Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Poleni wafiwa. Poleni CUF kuondokewa na kada wenu.
Duu! huyu mazee alikuwa mpiganaji sana katika jimbo la Tunduru kwa kugombea ubunge
mara tatu bila kupata. Nakumbuka baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2010 na
yeye kukosa tena ubunge,alihitisha mkutano pale Tunduru mjini na akawapa ukweli wa live
wananchi wa Tunduru kuwa kuna baadhi yenu ni wanafiki. maana hiweje kila uchaguzi mgo
mbea wa ccm anishinde mimi kwa kura 20 hadi 50? kwahiyo nachukuwa nafasi hii kusema
sitagombea tena kwenye chaguzi zijazo na nitabakia kuwa mwanachama wa kawaida tu wa cuf.
Baada ya kusema hivyo,wananchi waliowengi waliangua vilio vikubwa sana pale mkutanoni.Na
walijaribu kumsihi na ajaribu tena 2015 lakini mazee alikataa katakata na mapema mwaka huu
akahamia rasimi DSM.
Hiyo ndiyo historia chache ninayoifahamu kuhusiana na marehemu mazee wa cuf. Mungu amlaze
mahala pema peponi!