Mr.Blue ft. Ally Kiba - mboga saba official video

Blue mbona hazitendei haki nyimbo zake!?!?
Alikiba nae kaimba chorus nzuri kwenye video kavaa kishamba,hawa watu hawana washauri!
 
Verse 1 –Mr BlueMboga saba umeniteka, makahaba nawachekaKwenye mkataba nakuweka, kwenye mahaba nakuwekaNapiga ibada usije lala kwenye mkekaAah kama vumba likikataaAah ndumba halitovaaBila nyumba chumba kimoja utakaa?Nguo za mitumba nauliza mchumba utavaa? (Yeah)Yeah, basi mohoro, nakupenda na ngozi yako nyororoKote unakwenda hata kwenye vigodoroPenzi lako limenifunga minyororoBasi leo twende wapi? Nichukue bajaji nije kwenu MasakiTwende Coco Beach ukale mishikaki?Au Zara Moon ukale ugali samaki?Nachokupenda kuwa hujui kujivunaMtoto mzuri ila hujui kunichunaWatoto wa uswazi hawajui kunikunaMapenzi kamari ila hujui kunipunaPre-Chorus –Ali KibaNilipiga goti kwa Mungu na dua ikafikaHaya maisha yangu na wewe ukaridhikaChorus –Ali KibaEii…(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Unanifaa sana(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Nasikia raha(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Unanifaa sana(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Nasikia rahaVerse 2 –Mr BlueMtoto unajua njaa, (mtoto) unajau raha(Mtoto) kweli kifaa, (mtoto) kweli unafaaMoto bila ya mkaa, ndoto ya kila starWe ni joto kwangu baridi balaaBonge la bambataa, unapendeza unavovaaKwenye bed unavyocheza kama kwenye jukwaaMacho ya kulegeza, hii sio kungu nakataaKwenye giza waka waka kama taaUlaya bila visa nafika bila kupaaAh, mama halali wa pendoAchana na habari na skendoWanakaba kabari kila angleWanataka nife wateke mali wazibe pengoHawajui…Pengo langu halizibiki, hawasumbuiPendo gonjwa sugu halitibikiUnapendwa na babu na bibi, na mama na babaNakuita beki kwenye bonge la ligi unavyokabaMabrazameni ntawapiga shabaNiacheni na mboga saba, bakieni na makahabaNachompenda kuwa hajui kujivunaMtoto mzuri ila hujui kunichunaWatoto wa uswazi hawajui kunikunaMapenzi kamari ila hujui kunipunaPre-Chorus –Ali KibaNilipiga goti kwa Mungu na dua ikafikaHaya maisha yangu na wewe ukaridhikaChorus –Ali KibaEii…(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Unanifaa sana(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Nasikia raha(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Unanifaa sana(Oh yee ye oyee, oh yee ye oyee)Nasikia rahaOutroOh yee ye oyee, oh yee yee oyeeOh yee ye oyee, oh yee yee oyeeye
 
Blue anakuaga njema sana. Dogo anajua kuichezea mic. Siborekagi nikimsikia akishusha mistari.
 
VIDEO nzuri.... Audio hamna kitu... namkumbuka sana blue wa 2003-2009...

sahizi blue ameamua kuwa wa kawaida.... haya sasa na kiba kapiga chorus mbaya kabisa kuwahi kutokea...
Weeeeee kama sio mwanga basi mchawi wa maendeleo ya watu...toa yako basi tuoneee
 
Imefanana na taarabu..Ali kiba ndio ameimba kama Isha Mashauzi
Kuna namna waliifikiria kichwani wakaileta idea kwenye vitendo ikakataa ila wakaogopa kuambiana ukweli wakaipeleka kiaibuaibu mwisho imekuwa ya kawaida maana kiba kaamua kuifanya ya kawaida tu sio sanaaa.Blue anajitahidi ila freestyle verse asipende sana kuzihamishia kwenye kazi kabisa akubali kufikiria sana zaidi kabla ya kutoa wimbo nje ya hapo nyingi zitakuwa big g hata kabla ya show nyimbo imechuja#tuwakosoewajifunze#
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom