Mratibu wa zoezi la kuunga mkono jitihada za Rais Suluhu ni nani?

Mtukudzi

Senior Member
Nov 14, 2013
103
408
Mh. Samia Suluhu aliposema KAZI IENDELEE alimaanisha mambo yote 'mazuri' yaendelee kama ilivyokuwa kwa hayati JPM. Tunatambua kuwa mojawapo ya 'kazi' ambazo zilikuwa zikiendelea kwa kasi hapa nchini ni pamoja na 'kuunga juhudi' za Mh. Rais. Sasa inakuwaje kazi hizi haziendelei?.

Je mratibu/waratibu wametingwa na shughuli za bunge au tuwaeleweje sasa? Kufuatia hotuba ya Madam President, kuna watu hasa viongozi wa vyama vya upinzani wamejitokeza hadharani kuonyesha wazi wanaunga mkono juhudi za Mh. Samia. Kwa nini waratibu wa zoezi la kuunga mkono juhudi hatuwaoni Channel Ten live kunako ofisi za Lumumba wakiendelea na kazi yao?.

Tumewaona Mh. Mbowe akikiri kuwa amelazimika kutoka Dubai kuja kutoa ushuhuda wa matendo makuu ya Madame President. Siyo huyo tu, Sugu amesema amesitisha azma yake ya kuhamishia biashara zake South Africa kwa kuwa Rais Samia amemkosha. Lema yuko tayari kurejea Tanzania.

Chonde chonde waratibu timizeni wajibu wenu. Unafuu wa safari hii waungaji mkono hawana gharama yoyote na hapahitajiki matumizi ya vitisho na ushawishi kama ambao Mh. Lema alidai kuwahi kufanyiwa na Mh. Bashiru Aly. Mkichelewa sana watajitokeza waratibu fake wawafanyie utapeli waungaji mkono.

Kazi iendelee..!
 
Naomba pia kumfahamu Mratibu wa kuunga mkono juhudi za Rais aliyepita
Kwa ujumla ukiangalia kwa Rais aliyepita utaona zoezi lilikuwa linafuata pattern fulani. Hii inaashiria uwepo wa uratibu.
Vinginevyo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Bw. Mashinji anaweza kusaidia kujibu swali lako
 
Naomba pia kumfahamu Mratibu wa kuunga mkono juhudi za Rais aliyepita
Mfadhili alikuwa mwendazake,mtoa pesa Bashiru na mratibu Pole pole,

Field officers ni:
1. Sabaya DC Hai,
2. Gelasius Byakanwa RC Mtwara (huyu alikuwa Hai DC) ,
3. Alexander Mnyeti ( former Manyara RC, sasa hv mbunge Misungwi alikuwa DC Arumeru zoezi la kununua madiwani lilipoanzia),
4. Gambo former Arusha RC now Arusha MP,
5. RC Iringa Ally Happy
 
Mfadhili alikuwa mwendazake,mtoa pesa Bashiru na mratibu Pole pole,

Field officers ni:
1. Sabaya DC Hai,
2. Gelasius Byakanwa RC Mtwara (huyu alikuwa Hai DC) ,
3. Alexander Mnyeti ( former Manyara RC, sasa hv mbunge Misungwi alikuwa DC Arumeru zoezi la kununua madiwani lilipoanzia),
4. Gambo former Arusha RC now Arusha MP,
5. RC Iringa Ally Happy
Heri James na Bashite mbona siwaoni! Ina maana hawakuwepo! Halafu sioni hata jina la mmama mmoja tu! Vipi akina Anjela Kairuki, Jokate Mwegelo, nk. Nao hawakuchangia chochote!!
 
Heri James na Bashite mbona siwaoni! Ina maana hawakuwepo! Halafu sioni hata jina la mmama mmoja tu! Vipi akina Anjela Kairuki, Jokate Mwegelo, nk. Nao hawakuchangia chochote!!
Mkuu unaweza kui-expand tupate complicity wote wa kuratibu, kufadhili na kugharamia manunuzi ya zoezi la uungaji fake wa juhudi.
 
Naomba pia kumfahamu Mratibu wa kuunga mkono juhudi za Rais aliyepita
Dr. Bashiru Ally.

Naskitika sana kwamba mtu huyu alikuwa mwalimu wangu pale mlimani. Sijawahi kujua kwamba bwana Bashiru Ally ni mpumbavu wa kiwango cha kuamini kwenye Dola kushinda uchaguzi badala ya nguvu ya hoja
 
Back
Top Bottom