Wakuu, hakuna mahali niliposema nimetapeliwa na mtu kwa sababu sikuwa nimekopesha mtu. Ninachosema ni kwamba lengo langu la kumtafuta huyo mtu, lilikuwa ni ili kujiridhisha kama yuko serious nimuongezee mtaji na sasa awe amepata mtaji wa kutosha ambao ungemuwezesha kutoka alipo. Lakini kinyume chake akaleta dharau na kejeli ambazo kwa kweli sikutarajia. Hilo ndilo jambo lililonishangaza nakunisikitisha.
Naomba nisisitize tena, sikutapeliwa maana sikukopesha mtu, na wala sisikitiki kupoteza hela maana sikwenda kwa ajili ya kurudishiwa.
Na hoja ya hela ilikuwa ni kidogo au nyingi, hiyo si hoja ya msingi ya kumfanya mtu ajibehave hivyo.
Ni sawa na mtu anakuja anakukopa 2000 kwa hoja kuwa kakwama kabisa hana namna, unampatia kwa makubaliano kuwa atakurudishia tarehe fulani? Baada ya tarehe kupita, ukimtafuta ili kujua kulikoni, anakuambia mbona unanipigia simu asubuhi sana? Halafu mwingine anakuuliza yaani buku mbili ndio unafuatilia? Nafikiri si sawa. Suala si kiwango cha hela katika muktadha huu bali mazingira, na ndio maana inaweza kugombana na konda kwa chenji ya 100, si kwa sababu no nyingi lakini mazingira na staili ya mawasiliano.