Halafu kwa sasa hivi akili yako haipo sawa kabisa. Kwa sasa moyo ndio unaokuongoza. Nadhani kila ukifumba macho unamuona anavyovutia na umbo lake akiwa uchi, unayaona makalio yake yanavyovutia, kisha unapiga picha kuna jamaa mwingine anapendwa kuliko wewe na anayashika hayo makalio kadri anavyojisikia, ...hicho ndio kinakuumiza jomba. Okay fanya hivi jikaze kama miezi miwili hivi bila kumtafuta. Nina uhakika yeye na huyo jamaa hawezi kudumu zaidi ya miezi miwili, wataachana tu. Baada ya miezi miwili mtafute kupima upepo, ukikuta bado yupo na jamaa basi jiambie nafsini mwako kuwa huyo sio wako tena, na uweke nadhiri ya kuachana naye. Ila ukimkuta washamwagana na jamaa basi mrudie ili usiendelee kuumia. Huyo demu unampenda mpaka basi hivyo wewe ufuate moyo wako baada ya hiyo miezi 2 provided hayuko na jamaa.