Mpenzi wangu amebadilika ghafla

Mpenzi wangu amebadilika ghafla

Moja kwa moja kwenye mada

Mimi na mpenzi wangu tuna miezi mitano sasa!! Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti

Tulikutana Dar, nikiwa nafuatilia mishemishe flani hivi, na yeye huko ndio kwao, ila kwa sasa yupo mkoa mwingine!!

Kwa kweli baada ya kuonana, nilimuelewa sana, hata yeye alinipenda mno. Mpaka tukafikia stage ya kutambulishana kwa watu wetu wa karibu. Binafsi niliamini hapo mke nishapata!!

Nikaanza kumshirikisha mipango ya jinsi ya kufanikisha kuishi pamoja, yaani kurasimishwa kama mke na mume!!

Nilimuambia, ngoja nijipange vizuri, ili mwezi wa kumi nambili katikati, nikajitambulishe kwao!! Alifurahi sana!!

Sasa, katikati hapo, alinitembelea huku nilipo, na alifurahi sana kwa jinsi nilivompokea, na nilimkarimu kwelikweli, kama wife to be!!

Mara baada ya kurudi kwao, kwa kweli amebadilika sana!! Ana hasira, na gubu balaa!!

Yaani anaweza asinitafute hata wiki nzima, na nikimtafuta anajibu kwa ukali, na kwa kifupi sana!! Naweza tuma text whatsapp, na asijibu au akajibu kwa kuchelewa sana, tena shortcut

Na sasa ana mtindo, nikimpigia, tukiongea kidogo tu ananikatia simu!! Kwa kweli kitendo hicho kinanikera sana, na ninahisi ananidharau mno!!

Kwa kweli sielewi ni kipi kinachoendelea upande wake!!

Nilijaribu kumpigia tuzungumze, lakini alikuwa mkali balaa, na eti hataki kuzungumzia mambo hayo!! Akakata simu!!

Jamani hebu naombeni mnishauri, au mwenzangu atakuwa huko ashapata mwingine!!

Sio kwamba siwezi, lakini sikutaka kabisa kuachana naye kwa kuwa, sikutaka tena kutafuta mwanamke mwingine wa kuona, kwa sababu kwangu hiyo ni kazi kubwa sana!!

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu!!
Watu mna shida. hivi huoni umekataliwa mkuu. kagundua huna future
 
Mkuu kula vizuri, sali sana, tafua hela kwa nguvu zote, fanya mazoezi halafu uache kujipa umuhimu kwenye maisha ya watu wengine

Thank me later
Asante ndugu yangu kwa ushauri kuntu!
 
Moja kwa moja kwenye mada

Mimi na mpenzi wangu tuna miezi mitano sasa!! Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti

Tulikutana Dar, nikiwa nafuatilia mishemishe flani hivi, na yeye huko ndio kwao, ila kwa sasa yupo mkoa mwingine!!

Kwa kweli baada ya kuonana, nilimuelewa sana, hata yeye alinipenda mno. Mpaka tukafikia stage ya kutambulishana kwa watu wetu wa karibu. Binafsi niliamini hapo mke nishapata!!

Nikaanza kumshirikisha mipango ya jinsi ya kufanikisha kuishi pamoja, yaani kurasimishwa kama mke na mume!!

Nilimuambia, ngoja nijipange vizuri, ili mwezi wa kumi nambili katikati, nikajitambulishe kwao!! Alifurahi sana!!

Sasa, katikati hapo, alinitembelea huku nilipo, na alifurahi sana kwa jinsi nilivompokea, na nilimkarimu kwelikweli, kama wife to be!!

Mara baada ya kurudi kwao, kwa kweli amebadilika sana!! Ana hasira, na gubu balaa!!

Yaani anaweza asinitafute hata wiki nzima, na nikimtafuta anajibu kwa ukali, na kwa kifupi sana!! Naweza tuma text whatsapp, na asijibu au akajibu kwa kuchelewa sana, tena shortcut

Na sasa ana mtindo, nikimpigia, tukiongea kidogo tu ananikatia simu!! Kwa kweli kitendo hicho kinanikera sana, na ninahisi ananidharau mno!!

Kwa kweli sielewi ni kipi kinachoendelea upande wake!!

Nilijaribu kumpigia tuzungumze, lakini alikuwa mkali balaa, na eti hataki kuzungumzia mambo hayo!! Akakata simu!!

Jamani hebu naombeni mnishauri, au mwenzangu atakuwa huko ashapata mwingine!!

Sio kwamba siwezi, lakini sikutaka kabisa kuachana naye kwa kuwa, sikutaka tena kutafuta mwanamke mwingine wa kuona, kwa sababu kwangu hiyo ni kazi kubwa sana!!

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu!!
Tatizo lako ongea na mahera wa nec
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom