Mrejesho ajali ya coaster Tanga

Pole sana mkuu na mtoto wetu, mungu awape uponyaji na awalaze mahali pema peponi waliofariki katika ajali hiyo.

Katika ajali hii dreva wa coaster ni mzembe sana, kwa nini akimbize gari lenye abiria na ku overtake Lori bovu sehemu ya mlimani ambayo haoni mbele vizuri? ?

Serikali, msikae kimya ajali za barabarani hv sasa ni janga zito na kubwa hivi kweli imeshindikana kabisa kuzizidhibiti? ?
Mfano haya malori kuharibika barabarani ambapo ni nyembamba, hv serikali mmeshindwa kabisa kujenga diversions mfano wa vituo vya mabasi ila viwe virefu kila baada ya kilomita 10, kwa ajili ya kuegesha malori mabovu, yaliyopata hitilafu, madereva kupumzika nk hii ingekupunguza kwa kiasi kikubwa ajali hizi.
Pia traffic police rudisheni road patrol, kuna madreva wazembe wengi ambao mngeweza kuwabaini mara moja kuliko kukaa sehemu moja na kupima speed tu, viongozi wetu acheni kukariri mambo hayo hayo kila siku, jaribuni kuwa wabunifu, watu wengi wanapoteza maisha huko barabarani ni lazima sasa kitu kikubwa kifanyike.
Sijui hata kama ushauri wangu huu utamfikia yoyote na kuleta badiliko Kwny janga hili.
 
Pole sana! Mwenye Enzi Mungu aendelee kuwabariki! RIP kwa hao watu wa4 jamani!
 
Pole sana
 
Wanajamii. ... sikusudiii kuanzisha hoja ya kisiasa tafadhali nieleweni. Ila inafaa sana kujua. Mapesa yote yanayo kusanywa kweli tunashindwa kua na fungu ambalo linaweza kuwa tayari kukabiliana na mambo kama haya. Mtu anafika hospital anashonwa bila sindano ya ganzi? Hata gari la wagonjwa hakuna? Tanzania ndio inayoongoza kwa kukusanya kodi za bara bara Africa kwa nini kusiwe na fungu la kukabiliana na mambo kama haya?
 
Dah, hii thread imenisikitisha sana, pole sana mkuu, Msijali mtapona tu.
Na vipi kuhusu dripu? Walikuwekea? Manake umepoteza damu na maji mengi
 
Pole Mkuu@Kipumbwi Inshaallah mwenyezi Mungu atakupa Shifaa
 
Pole sana mkuu..Mungu ni mwema kwako
 
Ooh jamani poleni sana, Mola awaondolee maumivu na mpone haraka.

Hiyo habari ni ya kusikitisha sana juu ya hospitali zetu nchini hapa.
Waeleze wanaokutuma kutukana wenzio basi wafanye na yanayowahusu siyo pole wakati wewe ni kati ya tatizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…