Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,976
- 2,755
Nilienda mjini tarehe 27/02/2012 kuweka pesa yangu kwa wakala wa MPESA mjini. Wakala akapokea pesa na kuiweka akaniambia nisubiri msg ya kuwekea pesa toka MPESA kama kawaida. nilisubiri weee bila kupata ujumbe pamoja na juhudi nyingi kufanywa na wakala. mwisho niliamua kuondoka nikiacha id zangu na contact. Hadi leo sijapata huo ujumbe. nilirudi kwa wakala jana akanieleza nisubiri na hawezi kunirudishia pesa yangu kwa sababu tayari walishatuma MPESA. Wanasema eti MPESA kuna tatizo la network. Nimewapigia MPESA HQS simu yao ni unreachable. Je kuna mtu amepata Uzoefu huu wanajamii?