi amini mwenye furaha kuu mno mkuu
 
Sorry to say this man, Kaveli your ID and sometimes your style sounds like muhuni flan ila unaubinadamu Sana mkuu. Unaweza kuamini mtu hajaona chochote cha maana katika uzi wote ila kosa la tarehe tu.

Tukirudi kwenye mada, hii habari imenigusa sana. Vilevile sio wote wenye kukumbuka kushukuru au kutoa mrejesho kwa jamii.

Mungu aendelee kuwalinda na kuimarisha afya zao.
 
Sorry to say this man, @kavel your ID and sometimes style sounds like muhuni flan ila unaubinadamu Sana mkuu. Unaweza kuamini mtu hajaona chochote cha maana katika uzi wote ila kosa la tarehe tu.

Tukirudi kwenye mada, hii habari imenigusa sana. Vilevile sio wote wenye kukumbuka kushukuru au kutoa mrejesho kwa jamii.

Mungu aendelee kuwalinda na kuimarisha afya zao.
amen nashukuru sana mkuu ni kweli it was too touching because he just 30s years of age tunamuhitaji sana katika ngazi ya familia na katika taifa pia ukizingatia ni mfanyakazi wa serikali. figo zote zilikuwa zimefeli kabisa ila mungu ni mkuu sana ninweza kusema amepona kabisa kwa hali yake nzuri mno mkuu
 
amen nashukuru sana mkuu ni kweli it was too touching because he just 30s years of age tunamuhitaji sana katika ngazi ya familia na katika taifa pia ukizingatia ni mfanyakazi wa serikali. figo zote zilikuwa zimefeli kabisa ila mungu ni mkuu sana ninweza kusema amepona kabisa kwa hali yake nzuri mno mkuu

Ni kwa vile tu uwezo na wakati mwingine hospitali zetu vitendea kazi vinasumbua, lakini kufanya checkup za afya mara kwa mara ni muhimu sana pale inapobidi na uwezo kuruhusu.

Pia ni wito wa serikali kuwa na mikakati ya muda mrefu kuwa na hospitali za kisasa na wataam ili kuhudumia watu wengi kwa gharama nafuu.

Kama tumeweza kwenye taasisi ya moyo muhimbili na kwenye uwekezaji wa ndege, hata hili nna imani linawezekana, ni kuweka vipaumbele sahihi tu.
 
Ni kwa vile tu uwezo na wakati mwingine hospitali zetu vitendea kazi vinasumbua, lakini kufanya checkup za afya mara kwa mara ni muhimu sana pale inapobidi na uwezo kuruhusu.

Pia ni wito wa serikali kuwa na mikakati ya muda mrefu kuwa na hospitali za kisasa na wataam ili kuhudumia watu wengi kwa gharama nafuu.

Kama tumeweza kwenye taasisi ya moyo muhimbili na kwenye uwekezaji wa ndege, hata hili nna imani linawezekana, ni kuweka vipaumbele sahihi tu.
nimekupata vema sana mkuu naamini kwa mawazo kama haya yakifanyiwa kazi basi hatutafikiria kwenda india kwa matatizo kama haya Tanzania itakuwa centre ya wataalamu kama hawa na mambo mengi yata pata dawa ajira, kipato kukua n.k
 
Alhamdulillah Mwenyezi Mungu ashukuriwe saana kwa kumponyesha haraka. Ila ushauri wangu kwa mgonjwa awe anafuatilia vizuri sana ushauri na nasaha za madaktari kwa asilimia mia bila kuwacha kitu.
 
Alhamdulillah Mwenyezi Mungu ashukuriwe saana kwa kumponyesha haraka. Ila ushauri wangu kwa mgonjwa awe anafuatilia vizuri sana ushauri na nasaha za madaktari kwa asilimia mia bila kuwacha kitu.
ni kweli na kwa kweli anavyoonekana hataki utani na afya yake kwa sasa anajali sana anachoelekezwa na daktari wake mkuu
 
Sorry to say this man, Kaveli your ID and sometimes your style sounds like muhuni flan ila unaubinadamu Sana mkuu. Unaweza kuamini mtu hajaona chochote cha maana katika uzi wote ila kosa la tarehe tu.

Tukirudi kwenye mada, hii habari imenigusa sana. Vilevile sio wote wenye kukumbuka kushukuru au kutoa mrejesho kwa jamii.

Mungu aendelee kuwalinda na kuimarisha afya zao.


Mkuu Samaritan, heshima kwako kaka. Awali ya yote, I like your ID. It portrays something very nice. I'm sure you are among of nice people.

Kuhusu ID yangu na life style yangu hapa JF, yawezekana kweli inanireflect as mhuni flani, but wewe ni wa kwanza kuniambia hili. Nakushukuru sana kwa hili ndugu yangu, coz limenijenga na umenisaidia, itabidi nijitahidi kuchange my life style humu Jf ili nisiendelee kuwa 'judged by looking at the cover'. Lol

All in all, thanks mkuu. I am really humbled.

Back to topic, kwakweli nimeguswa sana na hili bandiko. Insha-Allah Mwenyezi Mungu azidi kumfanyia wepesi mgonjwa ili arejee kwenye majukumu yake ya kitaifa na kuijenga family yake.

Zaidi nimefurahi mdau kutuletea mrejesho in a very kind manner. Japo wengine wao hawakuona dhima yoyote kwenye mrejesho huu bali typing date error tu.

Tuzidi kumtumainia Mungu.

-Kaveli-
 
Mkuu Samaritan, heshima kwako kaka. Awali ya yote, I like your ID. It portrays something very nice. I'm sure you are among of nice people.

Kuhusu ID yangu na life style yangu hapa JF, yawezekana kweli inanireflect as mhuni flani, but wewe ni wa kwanza kuniambia hili. Nakushukuru sana kwa hili ndugu yangu, coz limenijenga na umenisaidia, itabidi nijitahidi kuchange my life style humu Jf ili nisiendelee kuwa 'judged by looking at the cover'. Lol

All in all, thanks mkuu. I am really humbled.

Back to topic, kwakweli nimeguswa sana na hili bandiko. Insha-Allah Mwenyezi Mungu azidi kumfanyia wepesi mgonjwa ili arejee kwenye majukumu yake ya kitaifa na kuijenga family yake.

Zaidi nimefurahi mdau kutuletea mrejesho in a very kind manner. Japo wengine wao hawakuona dhima yoyote kwenye mrejesho huu bali typing date error tu.

Tuzidi kumtumainia Mungu.

-Kaveli-
asante mkuu tupo pamoja
 
Kila la kher kwa mgonjwa!,samahani huyu donor ni mmoja wa familia ya mgonjwa amejitolea,au ilifanyika biashara huyu jamaa ameuzwa figo yake?,kubaki na figo moja hakuna madhara kiafya?...
 
Kila la kher kwa mgonjwa!,samahani huyu donor ni mmoja wa familia ya mgonjwa amejitolea,au ilifanyika biashara huyu jamaa ameuzwa figo yake?,kubaki na figo moja hakuna madhara kiafya?...
ndio kabisa ni mdogo wake mama mmoja baba mmoja wamezaliwa tumbo moja kabisa, hakuna biashara hapo mkuu ni jambo la upendo kwa kaka ndilo lilifanyika mkuu. kwa ninavosikia hakuna madhara labda madaktari waliopo humu watusaidie mkuu
 
ndio kabisa ni mdogo wake mama mmoja baba mmoja wamezaliwa tumbo moja kabisa, hakuna biashara hapo mkuu ni jambo la upendo kwa kaka ndilo lilifanyika mkuu. kwa ninavosikia hakuna madhara labda madaktari waliopo humu watusaidie mkuu
Yeah udugu kusaidiana sio kufafana,hebu ngoja tuone Madaktari wanasemaje kuhusu hili..
 
Back
Top Bottom