Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe unaendelea kama kawaida, "kuchukuliwa" na China ni uvumi mbaya tu

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
324.jpg

Hivi karibuni, habari kwamba "kwa sababu serikali ya Uganda imeshindwa kulipa madeni ya China, China itachukua uwanja pekee wa ndege wa kimataifa wa nchi hiyo Entebbe International Airport” imeenea kwa haraka kwenye mitandao ya kijamii na kuvutia ufuatiliaji mkubwa wa pande mbili za China na Afrika. Hivi sasa, mradi wa ujenzi na upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Entebbe ambao China inashiriki unaendelea kama kawaida, na Uganda bado ipo katika kipindi cha kusamehewa deni kwa mujibu wa mkataba uliosainiwa, kwa hivyo habari hii ni uwongo unaotuhumiwa kuharibu ushirikiano wa kirafiki baina ya pande hizo mbili, kabla ya kufanyika kwa mkutano wa nane wa mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC unaoendelea mjini Dakar, Senegal.

Kwenye tovuti ya Google, habari husika ilionekana kwa mara ya kwanza kwenye video iliyotolewa Oktoba 28 mwaka huu na NTVUganda, kampuni tanzu ya kampuni ya habari ya kibinafsi ya Kenya National Media Group. Video hiyo ilionyesha kuwa Waziri wa Fedha wa Uganda Matia Kasaija alizungumza na vyombo vya habari baada ya kuhojiwa bungeni. Alipoulizwa ni matokeo gani yangetokea kwa Uwanja wa Ndege wa Entebbe iwapo Uganda itashindwa kulipa mkopo kwa wakati, Bw. Kasaija alisema “hakuna hatari kama hii, na hata kama hali hii isiyowezekana itatokea, yaani wakati mamlaka ya usafiri wa anga haitakuwa na mapato ya kutosha ya kuhudumia mkopo huo, serikali kuu itaingilia kati." Siku iliyofuata, taarifa iliyotolewa na Bunge la Uganda ilithibitisha hoja hiyo. Lakini si NTVUganda wala bunge la Uganda ilitaja kuwa China "imekuwa au itakuchukua hivi karibuni uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebbe”.

Tarehe 25 Novemba, Gazeti la Monitor la Uganda lilichapisha makala kwenye tovuti yake yenye kichwa cha "Uganda inalazimishwa kukabidhi uwanja wa ndege ili kulipa pesa za China", ambayo ilikuwa chanzo cha uvumi kwamba "China itauchukua uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebbe". Makala hiyo inasema, kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa kati ya serikali ya Uganda na Benki ya Export-Import ya China mwezi Machi 2015, China ilitoa mkopo wa dola za Marekani milioni 207 kwa riba ya 2% kusaidia upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe.

Makubaliano hayo yanabainisha kuwa muda wa ulipaji wa deni ni miaka 20, ikijumuisha muda wa kusamehewa wa miaka 7 (riba ndiyo inayotakiwa kulipwa, na mkopo wenyewe haujalipwa kwa wakati huo). Makala hiyo ilieleza kuwa kwa mujibu wa makubaliano hayo, mara Uganda itakaposhindwa kutekeleza makubaliano yake, China ina haki ya kukata rufaa ya usuluhishi, na mali za msingi za Uganda ukiwemo Uwanja wa Ndege wa Entebbe, zinaweza kuchukuliwa na Benki ya Export-Import ya China. Siku iliyofuata akaunti ya @TanzaniaUpdates iliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa "China itachukua uwanja wa ndege wa Entebbe", kauli ambayo ilienezwa sana. Akaunti hii inajidai kuwa ni chombo cha habari cha kwanza cha lugha ya Kiingereza nchini Tanzania, lakini haipatikani kwa kutoa habari yoyote au tovuti yoyote kwenye Google isipokuwa akaunti za Twitter na Instagram.

1127964776_16343980385351n.jpg

1127964776_16343980648861n.jpg
Baada ya uvumi huo kuenea, msemaji wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Uganda Vianney Luggya, alitoa taarifa kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akikanusha madai kuwa Uwanja wa Ndege wa Entebbe ulitumiwa kubadilishana fedha. Alisisitiza kuwa, "hakuna ukweli wowote hapa." Kuhusu kama serikali ya Uganda inaweza kulipa mkopo huo, jibu la msemaji lilikuwa wazi sana, Uganda na China zilisaini mkataba wa mkopo wa kibiashara wa kawaida. Uganda itaweka mapato ya uwanja huo kwenye akaunti ambayo China ina haki ya kuangalia, lakini hii haimaanishi kuwa uwanja wa ndege unamilikiwa na China. Haya ni maudhui ya kawaida sana katika mkataba wa mkopo wa kibiashara. “Makubaliano hayo yametoa muda wa msamaha wa miaka 7. Bado tuko ndani ya kipindi hiki, ambapo Uganda inalipa riba tu na serikali haishindwi kufanya hivyo."

Mnamo tarehe 29 Novemba, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bw. Wang Wenbin alisema kila msaada wa kifedha unaotolewa na China kwa Uganda unatokana na mahitaji na matakwa ya upande wa Uganda, na umefanyiwa upembuzi yakinifu na utafiti unaolenga soko. Makubaliano ya mkopo yamesainiwa kwa hiari na nchi hizo mbili kupitia mashauriano na tuhuma ya taasisi ya fedha ya China kukamata na kudhibiti miradi na mali za Uganda ni uvumi wenye nia ovu tu na hauna msingi wowote. Hali halisi ni kuwa, hakuna mradi wowote wa ushirikiano kati ya China na Afrika ambao "umedhibitiwa" au "kuchukuliwa" na China kwa sababu ya matatizo ya madeni.

Hadi kufikia sasa, serikali za Uganda na China zote zimetoa ufafanuzi kuhusu suala hilo. Hata hivyo, kinachostahiki kufuatiliwa ni kuwa kuenea kwa habari hiyo ya uwongo hivi karibuni kulitokea katika vipindi viwili muhimu. Kipindi cha kwanza ni kwamba waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Antony Blinken alitembelea nchi tatu za Afrika mapema mwezi huu na kutangaza kwamba Rais Biden wa Marekani ataitisha "mkutano" wa nchi za Afrika ili kuonyesha "moyo" wa Marekani kuelekea bara la Afrika. ". Kuhusu kipindi cha pili, ilikuwa ni mkutano wa 8 wa mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika uliofanyika Dakar, Senegal ulioanza Novemba 29. Ni wazi kuwa nyuma ya wazushaji wa uvumi huu ni nchi za magharibi, ambazo kwa mara nyingine tena zinaipaka matope sura ya China barani Afrika. Kwa upande mmoja, wanajenga mazingira mazuri ya kuandaa mkutano wa kilele kati ya Marekani na Afrika, na pia kushambulia "mshindani" wake China.

Hivi sasa kutokana na juhudi za pande mbili za China na Uganda, mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Entebbe unaendelea vizuri na umefikia asilimia 75.1, na unatarajiwa kukamilika na kukabidhiwa Disemba, mwakani.
 
Back
Top Bottom