Mr Sugu na Mkoloni Wajiunga Rasmi na CHADEMA

Mr Sugu na Mkoloni Wajiunga Rasmi na CHADEMA

wengine wanajiunga na upinzani na wengine wanakwambia changia ccm!

demokrasia oyeeee
 
In the begining I thought it was imposible. Lakini sasa naona inawezekana.

Hivi yule JF member Mwenye ule ugonjwa usiotibika na klorokwini anaona muamko?
 
wakati mwingine tusiangalie kujiunga tu bali ni nani anajiunga na chama fulani. hao jamaa wataweza kuleta ushawishi gani kwenye mabadiliko ya upigaji kura? jina tu si hoja bali elimu ya kutosha pia. siasa si mashairi useme utakaa chini na kuandika kisha uende studio kurekodi. lakini kama wana nia ya dhati basi wafanye hivyo.
 
wakati mwingine tusiangalie kujiunga tu bali ni nani anajiunga na chama fulani. hao jamaa wataweza kuleta ushawishi gani kwenye mabadiliko ya upigaji kura? jina tu si hoja bali elimu ya kutosha pia. siasa si mashairi useme utakaa chini na kuandika kisha uende studio kurekodi. lakini kama wana nia ya dhati basi wafanye hivyo.
kamanda penye nia pananjia hawa jamaa wanaushawishi mkubwa sana hasa kwa vijana na wadau wengine wengi so chadema kama chadema ni muda wao wa kusonga mbele kwa mbele na sugu na wenzake wanaweza....... yes unabii utatimia dis year
 
sugu n mkoloni uv chosen the best portion! keep it up guys!
 
Waangalie very soon wataanza kufuatwa na TRA walipe kodi ya mauzo ya music wao. Kama wana vi-studio, watalazimika kuvifunga. Wamuulize mtu anayeitwa ASKOFU mchimba madini wa mererani.
 
Tunawakaribisha kwenye jahazi sote kwa pamoja tusongeshe
 
Hivi yule JF member Mwenye ule ugonjwa usiotibika na klorokwini anaona muamko?

Teh! Teh! Teh! Teh! Acha wafu wazike wafu wao bana!!!

Yule hawezekani keshakuwa sugu wa ujinga!!
 
Tunawakaribisha kwenye jahazi sote kwa pamoja tusongeshe

Kweli lakini na iwe kweli ni kwa hiari yao wenyewe na sio wamekuja kupandikizwa CHADEMA ili saa ikifika wakififishe chama. Nina imani nao nawaona vijana kweli kweli wana-mapinduzi, nawaona kama sio wale wenye njaa ambao kwa njaa yao wangeweza kupewa kitu kidogo waje wachafue utulivu wakati wa dakika za mwisho. Tunawakaribisha kwa sababu tuna matumaini!

Hivi wanatokea CCM au walikuwepo kuwepo tu!?
 
Waangalie very soon wataanza kufuatwa na TRA walipe kodi ya mauzo ya music wao. Kama wana vi-studio, watalazimika kuvifunga. Wamuulize mtu anayeitwa ASKOFU mchimba madini wa mererani.

CCM hawako Smart kiasi hicho. Na swala la Askofu linatumiwa na CCM wenyewe kuwatisha watu. kama kweli wana ubavu huo si wangefunga biashara za Ndesamburo na Mbowe!!??
 
Hongera nyingi kwenu vijana,mmeonyesha njia. Kila la heri.
 
CCM hawako Smart kiasi hicho. Na swala la Askofu linatumiwa na CCM wenyewe kuwatisha watu. kama kweli wana ubavu huo si wangefunga biashara za Ndesamburo na Mbowe!!??

Hawa mbona ni wanafanyabiashara wanaoijua vizuri Tax code!!, hawa wanalipa kodi yao kwa mujibu wa sheria na hawana malimbikizi.
Tabu inakuja pale wanapowafumbia macho watu wenye kuganga njaa hawalipi kodi, siku wakikuona ni threat wanatumia sheria hiyohiyo kukumalizia, utapigwa tax arrears za tokea umeanza biashara plus interest, unajikuta chini.
Tanzania ukifuata sheria unakuwa huru zaidi kuibana CCM ila kama unaishi kiujanja ujanja siku wakikuona unawatisha wanatumia loop hole hiyo. Hebu jiulize kwa nini wahindi wengi ni wachangiaji wa CCM?, ni kwa sababu ni wakwepa kodi wazuri ila wanatumia kivuli cha kuchangia ili walindwe.
 
Kampeni za Mwaka huu zitakuwa tamu sana!!!

Nilizembea kurekebisha taarifa zangu kwenye daftari, hata ivo itabidi nisafiri takribani km 600 kwenda kupiga kura yangu kwenye kata niliyojiandikishia wakati uleeeeeeeeee...
 
Prof Jiiiiize, Hapo Vipi,Hapo Sawa???
 
Samson hakutegemea kuwa Delilah anaweza kumuangusha na Goliath alicheka wakati anamwona Daudi anamsogolea. Some time inahitajika combination fulani kutengeneza bomu.
 
Hongereni sana wakuu!

Hongera pia kwa wote wanaopenda mabadiliko. Imekuwa ni jambo la kawaida katika nchi yetu wengi kushabikia CCM kwa kuwa wanaamini watafaidika kwa namna mbalimbali. Ndio maana hata wasomi wetu, wafanyabiashara hata watu walio nchi za nje kwa utashi wao wa ubinafsi wamekuwa mstari wa mbele kushabikia na kuchangia CCM wakiamini kuwa nao hawatasauliwa kwenye kupewa kipande cha keki. Ukweli wa nini wanakishabikia wanaujua wenyewe. Sijashawishika bado kuamini kuwa hao wote wanadhani CCM inafanya vyema katika kuongoza taifa hili, na kwamba hakuna watanzania wenye uchungu na kuhitaji mabadiliko, au hivyo ndivyo tulipaswa kuwa hata kama tungekuwa na viongozi bora. Kwa mantiki hiyo hata wasanii wetu wengi wamekuwa wakiingizwa kwenye mkumbo huo.

Kwa upande mwingine, mtu anayeeleza ukweli kadri anavyouona amekuwa adui mkubwa wa CCM na wapambe wao. Ukiona mtu yuko tayari kuueleza ukweli huo hadharani na mchana kweupe, ni lazima tumheshimu huyo mtu, na kukubali kuwa anatumia kichwa chake kufikiri, na sio kusaidiwa na wengine kufikiri. Ndio maana mimi nawaheshimu sana watu wote ambao wako mstari wa mbele kuleta mabadiliko katika nchi yetu. Mabadiliko ni jambo la lazima sio la hiari.

Nawapongeza sana wakuu hao waliojitoa mhanga kuutetea ukweli. Tunajua kuna gharama za kuingiza mchanga kwenye keki ya CCM, lakini ni gharama ambayo ni haki kuipigania, hii nchi ni yetu sote na sisi tunahitaji kuleta mchango wa kuiendeleza.
 
Back
Top Bottom