Mpenzi wangu amebadilika ghafla

Mpenzi wangu amebadilika ghafla

UMASKINI hakuna kinginee..!! Huna helaa kakaa na mazingira demu aliyokuta unaishi ni duni so kaona hapaa hakuna jipyaaaa si unajua pesa mbelee hawa viumbeee..
Bora useme wewe, eti kumkaza vizuri athubuuuutuuuu

Mwanamke hata akukute hanithi, kama una shekeli atajifanya we ndo unapeleka moto dunia hakuna
 
Naomba niwe tofauti na wachangiaji walio wengi.

1. Anakupenda sana.
2. Ana wivu sana kama mimi.
3. Kuna mambo madogo madogo ameyakuta hapo kwako yakamtia wivu akahisi uko na mtu mwingingine japo wewe unaweza kuyaona ya kawaida.
4. Hukuonyesha kumbembeleza, kumpetipeti badala yake ukanunua minyama, mikuku n.k
5. Swali: Alivyokuja ulimpa muda wako wa kutosha au ulikuwa busy na movies, kuangalia mpira n.k?

NB: Wanawake wakikosa kubembelezwa, show ikiwa kama ya Yanga msimu uliopita, usipompa attention akija kwako wanakuwaga na HASIRA, BITTER.

Pia ULISIKIA WAPI MAPENZI YASIYO NA MISUKOSUKO KIDOGO?
Mmmmh

Haki umemtia moyo mkaka wa watu
 
Acha tuu.. Hela ndo kila kituu haya maishaa...!! Kaza unavyowezaa huna helaa wee falaa tuu
Ndo wanaume wengi eti wanaamini hivo

Eti umpelekee moto mpaka azimie ndo hakuachi

Wanawake maboroo sio kivile kama wanaume, wanawake wanapenda mwanaume mwenye hela ili kumaliza shida zao, eg kupiga pamba, kupendeza in a whole matter ni mwendo wa kushindana na wenzie, hamna la zaidi ya umahiri dhidi ya mwenzie ( competence)
 
Moja kwa moja kwenye mada

Mimi na mpenzi wangu tuna miezi mitano sasa!! Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti

Tulikutana Dar, nikiwa nafuatilia mishemishe flani hivi, na yeye huko ndio kwao, ila kwa sasa yupo mkoa mwingine!!

Kwa kweli baada ya kuonana, nilimuelewa sana, hata yeye alinipenda mno. Mpaka tukafikia stage ya kutambulishana kwa watu wetu wa karibu. Binafsi niliamini hapo mke nishapata!!

Nikaanza kumshirikisha mipango ya jinsi ya kufanikisha kuishi pamoja, yaani kurasimishwa kama mke na mume!!

Nilimuambia, ngoja nijipange vizuri, ili mwezi wa kumi nambili katikati, nikajitambulishe kwao!! Alifurahi sana!!

Sasa, katikati hapo, alinitembelea huku nilipo, na alifurahi sana kwa jinsi nilivompokea, na nilimkarimu kwelikweli, kama wife to be!!

Mara baada ya kurudi kwao, kwa kweli amebadilika sana!! Ana hasira, na gubu balaa!!

Yaani anaweza asinitafute hata wiki nzima, na nikimtafuta anajibu kwa ukali, na kwa kifupi sana!! Naweza tuma text whatsapp, na asijibu au akajibu kwa kuchelewa sana, tena shortcut

Na sasa ana mtindo, nikimpigia, tukiongea kidogo tu ananikatia simu!! Kwa kweli kitendo hicho kinanikera sana, na ninahisi ananidharau mno!!

Kwa kweli sielewi ni kipi kinachoendelea upande wake!!

Nilijaribu kumpigia tuzungumze, lakini alikuwa mkali balaa, na eti hataki kuzungumzia mambo hayo!! Akakata simu!!

Jamani hebu naombeni mnishauri, au mwenzangu atakuwa huko ashapata mwingine!!

Sio kwamba siwezi, lakini sikutaka kabisa kuachana naye kwa kuwa, sikutaka tena kutafuta mwanamke mwingine wa kuona, kwa sababu kwangu hiyo ni kazi kubwa sana!!

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu!!
Kuna jambo kakusoma alipokuja kukutembelea akaona kumbe alikua anapotea
 
Usisahau kuleta mrejesho kwa maushauri iliopata ili nawengine wajifunze.sawa dogo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom