Mrejesho: Harakati za kutafuta mpaka kuandikishwa JWTZ

Mrejesho: Harakati za kutafuta mpaka kuandikishwa JWTZ

Himidt Lengo

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2018
Posts
389
Reaction score
370
Habarini ndugu ?

Ninawashirikisha baadhi ya harakati nilizofanya katika kutafuta kuandikishwa na kuwa askari JWTZ.

Ni ndoto yangu tangu nikiwa mdogo kiumri kuwa askari wa JWTZ hususa ni kuwa komandoo. Baada ya kuhitimu kidato cha nne nilitaka kwenda jeshini wazazi wangu wakanikatalia wakasema niende kidato cha tano kwa maana nilifaulu vizuri, nikaenda huko nikahitimu pia. Nilienda JKT kwa mujibu wa sheria sikubahatika kupata nafasi ya kubakizwa na kuendelea na jeshi la wananchi badae wazazi Wakanitaka kwenda chuo kikuu nikaenda kusoma nikahitimu shahada ya sayansi katika fizikia mwaka 2017.

Baada ya Kuhitimu chuo kikuu nilipambana sana kurudi jeshini ila sikufanikiwa. Nilitaka kuachana na haya masuala ya kutafuta uanajeshi lakini kila mda nafsi ikawa inaumia😭😭😭 na kuniambia kuwa ninatakiwa kupambana kwa namna yoyote ili mwishowe nikaitumikie nchi yetu ya Tanzania kupitia kuwa askari JWTZ, Ninaumia sana roho kutokuwa huko mpaka mda huu. Kwa kuwa sina mbanga wa kunisaidia nikaona mbanga ni mimi mwenyewe nikapambana.

Nikafanya maamuzi magumu sana nikabadili majina, nikafanya mtihani wa QT nikafaulu, mwaka uliofuata nikafanya mtihani wa kidato cha nne kama private candidate nikafaulu pia. Nikatafuta na nyaraka zingine muhimu nikazipata ili nikasome kozi ya afya ambayo jeshi linataka halafu nikiihitimu hiyo diploma basi nirudi JKT nikajitolee, ili nafasi za kuandikishwa JWTZ zikitolewa basi nifanye usaili nijiunge nao Tatizo likawa kupata kitambulisho cha NIDA chenye namba ya NIDA, majina na mwaka wa kuzaliwa tofauti na ile NIDA yangu ya kwanza, nilipambana kweli kweli lakini sikufanikiwa watu wa NIDA hata nilioahidi chochote kitu wakakataa na kuniambia haiwezekani. Oparesheni yangu niliyoipa jina la Oparesheni kuandikishwa jeshini ambayo ingechukua miaka saba, ikafeli !

Rejea huu uzi 👇


Nikajaribu kutafuta mtandaoni nchi ambazo zinapokea watu ambao sio hata raia wao ili wawe wanajeshi wao nikaona ni ufaransa kwa programu yao ya French Foreign Legion (FFL) lakini ni gharama sana mpaka kuweza kufanikiwa kuandikishwa FFL maana kuna gharama za visa za kusafiria, kuna nauli ya ndege, kuna hela ya kutumia kipindi mchakato wa usaili ukiendelea, na sina hiyo hela maana kwa sababu sijafanikiwa kujiunga na JWTZ labda ningefanikiwa kule FFL kwa kutumia hela.

OMBI KWA JWTZ: Kuna askari mna umri wa kuweza kuwa hata baba zetu lakini bado mpo jeshini. Kuna vijana tuna umri mdogo kuliko ninyi tunahitaji sana kuwa askari wa JWTZ, tunaomba mtupe nafasi na sisi pia tuje huko tutumikie wote hii nchi kupitia huko maana tunahitaji sana, Tusije kufa na ndoto zetu hazijatimitia. Roho inaniuma sana kukosa jeshi na miaka yangu hii 34 wakati kuna watu mna miaka 50 bado mpo sana mkilitumikia jeshi letu miaka kumi au na zaidi ya hapo, kwa nini mtubague sisi tulio na umri wa chini yenu ? Vita ikitokea mtatuwekea vigezo hivyo hivyo mnavyotuwekea au mnahisi tunafuata posho za jeshi tuu 😭😭😭 ? si tungekuwa wafanyabiashara kama malengo yetu ni kuwa mabilionea ?

Tafadhali tupeni nafasi, tukifia mazoezini kwa sababu ya umri wetu mnaoita ni mkubwa, ni vizuri tuu tutajivunia kuwa tumefia mazoezini JWTZ kuliko kufa kwa visababishi vya hovyo.

Ninawatakieni majukumu mema.​
 
Mkuu sifa ya hili jeshi ilishaenda na Mwamunyange saiv hakuna tofauti na kikundi cha kusifu na kuabudu

Maana madili yanayopigwa saiv sio pow Kabisa ufisadi tuu umejaa

Jeshi letu kwel la kwenda kongo kupigwa na kuludishwa bila hata silaha tena mnapitishwa Rwanda

Pambania mengine mkuu jeshi lilishapoteza sifa yake
 
Sasa kwa sababu imeshindikana kupata nafasi hiyo, na siwezi kuishi bila kuwa na Maisha ya kijeshi, na ninapenda sana jeshi, Kiufupi ninapenda sana kuendelea kufahamu Zaidi kuhusu silaha, mbinu za kivita Zaidi, kwata mbali mbali, kombati karate, singe n.k

Ninaomba kufahamishwa yafuatayo.

1. Jinsi ya kuomba nafasi ya kujiunga na mafunzo ya Jeshi la akiba (KJA)

2. Mafunzo ya KJA yanatumia mda gani ?

3. Mtu akihitimu yale mafunzo ya awali ya jeshi la akiba, je kuna mafunzo mengine yanaendelea kwa upande wa jeshi la akiba ?

4. Mafunzo ya juu ya mwisho kabisa yanayoruhusiwa kwa askari wa KJA ni ya ngazi ipi ?

5. Ninaomba kufahamishwa mtiririko wa vyeo ambavyo askari wa KJA anavipitia kuanzia cheo kidogo mpaka cheo cha juu kabisa. Huwa naskia volunteer leader, Kuna askari wa KJA wana V kwenye kombati zao wanazipataje ? na mambo kadha wa kadha kuhusu KJA ambayo siyafahamu ili niifahamu vizuri.

6. Intake nyingine ya KJA ni lini ? Ninahitaji kujiunga nao nikamtumikie mama Tanzania.
 
Ndugu umenivunja moyo na kunisikitisha sana, namana umehangaika sana kiasi hicho iliupate nafasi ya kuja kutupiga mabuti mitaani tarehe 29 Oktoba, Aiseee...
Pole mkuu, askari hayupo kwa ajiri ya kukupiga mabuti yupo kwa ajiri ya kukulinda uishi kwa amani. Inapotokea umevunja sheria ndio unadhibitiwa sasa ili usiharibu amani ya nchi. Ninawapenda sana watanzania wenzangu, siwezi kukuonea mkuu.
 
Mkuu sifa ya hili jeshi ilishaenda na Mwamunyange saiv hakuna tofauti na kikundi cha kusifu na kuabudu

Maana madili yanayopigwa saiv sio pow Kabisa ufisadi tuu umejaa

Jeshi letu kwel la kwenda kongo kupigwa na kuludishwa bila hata silaha tena mnapitishwa Rwanda

Pambania mengine mkuu jeshi lilishapoteza sifa yake
Asante kwa maoni yako mkuu.
 
Pole mkuu, askari hayupo kwa ajiri ya kukupiga mabuti yupo kwa ajiri ya kukulinda uishi kwa amani. Inapotokea umevunja sheria ndio unadhibitiwa sasa ili usiharibu amani ya nchi. Ninawapenda sana watanzania wenzangu, siwezi kukuonea mkuu.
Nazungumzia maandano ya amani ya kudai haki oktoba 29 namana na hapo tutakuwa tumevunja sheria, najua mabuti yatahusika hapa iwe isiwe.
 
Mkuu sifa ya hili jeshi ilishaenda na Mwamunyange saiv hakuna tofauti na kikundi cha kusifu na kuabudu

Maana madili yanayopigwa saiv sio pow Kabisa ufisadi tuu umejaa

Jeshi letu kwel la kwenda kongo kupigwa na kuludishwa bila hata silaha tena mnapitishwa Rwanda

Pambania mengine mkuu jeshi lilishapoteza sifa yake
Napiga meza mkono...
 
Sasa kwa sababu imeshindikana kupata nafasi hiyo, na siwezi kuishi bila kuwa na Maisha ya kijeshi, na ninapenda sana jeshi, Kiufupi ninapenda sana kuendelea kufahamu Zaidi kuhusu silaha, mbinu za kivita Zaidi, kwata mbali mbali, kombati karate, singe n.k

Ninaomba kufahamishwa yafuatayo.

1. Jinsi ya kuomba nafasi ya kujiunga na mafunzo ya Jeshi la akiba (KJA)

2. Mafunzo ya KJA yanatumia mda gani ?

3. Mtu akihitimu yale mafunzo ya awali ya jeshi la akiba, je kuna mafunzo mengine yanaendelea kwa upande wa jeshi la akiba ?

4. Mafunzo ya juu ya mwisho kabisa yanayoruhusiwa kwa askari wa KJA ni ya ngazi ipi ?

5. Ninaomba kufahamishwa mtiririko wa vyeo ambavyo askari wa KJA anavipitia kuanzia cheo kidogo mpaka cheo cha juu kabisa. Huwa naskia volunteer leader, Kuna askari wa KJA wana V kwenye kombati zao wanazipataje ? na mambo kadha wa kadha kuhusu KJA ambayo siyafahamu ili niifahamu vizuri.

6. Intake nyingine ya KJA ni lini ? Ninahitaji kujiunga nao nikamtumikie mama Tanzania.
Miaka 35 bado unawaza mambo ya kijinga no wonder umelikosa jeshi kwa akili hizo
 
Sijajua malengo yako hasa ni yapi Ila kwa ninavyojua kubadlisha majina na mwaka pale NIDA hiyo huduma IPO .
 
Sijajua malengo yako hasa ni yapi Ila kwa ninavyojua kubadlisha majina na mwaka pale NIDA hiyo huduma IPO .
Lengo ni kubadili majina yote, nipate namba ya nida tofauti na niliyo nayo ili kuendana na sifa ambazo jeshi linazitaka nikajiunge nao.
 
Back
Top Bottom