Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 305
Mkuu Kingiwakati mwingine tusiangalie kujiunga tu bali ni nani anajiunga na chama fulani. hao jamaa wataweza kuleta ushawishi gani kwenye mabadiliko ya upigaji kura? jina tu si hoja bali elimu ya kutosha pia. siasa si mashairi useme utakaa chini na kuandika kisha uende studio kurekodi. lakini kama wana nia ya dhati basi wafanye hivyo.
Kujiunga na chama huwa hatuangalii majina wala elimu ya mtu, yeyote anayetimiza masharti ya chama anaweza kuwa mwanachama hata kama hajui kusoma wala kuandika, labda utuambie mtu kuchaguliwa kuwa kiongozi au mpigadebe rasmi wa chama hapo ndipo tunaweza kuangalia who is who.
Ingawa sijui elimu ya Mr. Sugu na Mkoloni lakini wanaonekana wanaimudu vilivyo fani yao, hivyo endapo watakuwa wapiga debe wa Chadema wanaweza kuleta changamoto katika kampeni na kuvutia wapiga kura wengi hasa vijana.
Wakati CCM wanawachagua Hadija Kopa na Komba kuwapigia debe sijui kama walifanya interview au kuitisha vyeti vyao lakini huwa wanaleta changamoto kubwa sana wakati wa kampeni.