Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,163
- 11,230
Habari wanajamvi,
Nina mpenzi ambaye nilianza mahusiano naye wakati yeye yupo kidato cha Sita shule moja huko Bukoba.
Binti ni Mnyarwanda, kiukweli ni mzuri sana ukicheki nyoro inakuita.
Tulipendana sana na tulikuwa tukiongea kila siku jioni,pia nilikuwa nikiongea na marafiki zake sana,mimi nilikuwa Dar na yeye Bukoba.Nilifarijika nikajua ndoto ya kuoa mnyarwanda inatimia.Pesa ndogo ndogo za matumizi nilikuwa nampatia.Ilifika hatua hadi DP ya facebook akaweka picha yangu.
Alimaliza kidato cha sita na kujiunga UDSM kusomea sheria.
Miezi ya kwanza ya chuo mapenzi yalikuwa matamu na ndipo tukapata hata muda wa kula tunda la peponi.Mara ya kwanza sikutaka kumgegeda sababu alikuwa analindwa na sheria ya wanafunzi.
Hali ilibadilika baada ya kuzoea chuo na jiji,mtoto akawa hakamatiki,mapenzi akapunguza,mawasiliano akapunguza.
Facebook na Instagram akawa anaweka picha anakula bata na matozi na friends zake,picha wanazoweka ni za kuonesha makalio yalivyoumbika,ukweli kama kalio analo tena halisi.
Niliumia sana ukizingatia nilimpenda sana,nilipoteza muda wangu kwake lakini sasa hauthamini.
Kilichosababisha niandike uzi huu ni kuomba ushauri nifanye jambo gani niweze kumrudisha kwenye himaya yangu,ukweli nimemiss mapenzi yake,nakiri bado nampenda sana.
Basi hata nikishindwa kumrejesha basi nimshauri kuwa anapotea kwa mambo anayofanya, labda atanikumbuka kwa hilo.
Ushauri wenu ni muhimu wanaMMU.
Nina mpenzi ambaye nilianza mahusiano naye wakati yeye yupo kidato cha Sita shule moja huko Bukoba.
Binti ni Mnyarwanda, kiukweli ni mzuri sana ukicheki nyoro inakuita.
Tulipendana sana na tulikuwa tukiongea kila siku jioni,pia nilikuwa nikiongea na marafiki zake sana,mimi nilikuwa Dar na yeye Bukoba.Nilifarijika nikajua ndoto ya kuoa mnyarwanda inatimia.Pesa ndogo ndogo za matumizi nilikuwa nampatia.Ilifika hatua hadi DP ya facebook akaweka picha yangu.
Alimaliza kidato cha sita na kujiunga UDSM kusomea sheria.
Miezi ya kwanza ya chuo mapenzi yalikuwa matamu na ndipo tukapata hata muda wa kula tunda la peponi.Mara ya kwanza sikutaka kumgegeda sababu alikuwa analindwa na sheria ya wanafunzi.
Hali ilibadilika baada ya kuzoea chuo na jiji,mtoto akawa hakamatiki,mapenzi akapunguza,mawasiliano akapunguza.
Facebook na Instagram akawa anaweka picha anakula bata na matozi na friends zake,picha wanazoweka ni za kuonesha makalio yalivyoumbika,ukweli kama kalio analo tena halisi.
Niliumia sana ukizingatia nilimpenda sana,nilipoteza muda wangu kwake lakini sasa hauthamini.
Kilichosababisha niandike uzi huu ni kuomba ushauri nifanye jambo gani niweze kumrudisha kwenye himaya yangu,ukweli nimemiss mapenzi yake,nakiri bado nampenda sana.
Basi hata nikishindwa kumrejesha basi nimshauri kuwa anapotea kwa mambo anayofanya, labda atanikumbuka kwa hilo.
Ushauri wenu ni muhimu wanaMMU.