Mpenzi wangu amebadilika ghafla

Mpenzi wangu amebadilika ghafla

Naomba niwe tofauti na wachangiaji walio wengi.

1. Anakupenda sana.
2. Ana wivu sana kama mimi.
3. Kuna mambo madogo madogo ameyakuta hapo kwako yakamtia wivu akahisi uko na mtu mwingingine japo wewe unaweza kuyaona ya kawaida.
4. Hukuonyesha kumbembeleza, kumpetipeti badala yake ukanunua minyama, mikuku n.k
5. Swali: Alivyokuja ulimpa muda wako wa kutosha au ulikuwa busy na movies, kuangalia mpira n.k?

NB: Wanawake wakikosa kubembelezwa, show ikiwa kama ya Yanga msimu uliopita, usipompa attention akija kwako wanakuwaga na HASIRA, BITTER.

Pia ULISIKIA WAPI MAPENZI YASIYO NA MISUKOSUKO KIDOGO?
 
Alipo kuja kukutembelea ulifanya nae mapenzi? Kama ndio basi ulimuonea huruma kama ndugu yako,Pili kaona una maisha ya kawaida kakukimbia huyo
 
Unaeza kuwa na mpenzi Mwalimu ila jua mapenzi hayana Shule mkuu.
 
Moja kwa moja kwenye mada

Mimi na mpenzi wangu tuna miezi mitano sasa!! Mimi na yeye tunaishi mikoa tofauti

Tulikutana Dar, nikiwa nafuatilia mishemishe flani hivi, na yeye huko ndio kwao, ila kwa sasa yupo mkoa mwingine!!

Kwa kweli baada ya kuonana, nilimuelewa sana, hata yeye alinipenda mno. Mpaka tukafikia stage ya kutambulishana kwa watu wetu wa karibu. Binafsi niliamini hapo mke nishapata!!

Nikaanza kumshirikisha mipango ya jinsi ya kufanikisha kuishi pamoja, yaani kurasimishwa kama mke na mume!!

Nilimuambia, ngoja nijipange vizuri, ili mwezi wa kumi nambili katikati, nikajitambulishe kwao!! Alifurahi sana!!

Sasa, katikati hapo, alinitembelea huku nilipo, na alifurahi sana kwa jinsi nilivompokea, na nilimkarimu kwelikweli, kama wife to be!!

Mara baada ya kurudi kwao, kwa kweli amebadilika sana!! Ana hasira, na gubu balaa!!

Yaani anaweza asinitafute hata wiki nzima, na nikimtafuta anajibu kwa ukali, na kwa kifupi sana!! Naweza tuma text whatsapp, na asijibu au akajibu kwa kuchelewa sana, tena shortcut

Na sasa ana mtindo, nikimpigia, tukiongea kidogo tu ananikatia simu!! Kwa kweli kitendo hicho kinanikera sana, na ninahisi ananidharau mno!!

Kwa kweli sielewi ni kipi kinachoendelea upande wake!!

Nilijaribu kumpigia tuzungumze, lakini alikuwa mkali balaa, na eti hataki kuzungumzia mambo hayo!! Akakata simu!!

Jamani hebu naombeni mnishauri, au mwenzangu atakuwa huko ashapata mwingine!!

Sio kwamba siwezi, lakini sikutaka kabisa kuachana naye kwa kuwa, sikutaka tena kutafuta mwanamke mwingine wa kuona, kwa sababu kwangu hiyo ni kazi kubwa sana!!

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu!!
Cha kufanya na wewe mpotezee lkn usimtangazie kumuacha Bali we move on, usimpigie usimtext na ukiweza namba yake futa maana anaonekana kapata mwenye fedha zaidi yako na kama tujuavyo kwamba wanawake Wa sasa wanaamini mwanaume mwenye ela zaidi ndio husband material. Kwahyo asikuumize just move on.
 
Sasa fanya hivi...

Kuanzia leo usimtumie text wala kumpigia mpaka yeye akutafute asipokutafuta ndo ujue mwisho umefika.

Na akikutafuta usimshobokee, kuwa normal maana ukimshobokea imekula kwako.

Kuna swali umeulizwa hapo juu naona unalikimbia, je ulikula mzigo?
Halijala hili, limezubaa hivyo
 
IMENIBIDI NIANDIKE KWA HERUFI KUBWA ILI UNIELEWE KWANZA KABLA YA YOTE POLE SANA BROO

Ila naomba niende direct kwenye mada ikoo hivi wanawake ni watu wenye mambo mengi sana lazima usipowaelewa wataakumiza kichwa sana sasa naomba nikupe FALSAFA NANE kuhusu wanawake ukiona amefikia stage AMEBADILIKA GHAFLA unatakiwa ufahamu FALSAFA NANE

1.falsafa ya kwanza mwanamke anapokubadilikia inaonesha kuna jambo amekupigia kelele sana ubadilike lakini hubadiliki mpka kachoka

2.falsafa ya pili kuna mazingira mapya amekutana nayo sasa anaona wewe unampotezea muda

3.falsafa ya tatu anatingisha kibiriti wanawake always wanapenda kutingisha vibiriti jambo dogo wanalifanya kubwa ili akuone utachukua hatua Gani

4.falsafa ya nne kuna mtu amekutana nae kiuchumi yupo stable kuliko wewe na anataka kutia nia sasa wewe unaonekana kama kikwazo kwake

5.falsafa ya tano nguvu za njee inawezekana kabisa wazazi,marafiki au ndugu wamekaa nae na kumshauli aachane na wewe wanaona unampotezea muda wake

6.falsafa ya Sita mwanamke ameanza kupatwa na hofu kuna Dalili za wewe utamuacha uko mbali utamwacha

NINI CHA KUFANYA

ninachokushauli fanya ufanyavyo ukutane nae uso kwa uso mzungumze katika mazungumzo yenu hapo ndipo utapata picha kamili

Pia nakukumbusha don’t be hash to her ukiona amefika hatua hataki kuonana na wewe just be cool usichukue maamuzi kaa chini utulie
Huu ndo ushauri sasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom