BABA TUPAC
JF-Expert Member
- Sep 30, 2015
- 1,533
- 3,837
Wakuu,
Nimekuwa na huyu kwenye mahusiano kwa muda wa miezi sita sasa. Ana duka la vifaa vya simu maeneo ya Kariakoo na ndio hapo tulipofahamiana
Nilikuwa sifahamu mpaka leo nilipomuuliza upo wapi? Akasema nipo kuchukua mzigo umefika tokea wiki iliyopita, nikasema nakuja (nafahamu kampuni ambayo huwa inamletea mizigo yake). Akawa anakataa, nikasema poa. Nikahisi atakuwa na mwanaume, ikabidi niende kimya kimya.
Kufika nakuta kuna canter inapakia majeneza, nikamuuliza mzigo wako upo wapi? Akasema ndio huo hapo, nikawa mdogo kama piritoni.
Kumbe ana frem pale Muhimbili, huwa anaagiza majeneza China na Thailand. Nilitaka kula mzigo leo, sina hata hamu dah
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuwa na huyu kwenye mahusiano kwa muda wa miezi sita sasa. Ana duka la vifaa vya simu maeneo ya Kariakoo na ndio hapo tulipofahamiana
Nilikuwa sifahamu mpaka leo nilipomuuliza upo wapi? Akasema nipo kuchukua mzigo umefika tokea wiki iliyopita, nikasema nakuja (nafahamu kampuni ambayo huwa inamletea mizigo yake). Akawa anakataa, nikasema poa. Nikahisi atakuwa na mwanaume, ikabidi niende kimya kimya.
Kufika nakuta kuna canter inapakia majeneza, nikamuuliza mzigo wako upo wapi? Akasema ndio huo hapo, nikawa mdogo kama piritoni.
Kumbe ana frem pale Muhimbili, huwa anaagiza majeneza China na Thailand. Nilitaka kula mzigo leo, sina hata hamu dah
Sent using Jamii Forums mobile app


